picture

WELCOME

Wednesday, February 16, 2011

Tanzania wananchi masikini viongozi matajiri KIONGOZI HUWEZI SEMA NCHI NI MASIKINI NAUNAGUSWA NA UMASIKINI WA WANANCHI WAKO huku wewe ukitumia ndege aina ya Gulfstream 550..yenye thamani ya bilioni zaid ya 40 namawaziri wako wakitumia V8 prince yenye thamani ya milioni 280 kwakila moja bado wabunge mashangingiya landcruisa ya milioni zaidi ya 80 shule mbovu dawahakuna HOSPITALINI umeme taabu DOWANS uchumi hovyo mfumkowabei juu..!!..

MAGARI YA AINA HII V8 PRINCE MOJA LIKIUZWA KWA BEI YA MILIONI 280 magari ya aina hii kwanchi masikini NIDHULUMA NA UNYONYAJI NA UBEBERU UBWANYENYE wanao fanyiwa watu watabaka la chini  kwenye nchi nyingi za kiafrica NAAMINI  MATUMIZI YA MAGARI HAYA YANAEPUKIKA NA FEDHA HIZI ZAKUNUNULIA MAGARI ZINAWEZA KUHAMISHIWA KWENYE MIRADI MINGINE YAMAENDELEO  tena  hata mawaziri wanaweza kusafiriswa kwa basi moja toka dar hadi dodo au kokote waendako kwajili ya shuguli za kiserekali VILEVILE  HATA WABUNGE WANAWEZA KUSAFIRISWA KWAKUTUMIA MABASI nasio kila mbunge anunuliwe gari lake dereva wake mafuta apewe HII NIDHULUMA umasikini wetu mtaji wao viongozi wabadhirifu..!!..
 MAGARI YA AINA HII V8 PRINCE MOJA LIKIUZWA KWA BEI YA MILIONI 280 magari ya aina hii kwanchi masikini NIDHULUMA NA UNYONYAJI NA UBEBERU UBWANYENYE wanao fanyiwa watu watabaka la chini  kwenye nchi nyingi za kiafrica NAAMINI  MATUMIZI YA MAGARI HAYA YANAEPUKIKA NA FEDHA HIZI ZAKUNUNULIA MAGARI ZINAWEZA KUHAMISHIWA KWENYE MIRADI MINGINE YAMAENDELEO  tena  hata mawaziri wanaweza kusafiriswa kwa basi moja toka dar hadi dodo au kokote waendako kwajili ya shuguli za kiserekali VILEVILE  HATA WABUNGE WANAWEZA KUSAFIRISWA KWAKUTUMIA MABASI nasio kila mbunge anunuliwe gari lake dereva wake mafuta apewe HII NIDHULUMA umasikini wetu mtaji wao viongozi wabadhirifu..!!..
 HUWEZI SEMA UNAGUSWA NA UMASIKINI WA watanzania huku ukitumia V8 prince ya milioni 280 za kitanzania na mwingine akitumia ndege ya bilioni 40 ..!!..
 waheshimiwa wakishangaa nyumba zawapiga kura wao kana kwamba nimapango ya fisi NAPATA TAABU KUSEMA VIONGOZI WATANZANIA WANAGUSWANA UMASIKINI wawananchi wao ..!!..
 MAGARI YA AINA HII V8 PRINCE MOJA LIKIUZWA KWA BEI YA MILIONI 280 magari ya aina hii kwanchi masikini NIDHULUMA NA UNYONYAJI NA UBEBERU UBWANYENYE wanao fanyiwa watu watabaka la chini  kwenye nchi nyingi za kiafrica NAAMINI  MATUMIZI YA MAGARI HAYA YANAEPUKIKA NA FEDHA HIZI ZAKUNUNULIA MAGARI ZINAWEZA KUHAMISHIWA KWENYE MIRADI MINGINE YAMAENDELEO  tena  hata mawaziri wanaweza kusafiriswa kwa basi moja toka dar hadi dodo au kokote waendako kwajili ya shuguli za kiserekali VILEVILE  HATA WABUNGE WANAWEZA KUSAFIRISWA KWAKUTUMIA MABASI nasio kila mbunge anunuliwe gari lake dereva wake mafuta apewe HII NIDHULUMA umasikini wetu mtaji wao viongozi wabadhirifu..!!..

UMASIKINI UMEWATAFUNA WAZEE WETU AMBAO NDIO HAZINA YA TAIFA  wengine hufa wakiwa na halimbaya ya kimaisha njaa maradhi umasikini wakutisha makaazi duni hata sehemu ya kulala nimajunia na ngozi.NAUCHUKIA UMASIKINI HUU WAKUPANDIKIZWA na viongozi wasio waaminifu kwa taifa letu la tanzania.!!..


FIKA UJIONEE ndege zinavyo tua na kuondoka maeneo yanayo chimbwa dhahabu na wawekezaji nchini tanzania KISHA UFANANISHE NA WATANZANIA WANAO ISHI MAENEO YANAYO CHIMBWA DHAHABU HII NA wawekezaji najiuliza umasikini wa mtanzania upo wapina ninani chanzo je ipo siku utaodoka kabisa..!!??

Tuesday, February 15, 2011

TANZANIA WATAALAMU wakifanya kazi zao na sio wanasiasa kufanya kazi zakitaalamu TANZANIA itasongambele Leo utasikia MIGOMO YA DALADALA KESHO MIGOMO YA MADAKTARI KESHO KUTWA MIGOMO YA WAHADHIRI MTONDOGOO MIGOMO YA WAFANYAKAZI RELI NA WAFANYAKAZI WAVIWANDANI MARA WATUMISHI WA SEREKALI.kilakukicha WANASIASA wanachafua TAALUMA.!."Mtu asiye makini katika mambo madogo madogo hawezi kuwa makini hata katika mambo makubwa."

 BIASHARA YA KUKUSANYA CHUPA hii niajira tanzania..!!..
BIASHARA YA MKAA NA KUNI ZA KUPIKIA huyu nae amejiajiri hii ndio kazi yake MAISHA HAYANA KANUNI ..!!..
YOTE NJAA KAMA KINAVYO SOMEKA  chombo kilicho beba samaki za huyo mama UMASIKINI haukubaliki ..!!..
FOLENI YA CHAKULA jiulize asilimia %50ya watanzania niwatoto chini ya miaka 18 je ? wote wanakula wanashiba..!!..
UGALI HUU NIMAARUFU SANA MIKOA YA KANDA YA ZIWA  UGALI WAMTAMA NA UDAGA..niwangapi wanakula na kushiba tanzania..!!..
UGALI HUU NIMAARUFU SANA MIKOA YA KANDA YA ZIWA  UGALI WAMTAMA NA UDAGA..niwangapi wanakula na kushiba tanzania..!!..
UGALI HUU NIMAARUFU SANA MIKOA YA KANDA YA ZIWA  UGALI WAMTAMA NA UDAGA..niwangapi wanakula na kushiba tanzania..!!..

BIASHARA NDOGO NDOGO vitadhidi ya umasikini ..!!..
 

MIMI NIMESOMESHWA KWA KILIMO, NAKIHESHIMU SAAANA KILIMO CHA JEMBE.LA MKONO.itakua vipi wakulima wakigoma!!.
MIMI NIMESOMESHWA KWA KILIMO, NAKIHESHIMU SAAANA KILIMO CHA JEMBE.LA MKONO.itakua vipi wakulima wakigoma!!.
MIMI NIMESOMESHWA KWA KILIMO, NAKIHESHIMU SAAANA KILIMO CHA JEMBE.LA MKONO.itakua vipi wakulima wakigoma!!.
NAFURAHIA MAZAO YA mifugo kama nyama maziwa samadi ngozi na pembe lakini sio watanzania wote wanayamapa mazao haya ya mifugo na kuyatumia ipaswavyo kutumika ..!!..
NAFURAHIA MAZAO YA mifugo kama nyama maziwa samadi ngozi na pembe lakini sio watanzania wote wanayamapa mazao haya ya mifugo na kuyatumia ipaswavyo kutumika ..!!..
NAFURAHIA MAZAO YA mifugo kama nyama maziwa samadi ngozi na pembe lakini sio watanzania wote wanayamapa mazao haya ya mifugo na kuyatumia ipaswavyo kutumika ..!!..
NAFURAHIA MAZAO YA mifugo kama nyama maziwa samadi ngozi na pembe lakini sio watanzania wote wanayamapa mazao haya ya mifugo na kuyatumia ipaswavyo kutumika ..!!..
IPTL RICHIMOND SONGAS DOWANS .!!.
"Mtu asiye makini katika mambo madogo madogo hawezi kuwa makini hata katika mambo makubwa."
.NGUZO ZAUMEME shamba lipo mafinga nchini tanzania lakini hivi sasa mtanzania anatakiwa kulipia nguzo moja Tsh zaidi ya milioni moja ili kuweka umeme au kupata nishati ya umeme mita ya umeme zaidi ya laki nne zakitanzania najiuliza umeme nilini hautakua anasa badala yake umeme iweni bidhaa ya kutumika na kila mtu nchini tanzania nirahisi kumiliki kireti za bia sio rahisi kumiliki umeme au elimu bora na huduma nzuri za afya ..!!.."No nation has the right to make decisions for another nation; no people for another people."
Julius Kambarage Nyerere
IPTL RICHIMOND SONGAS DOWANS .!!.
"Mtu asiye makini katika mambo madogo madogo hawezi kuwa makini hata katika mambo makubwa."
.NGUZO ZAUMEME shamba lipo mafinga nchini tanzania lakini hivi sasa mtanzania anatakiwa kulipia nguzo moja Tsh zaidi ya milioni moja ili kuweka umeme au kupata nishati ya umeme mita ya umeme zaidi ya laki nne zakitanzania najiuliza umeme nilini hautakua anasa badala yake umeme iweni bidhaa ya kutumika na kila mtu nchini tanzania nirahisi kumiliki kireti za bia sio rahisi kumiliki umeme au elimu bora na huduma nzuri za afya ..!!.."No nation has the right to make decisions for another nation; no people for another people."
Julius Kambarage Nyerere
IPTL RICHIMOND SONGAS DOWANS .!!.
"Mtu asiye makini katika mambo madogo madogo hawezi kuwa makini hata katika mambo makubwa."
.NGUZO ZAUMEME shamba lipo mafinga nchini tanzania lakini hivi sasa mtanzania anatakiwa kulipia nguzo moja Tsh zaidi ya milioni moja ili kuweka umeme au kupata nishati ya umeme mita ya umeme zaidi ya laki nne zakitanzania najiuliza umeme nilini hautakua anasa badala yake umeme iweni bidhaa ya kutumika na kila mtu nchini tanzania nirahisi kumiliki kireti za bia sio rahisi kumiliki umeme au elimu bora na huduma nzuri za afya ..!!.."No nation has the right to make decisions for another nation; no people for another people."
Julius Kambarage Nyerere
IPTL RICHIMOND SONGAS DOWANS .!!.
"Mtu asiye makini katika mambo madogo madogo hawezi kuwa makini hata katika mambo makubwa."
.NGUZO ZAUMEME shamba lipo mafinga nchini tanzania lakini hivi sasa mtanzania anatakiwa kulipia nguzo moja Tsh zaidi ya milioni moja ili kuweka umeme au kupata nishati ya umeme mita ya umeme zaidi ya laki nne zakitanzania najiuliza umeme nilini hautakua anasa badala yake umeme iweni bidhaa ya kutumika na kila mtu nchini tanzania nirahisi kumiliki kireti za bia sio rahisi kumiliki umeme au elimu bora na huduma nzuri za afya ..!!.."No nation has the right to make decisions for another nation; no people for another people."
Julius Kambarage Nyerere
NILINI NYUMBA ZAAINA HII zitajengwa kama sehemu ya starehe ya mtu na sio makaazi ya watu masikini UMASIKINI WA WATANZANIA UNANI KERA NA KUNIUMIZA moyo wangu Eeemungu nifanye kuwa chombo cha mabadiliko katika nchi yangu ya tanzania NIONDOE UMASIKINI UJINGA NA MARADHI..!!..
WAKAAZI WAMWANZA WALIPO UMBANA NA ADHA YA USAFIRI BAADA YA DALADALA KUGOMA wakidai nauli iongezeke kutoka 250 hadi miatatu 300 kweli tanzania sasa nibalaa kila kona migomo NIISHARA YA KUUKATAA UMASIKINI hata askari wa usalama bara barani hawakuweza kuzuia watu kupanda gari kama hili nililo panda mimi jana baada ya kukosa usafiri jijini mwanza .NAJIULIZA ITAKUWAJE SIKU WAKULIMA WA JEMBE LA MKONO WAKIGOMA KULIMA MASHAMBA YAO NCHI TANZANIA njaa haitaliangamiza taifa hili ikiwa UMEME tu NA MAJI TUMESHINDWA kuyapatia ufumbuzi.!!.                                                                                                                                                WAKAAZI WAMWANZA WALIPO UMBANA NA ADHA YA USAFIRI BAADA YA DALADALA KUGOMA wakidai nauli iongezeke kutoka 250 hadi miatatu 300 kweli tanzania sasa nibalaa kila kona migomo NIISHARA YA KUUKATAA UMASIKINI hata askari wa usalama bara barani hawakuweza kuzuia watu kupanda gari kama hili nililo panda mimi jana baada ya kukosa usafiri jijini mwanza .NAJIULIZA ITAKUWAJE SIKU WAKULIMA WA JEMBE LA MKONO WAKIGOMA KULIMA MASHAMBA YAO NCHI TANZANIA njaa haitaliangamiza taifa hili ikiwa UMEME tu NA MAJI TUMESHINDWA kuyapatia ufumbuzi.!!..

Sunday, February 6, 2011

MAISHA BORA KWA KILA MDANGA NYIKA .kwa...kasi zaidi nguvu zidi ari zaidi..

Mzee huyu fundi viatu akiwa kalala sijui ninjaa au nimawazo maisha magumu na hajapata mteja wakushona ndara au kiatu HUYU NIASKARI MPIGANAJI AKIPIGAVITA UMASIKINI UJINGA NA MARADHI silaha anayo tumia ni kushona viatu kama inavyo onekana kwenye picha hapo..!!..

SHIDA YA MAJI NDUGU ZANGU imesababisha baadhi ya ndoa kuvunjika hasa kutokana na upatikanaji mgumu wamaji maji pia yameathiri maisha ya familia nyingi kutokana wanawake kutumia mdamwingi kutafuta maji kuliko kufanya shuguli za kimaendeleo UMASIKINI NIJANGA LA KITAIFA NCHINI TANZANIA..!!..

UMASIKINI ULIOPO VIJIJINI NCHI TANZANIA UNAVYO WAAATHIRI watanzania watoto kwa wakubwa kweli UMASIKINI BADO TISHIO TANZANIA..!!..

Ukiwaangalia watoto hawa na mazingira waliopo utangundua ama niyatima au niwatoto wamoja ya familia masikini na waathirika wa janga la umasikini nchi tanzania  NITAUCHUKIA DAIMA  ujinga umasikini na maradhi NA NITAKUA WAKALA wakuwaangamiza maadui hawa nchini kwangu Tanzania.
 mama huyu  wa huko mkoani tabora yeye na familia yake umasikini ujinga na maradhi nimoja ya matatizo alio nayo katika familia yake UMASIKINI nijanga la kitaifa ndugu jamaa yangu rafiki yangu mtanzania mwenzangu nakuomba ukubali kushiriki katika vita DHIDI YA UMASIKINI TANZANIA
 Ukiwaangalia watoto hawa na mazingira waliopo utangundua ama niyatima au niwatoto wamoja ya familia masikini na waathirika wa janga la umasikini nchi tanzania  NITAUCHUKIA DAIMA  ujinga umasikini na maradhi NA NITAKUA WAKALA wakuwaangamiza maadui hawa nchini kwangu Tanzania.
maji tanzania tatizo lililo kosa ufumbuzi wa kudumu hebu angalia maji haya je ? nihalali yatumike na binadamu..!!..
angalia kijana huyu  HII NIISHARA KUWA hakuna anae ukubali umasikini nchini tanzania..!!..
 WAZEE na Walemavu watanzania nao hawaukubali umasikini hivyo wamebuni  mbinu ya kuomba omba angalau nao waweze kupiga vita umasikini UMASIKINI JANGA LA KITAIFA NCHINI TANZANIA..!!..
 Ukiwaangalia watoto hawa na mazingira waliopo utangundua ama niyatima au niwatoto wamoja ya familia masikini na waathirika wa janga la umasikini nchi tanzania  NITAUCHUKIA DAIMA  ujinga umasikini na maradhi NA NITAKUA WAKALA wakuwaangamiza maadui hawa nchini kwangu Tanzania.



 mwanamke huyu akiwa amepewa msaada na wasamaria wema ili kumwahisha hospitali UMASIKINI nijanga lisilo kubalika katika jamii yoyote
ZAHANATI zinahitajika vijijini nchini tanzania kote ziwena huduma bora wauguzi wakutosha maabara bora na zenye vifaa vya kisasa magari ya wagonjwa LAKINI NCHINI TANZANIA usishangae viongozi kujipongeza kwakupata nyadhifa wakiishi maisha ya kifahari huku watu wakifa kwakukosa dawa mahospitalini wajawazito wakifia njiani kutokana na ubali wa kituo cha afya shule zikiwa hazina vyooo walimu hawapo wakutosha majengo mabovu madawati hakuna vitabu hakuna na kila kanda na mtaala wake  AMAKWELI KUFA KUFAANA TANZANIA viongozi matajiri wananchi masikini wakutisha UMASIKINI WA TANZANIA janga la kupandikizwa NITAUCHUKIA UMASIKINI NA KUUPIGA VITA HADI TONE LA MWISHO LA DAMU YANGU nakataa umasikini ujinga na maradhi sio haki ya watanzania ..!!..

VIJANA NA VITA YA umasikini TANZANIA

 HAYUPO ANAE UFURAHIA UMASIKINI mwanadamu wa aina yoyote umri wowo mwenye akili timamu ukimuuliza anapenda nini hata siku moja usitarajie kupata jibu la mtu kupenda umasikini  NENO UMASIKINI niadui ambae  kila mwanadanu awe mzungu mwarabu mhindi hata mwafrica hamkubali na kumkaribisha na akiingia kokote mikakati ya kumwangamiza adu huyu umasikini huanza mara moja na vita hivyo huwa vya kudumu na hadi adui huyu aondoke UMASIKINI huzaa ujinga UMASIKINI huzaa maradhi
 HIKI NI KIWANDA CHA WAJASIRIA MALI WAHUNZI WA VIFAA MBALI MBALI kwajili ya matumizi ya nyumbani mfano majiko ya kupikia vikaangio masufuria makarai NIULINGO WA MAPAMBANO YA VITA DHIDI YA ADUI UMASIKINI..!!..
haya nimajiko ya kupikia yalio tengenezwa na vijana wajasiria mali jijini mwanza hapa niuwanja wa mapambano nivita kali ya umasikini HAYUPO ANAE MPOKEA KWA FURAHA NA KUKUBALI KUISHI NA ADUI UMASIKINI ..!!..
Fundi wa kutengeniza vikaangio vya kukaangia vitumbua..!!...kajiajiri akipiga vita umasikini

Thursday, February 3, 2011

HATA WATANZANIA WAKILA MAJANI NDEGE YA RAIS LAZIMA by Bazil pesambili mramba..!!....Ndege ya Rais aina ya Gulfstream 550

Ndege ya Rais aina ya Gulfstream 550..!!.HATA WATANZANIA WAKILA MAJANI NDEGE YA RAIS LAZIMA by  Bazil pesambili mramba..!!.Inauwezo wa kutua DAR, Mwanza, Zanzibar, KIA basi. Uwanja wa dodoma lazima uongezwe urefu ndo inaweza kutua.NDEGE aina ya Gulfstream 550 (pichani) iliyonunuliwa  na  serikali kwa Shilingi bilioni 40 kwa ajili ya  matumizi  ya  Rais  na kuleta utata na mjadala mkubwa miongoni mwa wananchi,Mara baada ya ndege hiyo kununuliwa enzi za utawala wa Rais wa awamu ya tatu, Benjamin Mkapa kuliibuka malalamiko kutoka kwa wadau mbalimbali ambao walisema ilinunuliwa kwa fedha nyingi ambazo zingeweza kutumika kwa maendeleo ya taifa hususan ujenzi wa shule, hospitali nk lakini hoja hizo zilipuuzwa.

TANZANIA VIONGOZI NA UTAJIRI WATANZANIA NA UMASIKINI UJINGA NA MARADHI ..!!..

HOSPITALI ZETU NA HUDUMA DUNIdawa hakuna vitanda vichache wahudumu wa afya wachache ..!!..





Kuvunjwa mkataba wa Dowans..!!..
Msingi wa kuvunjwa mkataba kati ya TANESCO na Dowans ni ushauri wa wanasheria kutoka kampuni ya Rex-Attorneys. Ni  Kampuni hii ya kisheria iliyonadiwa bungeni kuwa, imebobea katika masuala ya sheria za kimataifa.
Agosti 28, mwaka 2008, Waziri Mkuu wa Tanzania, Mizengo Pinda (mwanasheria kitaaluma) aliimwangia sifa kampuni ya Rex-Attorneys bungeni.
Waziri Mkuu alisema; “Kutokana na utata uliojitokeza katika mchakato mzima kuhusu mkataba baina ya TANESCO na Richmond uliotiwa saini tarehe 23 Juni 2006...”
“...Serikali kupitia TANESCO iliamua kufanyike mapitio ya mkataba huo na kupata ushauri wa kitaalamu kutoka kwa wanasheria waliobobea katika masuala ya mikataba ya kimataifa wa Kampuni ya Rex Attorneys.
Kwa mujibu wa Waziri Mkuu, uchunguzi wa Rex Attorneys ulibaini mambo matatu aliyoainisha kati ya mengi.
Mosi; manunuzi ya huduma ya umeme na kuingia mkataba na Richmond Development Company LLC ulikiuka Sheria ya Manunuzi wa Umma ya mwaka 2004.
Pili, kutokana na ukiukwaji huo, mkataba baina ya TANESCO na Richmond Development Company LLC, haukuwa halali na hauna nguvu kisheria.
Tatu, hata kama mkataba husika ungekuwa halali, uhamishaji (assignment) wa mkataba huo kutoka RDEVCO badala ya Richmond Development Company LLC kwenda Dowans Holdings S.A. na hatimaye Dowans Tanzania Limited, haukuwa halali.
Yatokanayo na kauli ya Waziri Mkuu
Maelezo hayo ya Waziri Mkuu yanaibua mengi. Kwanza, uamuzi wa kuvunja mkataba haukuwa wa kisiasa.
Si uamuzi uliotokana na shinikizo la kisiasa kama inavyopotoshwa bali ni uamuzi uliojengwa au kufikiwa kutokana na ushauri wa kisheria. Kwa mujibu wa Pinda, ni ushauri kutoka kwa wanasheria wabobeaji.
Pili, kwa kupambanisha hukumu ya Mahakama ya Kimataifa ya Kibiashara ya Usuluhishi na maelezo ya Waziri Mkuu hasa katika kuipa sifa za ‘kutukuka’ Rex-Attorneys, tunajikuta tukilazimika kuhoji suala moja kati ya mawili au yote mawili na kimsingi tukawa na haki ya kuanza kupuuza upande mmoja kama si pande zote.
Masuala hayo mawili ni pamoja na umakini wa serikali (Waziri Mkuu) hasa kutokana na kuinadi kampuni ya Rex-Attorneys au tuhoji uwezo wa Rex Attorneys.
Hapa izingatiwe ile kauli kuwa serikali “ina mkono mrefu” kama ingeweza kutafiti kwa umakini kama kweli hakuna maslahi binafsi yaliyopiganiwa ili kupiga kumbo maslahi ya nchi.
TANESCO imetakiwa sasa kuilipa Dowans mabilioni kwa kuvunja mkataba na kukataa kulipia huduma za kampuni hiyo kwa TANESCO katika kipindi cha mkataba.
Hukumu hii inatoka katika wakati ambao ushauri wa Rex-Attorneys (wazoefu wa mikataba ya kimataifa) ukiwa katika makabati ya TANESCO.
Fedha zimetumika kununua huduma ya ushauri wa kisheria kutoka Rex-Attorneys. Kampuni hiyo bila shaka, imelipwa mamilioni (kodi za wananchi). Bila shaka, katika kupima thamani ya matumizi ya fedha (value for money) malipo kwa Rex Attorneys ni kashfa.
Na kwa maana hiyo, hasara kwa taifa si tu malipo yatakayofanywa kwa Dowans bali hata kwa kampuni iliyotoa ushauri ‘tasa’ wa kisheria
MUHTASARI ( EXECUTI VE SUMMARY) WA TAARI FA YA
KAMATI TEULE I LI YOUNDWA NA BUNGE LA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANI A TAREHE 13 NOVEMBA, 2007 KUCHUNGUZA MCHAKATO WA ZABUNI YA UZALI SHAJI UMEME WA DHARURA ULI OI PA USHI NDI RI CHMOND
DEVELOPMENT COMPANY LLC YA HOUSTON, TEXAS,
MAREKANI MWAKA 2006
1.0 UTANGULI ZI
Mheshimiwa Spika, kwa mujibu wa Kanuni ya 119 ya Kanuni za
Kudumu za Bunge, Toleo la 2007, naomba kutoa taarifa ya Kamati
Teule ya Bunge iliyoundwa tarehe 13 Novemba, 2007 na Bunge hili
Tukufu kuchunguza mchakato wa zabuni ya uzalishaji umeme wa
dharura uliofanyika mapema mwaka 2006 na kuipa ushindi Richmond
Development Company LLC ya Houston, Texas, Marekani.
Mheshimiwa Spika, awali ya yote naomba kuchukua fursa hii kwa
niaba ya wajumbe wenzangu wa Kamati Teule kukupongeza wewe
binafsi na Bunge lako Tukufu kwa uamuzi wa kuunda kamati hii
maalum kwa lengo la kufanikisha utekelezaji wa majukumu ya
kikatiba ya Bunge katika kuisimamia na kuishauri Serikali na vyombo
vyake kwa niaba ya wananchi.
Mheshimiwa Spika, baada ya hoja ya kuundwa kwa Kamati Teule
kuwasilishwa na kuafikiwa na Bunge, uliwateua Wabunge watano
wafuatao kuunda Kamati Teule ya Bunge kwa mujibu wa Kanuni ya
104(3) ya Kanuni za Bunge, Toleo la 2004:
(a) Mhe. Dk. Harrison George Mwakyembe, Mb
(b) Mhe. Eng. Stella Martin Manyanya, Mb (c) Mhe. Mohamed Habib Juma Mnyaa, Mb (d) Mhe. Lucas Lumambo Selelii, Mb
(e) Mhe. Herbert James Mntangi, Mb
1.2 Hadidu za Rejea Mheshimiwa Spika, tarehe 15 Novemba, 2007 uliipa Kamati Teule siku thelathini kukamilisha kazi yake na Hadidu za Rejea zifuatazo kwa ajili ya kutekeleza kazi hiyo ya uchunguzi:
1. Kubainisha Richmond Development Company LLC ni kina nani, na
ni kampuni ya shughuli zipi na hivyo kupima uwezo wake kupatiwa zabuni ya kuleta nchini na kujenga mtambo wa umeme wa gesi wa MW 100;
2. Kutathmini mchakato mzima wa jinsi zabuni waliyoshinda
Richmond ilivyoshughulikiwa kuanzia Kamati ya Zabuni hadi mwisho
ili kujiridhisha kuwa sheria, taratibu, miiko na maadili ya zabuni
yanayotawala zabuni za aina hiyo vilifuatwa au vipi;
3. Kutathmini mkataba baina ya Richmond Development Company
LLC na TANESCO ili kujiridhisha kuhusu uhalali wa masharti ya
mkataba huo ukizingatia gharama na masharti mengine ukilinganisha
na masharti yaliyomo katika mikataba ya aina hiyo iliyoafikiwa na
TANESCO/ Serikali;
4. Kubainisha huduma na misaada mbalimbali waliyopewa Richmond
kama vile kufunguliwa Letter of Credit na kupima uhalali wake;
5. Kuziangalia na kuzitolea maoni taarifa za TAKUKURU, PPRA na
taarifa zozote nyingine zilizoangalia utaratibu wa zabuni ya
Richmond; na
6. Kuangalia mambo mengine yoyote yenye uhusiano na mchakato
mzima wa Richmond ili kutoa mapendekezo ya kuboresha taratibu za
zabuni kwa siku zijazo, kwa maslahi ya Taifa letu.
1.3 Utekelezaji wa Majukumu
Mheshimiwa Spika, kwa mujibu wa Kanuni ya 104(3) ya Kanuni za
Bunge, Toleo la mwaka 2004, wajumbe walinichagua kuwa
Mwenyekiti wa Kamati Teule. Aidha Mhe. Eng. Stella Manyanya (Mb)
alichaguliwa kuwa Makamu mwenyekiti wa Kamati. Nakuomba,
Mheshimiwa Spika, nitumie fursa hii ya awali kuwashukuru wajumbe
wa Kamati kwa imani kubwa waliyotuonyesha mimi na Mhe. Eng.
Manyanya ya kutuchagua kwa kauli moja kuiongoza Kamati Teule ya
Bunge.
Mheshimiwa Spika, Kamati Teule ilianza kazi yake mara moja kwa
kukusanya na kuzisoma nyaraka mbalimbali za msingi kama vile
Mkataba kati ya TANESCO na Richmond Development Company LLC,
Sheria ya Ununuzi wa Umma (Public Procurement Act) ya Mwaka
2004 na Kanuni zake za mwaka 2005, taarifa ya uchunguzi ya Taasisi
ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU), wakati huo
ikiitwa TAKURU, na taarifa ya Mamlaka ya Udhibiti na Ununuzi wa
Umma (Public Procurement Regulatory Authority-PPRA) kuhusu suala
hilo.
Vilevile, Kamati Teule ilianza kuandaa hati (summons) kwa mujibu wa
vifungu 13(1) na 14(1) na (2) vya Sheria ya Haki, Kinga na Madaraka
ya Bunge ya Mwaka 1988 (Sura ya 296) za kuita mashahidi
mbalimbali waliohusika kwa njia moja au nyingine katika mchakato
wa zabuni hiyo ya uzalishaji wa umeme wa dharura.
Mheshimiwa Spika, hadi kufikia tarehe 15 Disemba, 2007 jumla ya
mashahidi 46 walihojiwa na maswali 2061 kuulizwa. Pamoja na
Kamati Teule kutumia vyombo vya habari kuwatia moyo watu wenye
ushahidi kuhusu suala hili ili wajitokeze na kuieleza Kamati Teule,
hakuna shahidi hata mmoja aliyekuja kwa hiari yake mwenyewe bila
kupelekewa hati ya kuitwa. Aidha, mashahidi wote waliotuletea
maelezo kimaandishi kwa njia ya simu au barua, hawakuweka majina
yao wala anuani zao, hivyo kuipa Kamati Teule wakati mgumu
kufuatilia kauli zao.
Mheshimiwa Spika, matokeo haya yanaonesha hali halisi iliyopo
Tanzania, hali ya uoga na ya kutojiamini inayowakumba Watanzania
walio wengi wanapotakiwa kuelezea kwa uwazi maneno yale yale
wanayoyanong’ona pembeni kwa hamasa kubwa. Kwa mtindo huu
Taifa letu linaweza kuishia kuwa la walalamishi wasio na ujasiri wala
dhamira ya dhati ya kukemea maovu pale inapobidi.
Mheshimiwa Spika, mashahidi wengi walioitwa kwa hati hususan
kutoka TANESCO, Wizara ya Nishati na Madini, Wizara ya Fedha na
Wizara ya Katiba na Sheria walionyesha hofu, mashaka na hali ya
kutojiamini kwa kutoa majibu yaliyofanana ya kiitifaki-itifaki na
yaliyokosa mvuto na ushawishi wa kawaida mithili ya watu
walioketishwa pamoja na kukaririshwa hoja za kujibu. Wataalam wa
TANESCO, mathalan, waliikataa Richmond Development Company
LLC mara tatu wakati wa kutathmini zabuni ya umeme wa dharura,
kwa hoja za kitaalam kuwa haifai kwa vigezo vyote muhimu.
Walipofika mbele ya Kamati Teule, wakawa wapambe nambari moja
wa kampuni hiyo, wote wakiimba sifa za kulazimisha za kampuni
hiyo!
Aidha, nyaraka nyingi ambazo Kamati Teule ilizipata toka Serikalini na taasisi mbali mbali, zilikuwa nakala zilizokosa mtiririko wa kimasijala. Kamati Teule ilipodai nyaraka halisi kulinganisha na nakala ilizokuwa nazo, ilipewa majalada yaliyoonyesha dalili zote za kukarabatiwa.
Mheshimiwa Spika, hali hii ilijitokeza zaidi kwa TANESCO na Wizara
ya Nishati na Madini. Jalada halisi kutoka TANESCO lilichukua siku
tatu kuifikia Ofisi Ndogo ya Bunge likiwa na nyaraka zenye namba
zilizokosa mtiririko stahili. Wizara ya Nishati na Madini ndiyo iliyotia
fora kwa kumtuma Msaidizi wa Katibu Mkuu, Ndugu Julius Sarota
tarehe 18 Disemba 2007 akiwa na maagizo ya kuwafungulia
Wajumbe wa Kamati Teule kurasa maalum tu na si nyinginezo hivyo
kuinyima Kamati Teule mtiririko halisi wa mawasiliano. Kamati Teule
haikuridhishwa na utaratibu huo, hivyo ilimtaka Msaidizi huyo wa
Katibu Mkuu aondoke na majalada yake na kumpelekea hati ya
kuitwa Katibu Mkuu, Ndugu Arthur Mwakapugi afike yeye mwenyewe
na majalada hayo.
Tarehe 19 Disemba 2007 Katibu Mkuu huyo kwa maneno mengi na
ya kuzunguka alithibitisha kuwa alichokifanya Msaidizi wake yalikuwa
maelekezo ya Wizara. Kwa kuzingatia uhaba wa muda wa
kukamilisha kazi ya Kamati Teule na kwamba suala hilo tayari lilikuwa
limechukua siku tatu nzima za Kamati Teule, ugeni wa Katibu Mkuu
huyo katika Wizara hiyo na katika masuala ya Bunge na uwezekano
uliokuwepo kwa Kamati Teule kupata taarifa za ziada kupitia njia
nyingine, Kamati Teule iliamua kusonga mbele na kumuacha Katibu

Mkuu huyo na siri kubwa za Wizara yake.
Mheshimiwa Spika, ni kutokana na changamoto hizo Kamati Teule
ikaona kuwa ni vyema baadhi ya Wajumbe wake waende Houston,
Texas, Marekani ili kupata taarifa za kina na za ziada kuhusu suala
hilo. Kamati Teule inakushukuru sana Mhe. Spika kwa kuzielewa
changamoto zilizokuwa zinaikabili Kamati Teule na kuwawezesha
Wajumbe watatu kwenda Washington DC kukutana na maafisa wa
Ubalozi wetu, na Houston Texas kukutana na wamiliki wa Richmond
Development Company LLC.
Mheshimiwa Spika, wajumbe hao walioondoka Dar-es Salaam
kwenda Marekani tarehe 10 Disemba 2007 ni:
(a) Mhe. Eng. Stella Martin Manyanya, Mb
(b) Mhe. Lucas Lumambo Selelii, Mb
(c) Mhe. Mohamed Habib Juma Mnyaa, Mb, na
(d) Ndugu Anselm L. Mrema (Katibu wa Kamati)
Mheshimiwa Spika, tarehe 12 Disemba 2007 Kamati Teule ilikuandikia
barua kukuomba uiongezee muda kwa sababu kuu mbili: Kwanza,
Wajumbe watatu kati ya watano na Katibu wa Kamati Teule walikuwa
nchini Marekani kuanzia tarehe 10 Disemba 2007 kujiridhisha na
taarifa mbalimbali ambazo Kamati Teule ilizipata kuhusu Richmond
Development Company LLC. Kwa kuwa Wajumbe hao walikuwa
wanategemea kurejea nchini tarehe 15 Disemba 2007 siku ambayo
Kamati Teule ilitakiwa kuwasilisha taarifa yake na kwa kuwa taarifa
ambazo wangezipata Marekani zingetakiwa kuingizwa kwenye taarifa ya Kamati Teule na hata kubadilisha baadhi ya masuala katika taarifa hiyo, muda wa ziada ulihitajika.
Pili, baada ya uchambuzi wa kina wa ushahidi wa maandishi na wa
mdomo uliotolewa mbele ya Kamati Teule chini ya kiapo, Kamati
Teule iligundua kuwepo kwa mgongano wa ushahidi, hivyo kutia
mashaka juu ya dhamira ya baadhi ya mashahidi. Kamati Teule iliona
umuhimu wa kuwaita tena baadhi ya mashahidi kuthibitisha kauli
zao, na hata kuwachukulia hatua za kisheria baadhi yao ambao
wangeendelea kusema uongo chini ya kiapo ili kulinda heshima ya
Bunge.
Mheshimiwa Spika, uliuona umuhimu wa kuiongezea muda Kamati
Teule, hivyo tarehe 13 Disemba 2007 ukaridhia ombi la Kamati Teule
na kuweka tarehe 31 Disemba 2007 kuwa tarehe ya kuwasilisha
taarifa ya uchunguzi. Tunakushukuru sana kwa hatua hiyo.
Mheshimiwa Spika, hadi kufikia tarehe 31 Disemba 2007 siku
ilipowasilisha taarifa yake kwako, Kamati Teule ilikuwa imewahoji
jumla ya mashahidi 75 na kuuliza maswali 2717 na kuzipitia nyaraka
na kumbukumbu 104. Mashahidi 4 kati ya hao walikuja kwa hiari yao
bila kupelekewa hati za kuitwa. Mashahidi 7 waliitwa mara mbili.
Mashahidi wawili, Ndugu Daniel Yona na Mhe. Rostam Aziz, (Mb)
walipelekewa hati za kuitwa mbele ya Kamati Teule lakini hawakufika
kwa maelezo kwamba walikuwa nje ya nchi.
Mheshimiwa Spika, Ndugu Daniel Yona alitakiwa na Kamati Teule
atoe maelezo kuhusu msingi wa uamuzi wake wa kuipa Richmond
Development Company LLC, haki maalum ya kipekee (exclusive right)
ya miezi 18 kuhusu mradi wa Bomba la Mafuta kutoka Dar es Salaam
hadi Mwanza mwaka 2004 wakati huo akiwa Waziri wa Nishati na
Madini. Maelezo ya ziada ya mradi huu nitayatoa baadaye.
Mheshimiwa Spika, vilevile Mhe. Rostam Aziz alitakiwa atoe maelezo
kuhusu uhusiano wake na Kampuni za Richmond Development
Company LLC na Dowans Holdings S.A baada ya mashahidi kadhaa
kudai kuwa ana uhusiano nazo. Aidha, alitakiwa na Kamati Teule
aeleze kwa nini anwani ya barua pepe ya kampuni yake ya Caspian Construction Ltd ilitumiwa na Dowans. Kamati Teule ilitaka vilevile kupata ufafanuzi kutoka kwake kuhusu baadhi ya wafanyakazi wa kampuni yake wanaosemekana kuwa ni watumishi vilevile wa
Dowans Holdings S.A.
Mheshimiwa Spika, leo tunapowasilisha taarifa hii mbele ya Bunge
lako tukufu, tunajisikia kuutua mzigo mzito sana ulioanza kutuelemea
kutokana na kuzongwa kila kukicha na kila aina ya uzushi, uchochezi,
uchonganishi na hata vitisho. Tumezushiwa kuhongwa magari ya
kifahari na fedha taslimu; tumetuhumiwa kuendesha vita dhidi ya Waislamu na mara nyingine tuhuma hiyo ikageuka kuwa vita dhidi ya
Wakristo ndani ya Serikali; tumesingiziwa kuibadilisha taarifa yetu
mara mbili, baadhi wakisema kwa ushawishi wa fedha, wengine
wakidai kwa shinikizo la Mhe. Spika na wengine kwa shinikizo la
Waziri Mkuu; tumeshuhudia pilikapilika za usiku na mchana za
kujipanga na kuwashawishi baadhi ya Mawaziri na Wabunge kuikana
taarifa hii na mapendekezo yake kiasi cha wengine wetu kujiuliza:
kulikoni mtu asiye na hatia kuweweseka?
Mheshimiwa Spika, naomba kwa niaba ya wajumbe wenzangu wa
Kamati Teule, kukuhakikishia wewe binafsi na Bunge lako tukufu
kuwa tumekamilisha kazi tuliyopewa kwa uaminifu na ujasiri
mkubwa, dhamira safi, moyo wa uzalendo na kwa kumtanguliza
mbele Mwenyezi Mungu katika kila tulilolifanya. Tulichukua kila
tahadhari tusibanwe na mgongano wowote wa kimaslahi kiasi
kwamba mjumbe mwenzetu, Mhe. Eng. Stella Manyanya, mwajiriwa wa muda mrefu wa TANESCO ambaye alikuwa kwenye likizo isiyo na malipo, akaamua kukatisha ajira yake kwa kujiuzuru. Aidha,
tunakuhakikishia Mheshimiwa Spika kuwa hatukupokea senti tano ya
mtu wala baiskeli yake. Mwenye ushahidi tofauti, basi alithibitishie
Bunge hili tukufu. Mimi na wajumbe wenzangu wa Kamati Teule tuko
tayari kuwajibika kisiasa.
2.0 UKAME NA TATI ZO LA UZALI SHAJI UMEME NCHI NI
Mheshimiwa Spika, kwa takribani miaka mitatu mfululizo kuanzia
mwaka 2002 nchi yetu ilikumbwa na tatizo la ukosefu wa mvua za
kutosha. Athari za tatizo hilo hasa katika uzalishaji umeme, zilianza
kuonekana mwaka 2004, na kufikia mwishoni mwa mwaka 2005
ikawa dhahiri kwamba nchi ilikuwa inaelekea kwenye janga kubwa la
upungufu wa umeme. Mahitaji ya mitambo ya gesi ya kuzalishia
umeme wa dharura yakajitokeza.
Kutokana na hali hiyo, mwezi Disemba 2005 TANESCO iliiomba
Serikali kufikiria na kuidhinisha mpango wa kukodisha mitambo ya
kuzalisha umeme wa dharura kwa kutumia gesi kutoka kwenye
makampuni yanayofahamika kwa biashara hiyo chini ya Mikataba ya

kuuziana umeme kwa muda usiopungua miezi kumi na mbili.
Mheshimiwa Spika, tarehe 28 Disemba 2005 Serikali ilikubali ombi
hilo na kuiruhusu TANESCO kuwasiliana moja kwa moja na kampuni
ya SONGAS iliyopo nchini kuhusu mahitaji hayo ya dharura. Bila
kuchelewa TANESCO wakawasiliana na SONGAS ambayo ikaanza
mara moja kuandaa makisio ya mradi huo. Tarehe 11 Januari 2006,
CDC Globeleq, kampuni mama ya SONGAS, iliwasilisha TANESCO
makisio ya kukodisha mitambo ya gesi ya kuzalisha umeme wa MW 74 ambayo ingefungwa Ubungo na kuanza kuzalisha umeme katikati ya mwezi Aprili 2006.
Tarehe 13 Januari 2006 Bodi ya Zabuni ya TANESCO ilianza kujadili
zabuni hiyo ya CDC Globeleq na siku sita baadaye, yaani tarehe 19
Januari 2006, Bodi hiyo ikathibitisha mapendekezo ya zabuni hiyo na
kuingia katika majadiliano na CDC Globeleq. Tarehe 30 Januari, 2006
Bodi ya Zabuni ya TANESCO iliyakubali mapendekezo ya Kamati ya
Tathmini ya kuingia mkataba wa uzalishaji umeme kwa miaka mitano
au mitatu kama ifuatavyo: (i) miaka mitano kwa bei ya senti za
Kimarekani 3.2/ kWh; au (ii) miaka mitatu kwa bei ya senti za
Kimarekani 5.3/ kWh. Chini ya mpango huo, mitambo hiyo ya
kuzalisha umeme ingekuwa mali ya TANESCO baada ya kipindi cha
kukodi kumalizika.
Mheshimiwa Spika, taarifa hizi pamoja na mapendekezo ya Wizara ya
Nishati na Madini yaliwasilishwa na kujadiliwa katika Kikao cha Baraza
la Mawaziri cha tarehe 10 Februari 2006, yaani siku nne baada ya
kuanza mgao wa umeme kwa mikoa yote ya Tanzania Bara
inayounganishwa na Gridi ya Taifa. Pamoja na mambo mengine,
Baraza la Mawaziri liliweka msimamo wa Serikali wazi kuwa CDC
Globeleq ikubali kuiuzia Serikali mitambo yake au iikodishe Serikali
kwa bei ambayo Serikali ingeridhika nayo na siyo kwa kipindi cha
miaka mitano bali kipindi kile tu cha matatizo ya umeme kutokana na
ukame.
Hata hivyo, Mheshimiwa Spika, utekelezaji wa maamuzi ya Baraza la Mawaziri haukuwa makini. Kwani siku hiyo hiyo ya tarehe 10 Februari 2006, Wizara ya Nishati na Madini, badala ya kuwatumia ujumbe
sahihi CDC Globeleq kuwa Serikali inataka wabadilishe masharti yao
kama nilivyokwishaeleza, ikapeleka ujumbe tofauti kabisa kuwa
Serikali inafuta mpango wa kukodisha mitambo kutoka kwao.
Mheshimiwa Spika, pamoja na kumhoji aliyekuwa Waziri wa Nishati na Madini kipindi hicho Mhe. Dk. I brahim Msabaha, (Mb) na Katibu Mkuu wa Wizara hiyo Ndugu Arthur Mwakapugi kwa muda mrefu na katika siku nne tofauti, Kamati Teule ilishindwa kupata majibu ya
uhakika kwa maswali yake manne:
(i) Je, kulikuwa na kikao kingine cha Baraza la Mawaziri siku hiyo hiyo ya tarehe 10 Februari, 2006 kilichotengua maamuzi yake ya awali ya siku hiyo hiyo?
(ii) I kiwa jibu ni hapana, kwa nini Wizara ilipeleka CDC Globeleq
ujumbe tofauti na ule ulioagizwa na Baraza la Mawaziri?
(iii) Kwa nini Wizara isitume barua hiyo baada ya kushindwa
kuwashawishi CDC Globeleq kubadilisha masharti yao?
(iv) Maamuzi kama hayo, siku nne ndani ya mgao wa umeme wa nchi
nzima na katika kipindi ambacho Serikali haikuwa na mkakati
mbadala uliokuwa umeiva kama wa CDC Globeleq, hayo kweli
yalikuwa maamuzi makini ya kunufaisha Taifa?
Mheshimiwa Spika, kutokana na msimamo huo mpya wa Wizara,
TANESCO ikaachana na mpango wa kukodisha mitambo na kuelekeza
nguvu zake kwenye kununua mitambo mipya ya kuzalishia umeme.
Hivyo, tarehe 20 Februari 2006, TANESCO iliwasilisha kwa Katibu
Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini mpango wa ununuzi wa moja
kwa moja kutoka kwa watengenezaji wa mitambo ya kuzalishia
umeme wanaofahamika duniani chini ya utaratibu unaotambuliwa
kama international shopping chini ya Sheria ya Ununuzi wa Umma ya
mwaka 2004 na Kanuni zake.
Hatua hiyo ikafuatiwa na kikao cha Waziri wa Nishati na Madini na
watendaji wa Wizara na TANESCO tarehe 21 Februari 2006 ambacho
Waziri alikitumia kusisitiza kuwa mpango wa Serikali si kukodisha
mitambo bali kununua na kuiagiza TANESCO kutangaza zabuni mara moja. Waziri alitaka tangazo la zabuni lichapishwe magazetini siku ya Alhamisi tarehe 23 Februari 2006 na kuwapa TANESCO masharti
yafuatayo:
(i) zabuni ifunguliwe baada ya siku 10 (yaani tarehe 6 Machi 2006);
(ii) tathmini ya zabuni ifanyike kwa siku mbili (tarehe 7 - 8 Machi
2006).
2.1 Maandalizi ya Zabuni
Mheshimiwa Spika, tarehe 22 Februari 2006 TANESCO iliomba idhini
ya Mamlaka ya Udhibiti wa Ununuzi wa Umma (PPRA) kutangaza
zabuni hiyo kwa muda wa siku 10 badala ya siku 45 zinazoainishwa
katika Kanuni za Ununuzi. Tarehe hiyo hiyo ya 22 Februari 2006,
PPRA ikaijibu TANESCO kwa kuitahadharisha kuwa utaratibu huo
utakuwa kinyume cha taratibu na Kanuni za ununuzi. Muda wa siku
10 hautoshi kuitisha zabuni ya kimataifa na kuweza kupata wazabuni
wenye sifa zinazohitajika.
Mamlaka ikaishauri TANESCO kuwa badala ya kutumia njia ya
kutangaza zabuni ya kimataifa (international competitive tendering)
itumie njia mbadala ya ununuzi wa kimataifa (international shopping)
ambapo makampuni mengi yanayotengeneza mitambo ya kuzalisha
umeme yanaalikwa na “kuyashindanisha kwa kuyaomba yawasilishe
zabuni zao badala ya kutangaza kwani utaratibu huo ungesaidia
kuondoa makampuni ya kati yasiyohusika na uzalishaji umeme”.
Mheshimiwa Spika, tarehe hiyo hiyo 22 Februari, 2006 TANESCO
ikaiarifu Wizara kuhusu ushauri wa PPRA. Wizara ikaukataa na
kuiagiza TANESCO kutekeleza agizo la Waziri bila kukosa kwa
kuitangaza zabuni hiyo. Zabuni hiyo ikatangazwa kwa utaratibu wa
ndani tarehe 23 Februari 2006. Hatua hiyo iliishitua PPRA ambayo
iliiandikia barua TANESCO kuelezea kushangazwa kwake na hatua ya
shirika hilo kukaidi ushauri wa kitaalamu na wa kisheria. PPRA
ikasisitiza kuwa, njia pekee kwa TANESCO kupata wazabuni wazuri
na wenye sifa stahili katika kipindi kifupi ni kutumia utaratibu
ilioupendekeza wa international shopping.
Mheshimiwa Spika, hali ya uzalishaji umeme nchini iliendelea kuwa
tete na kulazimu kikao cha Baraza la Mawaziri kufanyika tarehe 23
Februari 2006, na kuagiza utaratibu wa haraka (fast track) wa kukodi
mitambo ya kuzalishia umeme wa dharura ufanyike. Katika
kutekeleza maamuzi hayo, Baraza liliagiza kuwa Sheria ya Ununuzi
wa Umma ya mwaka 2004 na Kanuni zake za mwaka 2005
zizingatiwe. Pamoja na msisitizo huo wa Baraza la Mawaziri, Wizara
ya Nishati na Madini ikaendelea kuishinikiza TANESCO kufuata
maagizo ya Wizara na si vinginevyo.
Mheshimiwa Spika, TANESCO ikionyesha dhahiri kusukumwa tu na
Wizara, ikaiandikia tena PPRA Jumapili tarehe 26 Februari 2006
kuelezea kuwa sasa imeagizwa na Serikali kuitangaza zabuni hiyo
magazetini, hivyo mamlaka hiyo ya udhibiti wa ununuzi wa umma
itoe idhini ya kutangaza zabuni ya kimataifa kwa siku chache kuliko
zilizowekwa na sheria. TANESCO huku ikijua kabisa kuwa PPRA
isingeweza kuipata na kuijibu barua hiyo Jumapili, ikatangaza zabuni
hiyo magazetini tarehe 27 Februari 2006 na kuwataka wazabuni
wawasilishe zabuni zao tarehe 6 Machi 2006 yaani siku 10 baada ya
kuchukua nyaraka za zabuni tarehe 24 Februari 2006.
Tarehe 1 Machi 2006 PPRA ikaijibu TANESCO kuwa pamoja na
kuendelea na zabuni hiyo, isingekuwa rahisi kwa Shirika hilo la
umeme la Taifa kupata mzabuni anayefaa katika kipindi hicho kifupi
cha siku 10. Hata hivyo PPRA ikaitaka TANESCO kuufuatilia utaratibu
mzima wa zabuni hiyo kwa karibu ili kuhakikisha kuwa taratibu
zinafuatwa, ili kuepusha malamiko yasiyo ya msingi kutoka kwa
wazabuni.
Mheshimiwa Spika, pamoja na kuipongeza PPRA kwa kuonyesha
subira ya hali ya juu, uwazi na ukweli wa kitaaluma, Kamati Teule
ilishindwa kubaini moja kwa moja chanzo cha ujasiri wa kiburi ndani
ya Wizara ya Nishati na Madini kiasi cha kupindisha maamuzi ya
Baraza la Mawaziri kama tulivyoona na kukaidi ushauri wa Mamlaka
iliyowekwa kisheria. Aidha Kamati Teule ilishangazwa na Ofisi ya
Waziri Mkuu iliyokuwa ikifuatilia kwa karibu sana mchakato huo,
kushindwa kukemea ukaidi huo wa Wizara ya Nishati na Madini.
2.2 Mchakato wa Zabuni ndani ya TANESCO
Mheshimiwa Spika, hadi muda wa zabuni ulipoongezwa, yaani tarehe
20 Machi 2006, jumla ya wazabuni ishirini na sita (26) walinunua
nyaraka za zabuni zilizouzwa kwa fedha isiyorejesheka (non
refundable) ya Dola za Kimarekani 100. Ni wazabuni wanane (8) tu
ndio waliorudisha nyaraka za zabuni hiyo kama ifuatavyo:
(i) M/ S Aggreko International Projects Ltd ya Uarabuni,
(ii) M/ S Quantus ya Ujerumani,
(iii) M/ S APGUM Co. Ltd ya Ujerumani,
(iv) M/ S Globeleq Ltd ya Kanada,
(v) M/ S Real Energy Projects ya Uingereza,
(vi) M/ S Renco SPA ya I talia,
(vii) M/ S Richmond Development Company LLC ya Marekani, na
(viii) M/ S GAPCO(T) Ltd ya Tanzania.
Mheshimiwa Spika, zabuni zikafunguliwa na wazabuni wote wanane
waliorudisha nyaraka zao za zabuni waliwakilishwa kwenye ufunguzi.
TANESCO ikaunda Kamati ya Kutathmini Zabuni iliyokuwa na
wajumbe 12, kati yao wanane walitoka TANESCO, wawili kutoka
kampuni ya ushauri ya Lahmeyer I nternational, mmoja kutoka Wizara
ya Fedha na mwingine Wizara ya Nishati na Madini. Kamati hiyo
ilipewa wiki moja tu kumaliza kazi yake na kuiwasilisha taarifa ya
tathmini kwenye Bodi ya Zabuni ya TANESCO tarehe 28 Machi, 2006.
2.3 Vigezo vya Tathmini (Preliminary Evaluation)
Mheshimiwa Spika, Kamati ya Tathmini ikitumia vigezo mahsusi
karibu ya 30 vya kupima uwezo wa mzabuni, ikathibitisha kuwa
hakuna mzabuni hata mmoja kati ya wanane aliyetimiza au kukidhi
vigezo vya zabuni vilivyowekwa. Kutokana na hali ya kutisha ya
ukosefu wa umeme nchini, Kamati ya Tathmini ikalazimika kuondoa
zaidi ya nusu ya vigezo na kubakiza tisa tu ilivyoviona muhimu sana
kwa ngazi ile ya uchambuzi ili kumpata mshindi katika kundi
hilo la wazabuni wanane. Vigezo vilivyobakizwa ni:
(i) Muda wa kuleta mtambo na kuanza kazi,
(ii) Dhamana ya zabuni (Tender Security),
(iii) Uwepo wa mtambo tayari kuletwa Tanzania,
(iv) Uzoefu wa mzabuni kutekeleza miradi/ kuendesha mitambo ya
aina hiyo,
(v) Uzoefu na sifa za kitaaluma/ kiufundi za mzabuni,
(vi) Viambatisho vya idhini ya kisheria kuweza kufanya maamuzi ya
mwisho (Power of Attorney),
(vii) Uwepo wa maelezo ya lazima ya kiufundi,
(viii) Ujazaji fomu ya zabuni kikamilifu, na
(ix) Mchanganuo wa bei/ gharama ya umeme.
Mheshimiwa Spika, wazabuni wote wanane wakafanyiwa tathmini ya pili kwa kuzingatia vigezo hivyo tisa tu. Hata hivyo matokeo yakawa yale yale. Wazabuni wote wanane wakashindwa kukidhi vigezo hivyo vichache.
Mheshimiwa Spika, nyaraka tulizozipata kutoka TANESCO
zinaonyesha maeneo mbalimbali ya udhaifu miongoni mwa wazabuni
hao kama ifuatavyo:-
i) M/ S Aggreko I nternational Projects Ltd ya Uarabuni ilikutwa na
maeneo 7 yenye mapungufu,
(ii) M/ S Renco SPA ya I talia maeneo 9,
(iii) M/ S APGUM Co. Ltd ya Ujerumani maeneo 12,
(iv) M/ S GAPCO(T) Ltd ya Tanzania maeneo 13,
(v) M/ S Globeleq Ltd ya Kanada maeneo 14,
(vi) M/ S Real Energy Projects ya Uingereza maeneo 15,
(vii) M/ S Quantus ya Ujerumani maeneo 16, na
(viii) M/ S Richmond Development Company LLC ya Marekani ilikutwa
na maeneo 17 yenye mapungufu.
Mheshimiwa Spika, Kamati ya Tathmini haikuona busara kutangaza
kuwa imeshindikana kabisa kumpata mshindi. Hivyo, ikapunguza
vigezo zaidi na kubakiza vitano tu kama ifuatavyo:
(i) muda ambao mtambo utaanza kazi,
(ii) uwepo wa mtambo tayari kuletwa Tanzania,
(iii) uzoefu wa mzabuni kutekeleza miradi/ kuendesha mitambo ya
aina hiyo,
(iv) uzoefu na sifa za kitaaluma/ kiufundi za mzabuni, na
(v) uwepo wa maelezo ya lazima ya kiufundi.
Katika hatua hii wazabuni wanne (4) wakashindwa kukidhi vigezo
vichache vilivyobakizwa, hivyo kushindwa kufuzu kuingia hatua ya pili
ya kufanyiwa tathmini ya kina (detailed evaluation). Wazabuni
wengine wanne wakaonekana kuwa na afadhali kidogo na
kuruhusiwa kuingia hatua ya pili ya kufanyiwa tathmini ya kina. Nao
ni:
(i) M/ S Real Energy Projects ya Uingereza,
(ii) M/ S Renco SPA ya I talia,
(iii) M/ S GAPCO(T) Ltd ya Tanzania, na
(iv) M/ S Richmond Development Company LLC ya Marekani.
Mheshimiwa Spika, tathmini ya kina ya wazabuni hao wanne
walioonekana afadhali kidogo, ilionyesha kuwa Richmond
Development Company LLC ya Marekani bado ilikuwa na mapungufu
mengi yaani 13 kupita wazabuni wengine watatu. M/ s Renco SPA ya
I talia ilifuatia kwa kuwa na mapungufu 10; M/ s GAPCO (T) Ltd ya
Tanzania mapungufu 9 na M/ s Real Energy Project ya Uingereza
mapungufu 8. Kamati ya Tathmini iliwasilisha matokeo ya tathmini
kwa Bodi ya Zabuni ya TANESCO ikielezea kwamba hakuna mzabuni hata mmoja aliyetimiza masharti, hivyo wote walikosa sifa za kupata zabuni. Hivyo Kamati ikashauri zabuni itangazwe upya.
Mheshimiwa Spika, Bodi ya Zabuni ya TANESCO baada ya kuridhia mapendekezo hayo, iliyawasilisha kwenye Bodi ya Wakurugenzi wa TANESCO tarehe 30 Machi 2006. Bodi ya Wakurugenzi ya TANESCO ilipitia tathmini nzima na kuamua kwa kauli moja kuishauri Serikali kurejea kwenye ushauri wa PPRA wa kutumia njia ya international shopping ili kupata quotations moja kwa moja kutoka kwa
watengenezaji wa mitambo ya kuzalishia umeme kwa gesi.
Kesho yake, yaani tarehe 1 Aprili 2006 Waziri wa Nishati na Madini,
wakati huo Mhe. Dk. I brahim Msabaha, (Mb.) akionesha dhahiri
kutotaka njia ya international shopping kutumika, akawaita wajumbe
wote wa Bodi ya Wakurugenzi ya TANESCO na kuwaagiza
wahakikishe kuwa Bodi ya Zabuni ya shirika inawaita tena wazabuni
wote waliojitokeza awali na makampuni mengine yoyote yenye
uwezo wa kuingiza nchini mitambo hiyo. Aidha, Mhe. Dk. I brahim
Msabaha, (Mb.) alisisitiza kwa barua kwamba:
“Mshindi wa tenda ya ununuzi wa mitambo mipya atajulikana baada
ya idhini ya Serikali kutolewa. Composition ya wajumbe wa TANESCO
Tender Board ibadilishwe na kuimarishwa kwa kuwa na wajumbe
wenye uwezo na ni pro-active”.
Mheshimiwa Spika, ni dhahiri kuwa agizo hili la Waziri lilikuwa batili
kwani Sheria ya Ununuzi wa Umma haimpi Waziri mamlaka ya
kuingilia uteuzi wa Wajumbe wa Bodi za Zabuni za mashirika yaliyo
chini ya Wizara yake. Agizo hilo la Waziri likafuatiwa na uamuzi wa
Waziri Mkuu wa kuliondoa suala hilo mikononi mwa TANESCO na
kulikabidhi kwa Kamati Maalum iliyokuwa inaundwa na Katibu Mkuu
(Hazina), Katibu Mkuu (Nishati) na Mwanasheria Mkuu wa Serikali.
Tarehe 13 Aprili 2006, Mkurugenzi Mwendeshaji wa TANESCO wakati huo, Bw. Adriaan Van De Merwe, akaiondoa TANESCO rasmi kutoka kwenye mchakato huo kwa kumtumia Katibu Mkuu wa Wizara ya
Nishati na Madini nyaraka zote kuhusu zabuni yenyewe na uchambuzi
wote uliofanywa na TANESCO.
2.4 Mchakato wa Zabuni Ndani ya Wizara
Mheshimiwa Spika, tarehe 20 Aprili 2006, Wizara ya Nishati na Madini
iliamua kuunda timu ya wataalamu ili ichague mzabuni mmoja kati ya
wanane walioshiriki kwenye zabuni na kufanya naye majadiliano ya
mkataba. Katika kutekeleza azma hiyo, Serikali ilikuwa tayari
imejiandaa na kamati zake zifuatazo: Kamati ya Makatibu Wakuu,
Kamati ya Watalaam na Kamati ya Serikali ya Majadiliano.
Kamati ya Makatibu Wakuu iliundwa katika kikao cha Baraza la
Mawaziri cha tarehe 10 Februari 2006, ikiwajumuisha Makatibu
Wakuu wa Wizara ya Nishati na Madini, Wizara ya Fedha na
Mwanasheria Mkuu wa Serikali. Kamati hii ilipewa jukumu la
kusimamia mchakato mzima wa zabuni. I li kuharakisha zoezi hilo,
Serikali iliunda Kamati ya Wataalam (Team of Experts) ili kuisaidia
kwa karibu Kamati ya Makatibu Wakuu.
Mheshimiwa Spika, Kamati Teule iligundua kuwa Kamati ya Wataalam ndiyo iliyokuwa inafanya maamuzi ya msingi katika mchakato huu na iliyokuwa na mawasiliano ya karibu na Katibu Mkuu wa Wizara ya
Nishati na Madini, kwani kufuatana na ushahidi wa Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha, Ndugu Gray Mgonja, Kamati ya Makatibu Wakuu ilikutana mara moja tu toka iundwe.
Kazi ya kwanza ya Kamati hiyo ya Wataalam ilikuwa ni kupitia upya
na kuichambua tathmini iliyofanywa na TANESCO. Kazi ya pili ya
Kamati hiyo ilikuwa ni kumpata mzabuni ambaye angeweza
kutekeleza mradi huo wa umeme wa dharura kwa haraka. Katika
kutekeleza majukumu yake, Kamati hiyo ikatupilia mbali vigezo vya
msingi vilivyotumika na Kamati ya Tathmini ya TANESCO na kuweka
vipya ambavyo, kwa maoni ya Kamati Teule, vilifanana na vigezo vya
mchezo wa zamani wa watoto wa sadakarawe: “mwenye kupata
apate, mwenye kukosa akose”.
Mheshimiwa Spika, vigezo hivyo vilikuwa:
(i) Uwepo wa mitambo yenyewe pamoja na mitambo ya akiba,
(ii) Uunganishwaji wake kwenye gridi ya Taifa,
(iii) Hali ya usalama wa mitambo yenyewe kwa kulinganisha na
usalama wa gridi ya Taifa,
(iv) Muda wa kuleta mitambo, na
(v) Bei ya umeme.
Mheshimiwa Spika, kwa maoni ya Kamati Teule vigezo hivyo vilikuwa
haviendani na uzito na utaalam wa kazi iliyokusudiwa. Pia vilikuwa
vinatoa mwanya bayana kwa wazabuni hata walio dhaifu
kupenyezwa.
Mheshimiwa Spika, Kamati ya Wataalamu ikawaalika wazabuni wote
8 kwa usaili wa kuwapima kufuatana na vigezo hivyo vipya. Mzabuni
mmoja kati ya wazabuni wanane, M/ S GAPCO (T) Ltd hakushiriki.
Baada ya usaili huo, Kamati hiyo ikapata wazabuni wanne ambao
walionesha kukidhi vigezo hivyo vipya. Wazabuni hao ni: Richmond
Development Company LLC, Renco SPA, Aggreko I nternational
Projects Ltd na APGUM Co. Ltd.
Aggreko I nternational Projects Ltd walidai kuwa na uwezo wa
kuzalisha umeme wa MW 40 kwa senti za Kimarekani 6.0/ kWh;
Renco SPA walidai kuwa na uwezo wa kuzalisha umeme wa MW 60
kwa senti 10.0/ kWh; Richmond Development Company LLC alidai
kuwa na uwezo wa kuzalisha umeme wa MW 100 kwa senti
4.99/ kWh; na APGUM Co. Ltd ilidai kuwa na uwezo kuzalisha umeme
wa MW 100 kwa senti za Kimarekani 5.4/ kWh.
Mheshimiwa Spika, kutokana na madai hayo ambayo hayakuwa na
uthibitisho, Kamati ya Wataalamu ikaipendekeza Richmond
Development Company LLC kuingia kwenye majadiliano ya mkataba
na Serikali. Katika kuhalalisha ushindi huo wa Richmond Development
Company LLC wajumbe wote wa Kamati hiyo ya wataalamu, Waziri
wa Nishati na Madini aliyetangulia Mhe. Dk. I brahim Msabaha (Mb),
Waziri wa sasa wa Wizara hiyo, Mhe. Nazir Karamagi (Mb), Katibu
Mkuu wake, Ndugu Arthur Mwakapugi, Mwanasheria Mkuu wa
Serikali Mhe. Johnson Mwanyika, (Mb), Katibu Mkuu wa Wizara ya
Fedha, Ndugu Gray Mgonja na maafisa wote waandamizi wa Serikali
na TANESCO waliotoa ushahidi mbele ya Kamati Teule, walitoa kauli
zilizofanana mithili ya wimbo maarufu kuhusu sifa za Richmond
Development Company LLC zilizoifanya ishinde, kuwa:
(i) kwanza, bei yake ya umeme ilikuwa chini kupita makampuni
mengine;
(ii) pili, kampuni hiyo ilikuwa na ubia na kampuni kubwa na maarufu
duniani ya Pratt & Whitney ya Marekani inayotengeneza mitambo
mbalimbali ya umeme; na
(iii) tatu, iliwasilisha pendekezo lake kama mwendelezaji miradi.
Mheshimiwa Spika, pamoja na wimbo huo wa Richmond kunoga,
Kamati Teule ilishangazwa na udhaifu mkubwa wa hoja hizo uliokuwa
haulingani kabisa na ujuzi na uzoefu walionao watendaji wa
TANESCO na Serikali, hivyo kujenga hisia kuwa Richmond
Development Company LLC ilibebwa. Kwa mfano, hoja ya kwanza
inayohusu bei iliyopendekezwa na Richmond Development Company
LLC kuwa ilikuwa ndogo, haijitoshelezi. Je, Kamati hiyo ililinganisha
bei hiyo na kigezo kipi? Kwani katika kuangalia kumbukumbu za
mchakato wa majadiliano, Kamati hiyo haikuwa na kiwango chochote
cha makadirio ya bei ya umeme wa kukodi ambacho kingetumika
kama kigezo cha kupima unafuu huo kama ulikuwepo badala ya
kulinganisha na bei kubwa za makampuni ambayo yalikwisha
tubebesha mzigo mkubwa wa malipo hapo awali.
Aidha, Kamati Teule ilipata tetesi na baadaye ushahidi kuwa
Richmond Development Company LLC ilikuwa na wapambe ndani ya
Wizara ya Nishati na Madini na TANESCO waliokuwa wanaipa taarifa
(insider dealing). Mfano mdogo tu ni wa Ndugu Mohamed Saleh,
aliyekuwa Mkurugenzi wa Usambazaji wa TANESCO na rafiki wa
karibu wa wamiliki wa Richmond Development Company LLC.
Alishiriki kwenye Kamati ya Wataalam na Kamati ya Serikali ya
Majadiliano. Alipostaafu tu TANESCO, akawa mmoja wa wahandisi
waandamizi wa DOWANS HOLDI NGS S.A iliyochukua majukumu ya
Richmond Development Company LLC.
Pili, Mheshimiwa Spika, hoja ya kwamba kampuni hiyo ilikuwa na
ubia na kampuni kubwa ya Pratt & Whitney, haikuwa ya kweli. Katika
mchakato wote wa zabuni ndani ya TANESCO, moja ya masuala
kadhaa yaliyoifanya Richmond Development Company LLC isitiwe
maanani, ni ukosefu wa ushahidi wa kisheria wa ubia (consortium
agreement) kati yake na Pratt & Whitney. Baada ya kubanwa na
Kamati Teule kuhusu ushahidi wa mahusiano wa kampuni hizo mbili,
Wajumbe wa Kamati ya Wataalamu waliwasilisha mbele ya Kamati
Teule ushahidi wa aina mbili: kwanza business card ya mzungu
mmoja aliyejulikana kwa jina la John Perun aliyejiita mwakilishi wa Pratt & Whitney, na pili, kivuli cha mkataba wa kurasa nne kati ya Richmond Development Company LLC na Pratt & Whitney wa
kubadilishana taarifa na siyo kuzalisha umeme. Aidha mkataba huo ulikuwa haujathibitishwa na wakili au shahidi yeyote wa kuaminika kuwa mkataba halali. Kamati Teule imesikitishwa na kushangazwa kwa kiwango cha chini cha umakini kilichoonyeshwa na wataalam wetu hususan kutoka Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali katika kushughulikia suala hili.
Mheshimiwa Spika, viongozi wote wa Serikali waliohojiwa na Kamati
Teule walisisitiza kuwa uamuzi wa kuipa Richmond Development
Company LLC kazi hiyo ya kuzalisha umeme wa dharura, ulichangiwa
kwa kiasi kikubwa na madai ya kampuni hiyo kuwa na ubia na
kampuni maarufu ya Pratt & Whitney. Hivyo basi, ushahidi wa
uhusiano wa kisheria wa Kampuni hizo mbili, ulikuwa suala la msingi
ambalo wataalamu wetu waliwajibika kulipa uzito ili kulinda maslahi
ya nchi.
Katika tovuti yake (www.rdevco.com) Richmond Development
Company LLC ilikuwa inajitangaza kimataifa kuwa kampuni yenye
miradi mikubwa Tanzania ya ujenzi wa kiwanja cha kisasa cha
michezo, ujenzi wa bomba la mafuta la kilometa 1,150 na ukarabati
wa viwanja kadhaa vya ndege. Kamati Teule ilishindwa kuelewa kwa
nini Kamati ya Wataalam haikuihoji Richmond Development Company
LLC kuhusu uongo huo bayana ambao ulikuwa ushahidi wa kutosha
kuipotezea sifa za kuwa mzabuni.
Hoja ya tatu, Mheshimiwa Spika, ya kwamba Richmond Development
Company LLC ni mwendelezaji miradi, ilitakiwa vile vile ifanyiwe kazi
badala ya kuiamini tu. Wizara ya Nishati na Madini haiwezi kukwepa
lawama kwa kufumbia macho ukweli kuwa Richmond Development
Company LLC ilishakuwa na Mkataba na Wizara hiyo uliosainiwa
tarehe 30 Juni 2004, Mkataba uliovunjika mwezi Januari 2006 kwa
kampuni hiyo ya Kimarekani iliyojitambulisha kama mwendelezaji
miradi kushindwa kutekeleza sehemu yake ya mkataba. Wizara
inaelewa fika kuwa kampuni hiyo ilishindwa utekelezaji kutokana na
kuyumba kifedha. Mwendelezaji miradi gani ambaye anashindwa
kumudu hata fedha ya kununulia maafisa wake tiketi ya ndege
kutoka Dar-es-Salaam hadi Afrika Kusini na kurejea, kama
ilivyoelezwa na Mkurugenzi wa Tanzania Green Company Ltd?
Mheshimiwa Spika kama tulivyodokeza hapo awali, baada ya Kamati
ya Wataalam kumaliza kazi yake na kuwasilisha taarifa Serikalini, Kamati ya Serikali ya Majadiliano (Government Negotiation Team) ikiwa na wajumbe kutoka TANESCO, Wizara ya Nishati na Madini, Wizara ya Fedha, Benki Kuu na Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa
Serikali, ikaanza mchakato wa majadiliano ya mkataba na Richmond
Development Company LLC.
Mheshimiwa Spika, kama ilivyotokea kwa Kamati ya Wataalam,
Government Negotiation Team vile vile haikufanya kazi ya kuridhisha
japokuwa ilikuwa na uwakilishi mpana. Kwa mfano, suala la
kukosekana kwa consortium agreement kati ya Richmond
Development Company LLC na Pratt & Whitney halikuwasumbua
kabisa wajumbe wa Kamati ya Serikali ya Majadiliano. Wajumbe hao, akiwemo mwakilishi wa Mwanasheria Mkuu wa Serikali, waliichukulia business card ya Bwana John Perun na mkataba wa kubadilishana taarifa kati ya kampuni hizo mbili kuwa ushahidi wa kutosha wa ubia au ushirikiano. GNT ilishindwa hata kusisitiza kuwa ubia wa kampuni hizo uwekwe wazi katika mkataba kati ya TANESCO na Richmond
Development Cpompant LLC.
Aidha, kwa kuelewa kuwa Richmond Development Company LLC
haikufanyiwa uchunguzi wa awali (due diligence) GNT ilishindwa
kupendekeza kwa Serikali umuhimu wa kuifanyia Kampuni hiyo
uchunguzi baada ya kuiteua (post-qualification) kujua uwezo wake
kifedha, kiutendaji, kiutalaam na kiuzoefu. Katika mahojiano na
Wajumbe wa GNT, Kamati Teule iligundua kuwa masuala mengi
waliyapitisha kwa mazoea tu, baadhi ya wajumbe wake wakiamini
kuwa mikataba ya aina hiyo inatoka Benki ya Dunia na vipengele
vyake havibadiliki. GNT ilifika mahali ikakubali bila vigezo vya
kueleweka kwamba Richmond Development Company LLC
ikichelewesha utekelezaji wa mradi itailipa TANESCO faini ya Dola za
Kimarekani 10,000 au sh. milioni 12.5 tu kwa siku, lakini Richmond itaidai TANESCO ilipe Dola za Kimarekani 121,811 au sh. milioni 152 kila siku hadi mwisho wa mkataba kama gharama za kudumu za
uwezo wa mitambo yao (capacity charges), wazalishe umeme,
wasizalishe! Haiingii akilini!
Mheshimiwa Spika, tarehe 19 Juni, 2006, Bodi ya Zabuni ya
TANESCO ilikutana na kupitisha uamuzi rasmi wa kufuta zabuni
waliyokuwa wanashughulikia awali na kutangaza kuwa “TANESCO
isihusishwe na mkataba wowote utakaotokana na nyaraka za zabuni
waliyoifuta”.
Lakini siku hiyo hiyo ya tarehe 19 Juni 2006, Waziri wa Nishati na
Madini alimwandikia Waziri Mkuu dokezo kuwa majadiliano ya awali
na Richmond Development Company LLC yamekamilika hivyo Serikali
iiteue kampuni hiyo kwa lengo la kuingia mkataba na TANESCO wa
kuzalisha umeme wa dharura kwa miaka miwili. Sehemu ya barua
hiyo inasomeka:
“Kamati ya Serikali ya Majadiliano (GNT) inayojumuisha wataalam
kutoka Wizara Fedha, Wizara ya Nishati na Madini, Ofisi ya
Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Benki Kuu na TANESCO ilifanya
majadiliano na Richmond Development Company LLC ya Houston,
Marekani kutoka tarehe 8 hadi 16 Juni 2006, kwa kuzingatia
maelekezo yako.”
Mheshimiwa Spika, tarehe 21 Juni 2006, Katibu wa Waziri Mkuu
Ndugu B. Olekuyan aliiandikia Wizara ya Nishati na Madini kuitaarifu
kuwa Mhe. Waziri Mkuu amekubali mapendekezo na ushauri wa
Waziri wa Nishati na Madini kama ulivyokuwa umeletwa.
Siku hiyo hiyo tarehe 21 Juni 2006, Waziri wa Nishati na Madini
akamwandikia dokezo Katibu Mkuu wake aiagize TANESCO iingie
mkataba mara moja na Richmond Development Company LLC baada
ya Waziri Mkuu kuidhinisha mapendekezo ya Wizara. Muda mfupi
baadaye, kwa kutekeleza agizo la Waziri, Katibu Mkuu wa Wizara ya
Nishati na Madini akamwandikia barua Mwenyekiti wa Bodi ya
Wakurugenzi ya TANESCO Balozi Fulgence Kazaura kumwagiza
ahakikishe kuwa TANESCO inasaini mkataba na Richmond
Development Company LLC.
Mheshimiwa Spika, I jumaa ya tarehe 23 Juni 2006, Kaimu
Mkurugenzi Mwendeshaji wa TANESCO, Bwana Johannes .G.
Lottering, aliitwa Wizara ya Nishati na Madini na kuagizwa kusaini
Mkataba huo kati ya TANESCO na Richmond Development Company
LLC. Pamoja na kusita kwake, hatimaye alisaini mkataba huo.
Kamati Teule inaelewa hisia walizokuwa nazo viongozi wa ngazi
mbalimbali wa TANESCO kutokana na uongozi wa kiimla wa Wizara
ukipata nguvu kutoka Ofisi ya Waziri Mkuu. Tulichokiona awali kwa
maana ya mchakato wa Zabuni kuchukuliwa na Wizara, ulikuwa
ukiukwaji wa sheria na utaratibu mzima wa uwajibikaji. Pamoja na dharura iliyokuwa inaikabili Taifa, Serikali haiwezi kuwa kinara wa kuvunja sheria za nchi. Ni maoni ya Kamati Teule kuwa Wizara
ilikiuka siyo tu masharti ya sheria na kanuni za ununuzi wa umma,
bali vilevile maagizo mbalimbali ya Baraza la Mawaziri.
Mheshimiwa Spika, Kamati Teule isingelikerwa sana na matukio haya
kama Wizara ambayo ni taasisi ya ununuzi (procurement entity)
kama ilivyo TANESCO, ingemalizia mchakato wake kwa kusaini
mkataba huo yenyewe. Kuishinikiza TANESCO kusaini mkataba
ambao vyombo vyake halali vilikuwa havijaupitia, ni udanganyifu,
upotoshaji wa hali ya juu wa taratibu za kazi na sheria na udhalilishaji
wa vyombo vya maamuzi ndani ya TANESCO. I nashangaza kuwa
baada ya kudhalishwa na Wizara kwa kiwango hicho, chombo kikuu
cha maamuzi cha TANESCO, yaani Bodi ya Wakurugenzi,
hakikuchukua hatua ya heshima ya kujiuzulu.
Mheshimiwa Spika, kama nilivyodokeza awali, Kamati Teule ilishindwa
kubaini moja kwa moja chanzo cha ujasiri wa kiburi ndani ya Wizara
ya Nishati na Madini kiasi cha kupindisha maamuzi ya Baraza la
Mawaziri bila wasiwasi wowote, kukaidi ushauri wa kitaalamu wa
Mamlaka ya Udhibiti wa Ununuzi wa Umma mara tatu mfululizo na
kinyume na maagizo ya Baraza la Mawaziri yaliyotaka Sheria ya
Ununuzi wa Umma izingatiwe, kukiuka sheria kwa makusudi kwa
kuingilia mchakato wa zabuni wa taasisi nyingine ya ununuzi,
kuvipuuza vyombo vya ndani vya maamuzi vya TANESCO (Bodi ya
Wakurugenzi, Bodi ya Zabuni n.k), kuilazimisha Bodi ya Menejimenti
ya TANESCO kuridhia maamuzi yaliyofanywa na Wizara ya kuibeba
Richmond Development Company LLC kinyume cha sheria na
taratibu, n.k. Aidha Kamati Teule ilishangazwa na Ofisi ya Waziri
Mkuu iliyokuwa ikifuatilia kwa karibu mchakato huo, kushindwa
kukemea ukaidi huo wa Wizara ya Nishati na Madini.
Baadhi ya mashahidi, wakiwemo waandishi wa habari mashuhuri
nchini, waliinyooshea kidole Ofisi ya Waziri Mkuu kuwa msingi wa
ubabe uliokithiri wa Wizara ya Nishati na Madini katika kuibeba
Richmond. Aidha baadhi ya nyaraka ambazo Kamati Teule ilipata
katika uchunguzi wake zilionesha kuwa maelekezo na maamuzi
mengi ya msingi yalikuwa yanafanywa na Waziri Mkuu badala ya
Wizara. Mfano ni barua kutoka Wizara ya Nishati na Madini kwenda
kwa Waziri Mkuu tuliyoinukuu ukurasa wa 31 wa taarifa hii, ikitamka
wazi kuwa GNT ilifanya majadiliano na Richmond Development
Company LLC tarehe 8 hadi 16 Juni 2006 “kwa kuzingatia maelekezo”
ya Waziri Mkuu.
Vilevile, Mheshimiwa Spika, tarehe 13 Julai 2006 Waziri wa Nishati na Madini akamwandikia Katibu Mkuu wake kuwa, “Nimezungumza tena na Mheshimiwa Waziri Mkuu leo juu ya bei ya mitambo ya Aggreko. Msimamo ni ule ule niliokueleza awali na ameagiza tuulizie Richmond kama anaweza kutoa 40 MW kwa bei isiyozidi ile ile ya 4.99 cents per kWh na kama tunaweza kuipata basi achukuliwe Richmond”.
Mheshimiwa Spika, ushiriki huu wa karibu wa Waziri Mkuu katika kila
hatua ya zabuni ya umeme wa dharura, si lazima uwe ushahidi wa
kwamba kiongozi huyo wa kitaifa alihusika katika kuibeba Richmond.
Unaweza pia ukawa ushahidi wa staili yake ya kawaida kabisa ya
uongozi katika kufuatilia masuala yote ya kitaifa kwa karibu sana
tukizingatia kwamba nchi wakati huo ilikuwa katika kipindi kigumu
sana cha ukosefu wa umeme. Watu pekee waliokuwa wanaujua
ukweli wenyewe, ukweli ambao ungeipa Kamati Teule msingi wa
kumhoji Waziri Mkuu kwa kiapo, walikuwa watatu: Waziri Dk.
Msabaha (Mb), Katibu Mkuu Mwakapugi na Mwenyekiti wa Bodi
Balozi Kazaura.
Mheshimiwa Spika, Kamati Teule ikawaita kwa mara ya pili Dk.
Msabaha (Mb) na Ndugu Mwakapugi kwa mahojiano zaidi. Wote
wawili, wakiwa ndani ya kiapo, walikataa katakata kupokea maagizo
kutoka kwa Waziri Mkuu ya kuipa Richmond upendeleo. Lakini Mhe.
Dk. Msabaha (Mb), baada ya mahojiano chini ya kiapo, akaiuma sikio
Kamati Teule kuwa katika suala hilo yeye atakuwa kondoo wa kafara
tu au, kwa maneno yake mwenyewe, “Bangusilo” kwa lugha ya
Kizaramo. Maelezo hayo ya ziada nje ya kiapo ya Mheshimiwa Waziri yaliyotoa ujumbe kuwa “si yeye ila mkuu wake wa kazi”, yalioana na maelezo aliyoyatoa Balozi Kazaura nje ya kiapo tarehe 30 Novemba, 2007. Mara baada ya kumaliza mahojiano kwa kiapo na Kamati
Teule, Balozi akatoa maelezo ya ziada kuwa Richmond ilikuwa mradi
wa “Bwana Mkubwa” na “mshiriki wake mkubwa kibiashara”,
akimaanisha Mhe. Waziri Mkuu na Mhe. Rostam Aziz (Mb).
Mheshimiwa Spika, tumelazimika kueleza hata mambo tuliyoelezwa
kwa siri kiungwana (in confidence) kutokana na uzito wa suala
lenyewe na dhamana kubwa tuliyopewa na Bunge ya kuelezea
kilichotokea kwa uwazi na ukweli. Lakini ushahidi huu wa ziada na
nje ya kiapo wa viongozi hawa wawili, haukutoa msaada stahili kwa
Kamati Teule kwa kuwa msingi wa maamuzi yote ya Bunge si
minong’ono au tetesi, bali taarifa zenye uthibitisho halisi. Ni dhahiri
kuwa, kwa watumishi hao “waaminifu” wa Serikali, isingelikuwa rahisi
kumtaja Waziri Mkuu chini ya kiapo. Hatua hiyo inahitaji ujasiri
mkubwa na uzalendo wa hali ya juu.
Pamoja na woga uliokuwa dhahiri wa watumishi hao, ushahidi wa
maandishi, wa mdomo na kimazingira ambao Kamati Teule iliupata
kutoka kwa mashahidi mbalimbali, unamhusisha Waziri Mkuu na
mchakato wa maamuzi katika suala hili la Richmond.
Mheshimiwa Spika, uvumi wa kuhusika kwa Waziri Mkuu na baadhi
ya washiriki wake wa karibu katika suala hili la Richmond umeenea
sehemu nyingi nchini kwa kiwango cha kushangaza. Kamati Teule
inaelewa kuwa uvumi huo unaweza kuwa umechangiwa na
mahasimu wake kisiasa, lakini uharaka, urahisi na wepesi wa
wananchi kuziamini tetesi hizo, unazua maswali mengi kuhusu imani,
taswira, na heshima aliyojijengea yeye mwenyewe katika jamii.
3.0 MKATABA KATI YA TANESCO NA RI CHMOND DEVELOPMENT
COMPANY LLC
3.1 Maudhui na Utekelezaji wa Mkataba
Mheshimiwa Spika, kama tulivyoona awali, Mkataba kati ya TANESCO
na Richmond Development Company LLC hatimaye ulisainiwa na
pande zinazohusika Jijini Dar-es-Salaam tarehe 23 Juni 2006.
Madhumuni ya Mkataba yameainishwa wazi katika Utangulizi wa
Mkataba kuwa ni kusambaza umeme wa dharura kwa kutumia
mitambo ya kukodi ya kuzalisha umeme wa MW 105.6 kutokana na
gesi.
Madhumuni ya msingi ya Mkataba huu yalikuwa kuzalisha na
kusambaza umeme wa dharura (emergency power supply) katika
kipindi cha ukame kilicholikumba Taifa. Ndiyo maana tangazo la awal
la zabuni la TANESCO liliweka kipindi kifupi cha miezi 12 tu cha
kutumia umeme huo wa dharura na muda huo ungeweza kuongezwa
kutegemea hali ya uzalishaji umeme nchini. Lakini Mkataba huo umeongeza muda kutoka miezi 12 hadi 24 na kuifanya dhana ya “umeme wa dharura” ipotee kabisa katika mradi huo.
Mheshimiwa Spika, Kamati Teule haikuona mantiki ya kuongeza
muda mapema hadi miaka miwili wakati fursa ya kuongeza muda
baada ya mwaka mmoja ilikuwepo kutegemeana na hali ya mvua
nchini. Uamuzi wa kuongeza muda kabla ya kutathmini hali ya mvua
na upatikanaji maji kwenye mabwawa yetu ya kuzalishia umeme,
ulikosa uzalendo na hauwezi kukwepa tuhuma ya ufisadi. Uamuzi huo
umeibebesha nchi gharama kubwa zisizo za lazima kwani miezi sita tu baada ya kusaini Mkataba huo, mabwawa ya kuzalishia umeme nchini yalikuwa yameshajaa.
Hivyo, Mheshimiwa Spika, tunalazimika chini ya Mkataba huo kulipia,
mbali na gharama ya umeme wenyewe, uwepo wa mitambo hiyo
nchini (capacity charges) kwa gharama ya sh. milioni 152 kila siku
kwa miaka miwili mfululizo badala ya mwaka mmoja. Aidha kutokana
na mabwawa yetu kuzalisha umeme usio na gharama kubwa,
mitambo hiyo ya kukodisha ambayo umeme wake ni aghali hutumika
chini kabisa ya kiwango kilichokusudiwa (underutilisation).
Mheshimiwa Spika, Kamati Teule inasisitiza kuwa udharura wa mradi
huu ulimalizika pale mabwawa yetu yalipoanza kujaa maji polepole
kutokana na mvua kubwa zilizokuwa zinanyesha nchini mwishoni
mwa Disemba, 2006 na kufikia kilele stahili mapema mwezi Februari
2007. Hivyo kitendo cha Wizara kuikubalia kampuni iliyoshindwa
kutekeleza sehemu yake ya Mkataba kwa wakati muafaka, Richmond
Development Company LLC, kuyahamishia majukumu yake kwa
kampuni nyingine ya Dowans Holdings S.A. bila kuufanyia Mkataba
huo marekebisho stahili ya kuipunguzia nchi mzigo wa malipo,
hakikuwa cha kizalendo bali cha kukidhi maslahi binafsi ya kibiashara.
Mheshimiwa Spika, mbali na hoja hiyo, tulikuwa na fursa ya wazi ya
kuuvunja mkataba huo bila madhara yoyote ya kisheria chini ya
kifungu cha 12.3 cha Mkataba. Tarehe 27 Oktoba, 2006 TANESCO
ilichukua hatua ya kwanza kuelekea huko kwa kuitumia Richmond
Development Company LLC taarifa ya tahadhari (Default Notice)
iliyoelezea mapungufu ya Richmond yalitohitaji majibu ya uhakika:
kushindwa kwa kampuni hiyo kusafirisha angalau mtambo wa
kwanza wa wastani wa unit 22 kW kuja Tanzania; kushindwa kwa
kampuni hiyo kutoa taarifa za mara kwa mara za maendeleo ya
utekelezaji wa mradi; uwepo wa kampuni hiyo Marekani kihalali;
uwezo wa kampuni hiyo kitaalamu na kifedha kuweza kutekeleza
Mkataba huo wa umeme wa dharura katika muda muafaka.
Mheshimiwa Spika, kimya cha Richmond kikailazimu TANESCO
kuiandikia tena kampuni hiyo tarehe 17 na 23 Novemba 2006
kuikumbusha kuhusu hoja zake za awali ambazo hazikujibiwa na
kudai maelezo kuhusu taarifa za kwamba kampuni hiyo haikuwa na
mahusiano na Pratt & Whitney iliyotegemewa sana kubeba sehemu
kubwa ya majukumu ya mradi.
Mheshimiwa Spika, Wizara ya Nishati na Madini haikufurahishwa na
mwelekeo huo wa TANESCO wa kuvunja Mkataba huo licha ya
kwamba hali ya maji nchini ilizidi kuwa nzuri na kampuni hiyo ya
Marekani ilikuwa haionyeshi dalili ya kuweza kutekeleza mradi huo
kinyume na makubaliano. Aidha, TANESCO ilikuwa imepata
uthibitisho usio na shaka kutoka kampuni mashuhuri ya mawakili ya
Virginia, Marekani iitwayo Hunton & Williams LLP kwamba Richmond
Development Company LLC ilikuwa kampuni ya mkobani (brief-case
company).
Waziri wa Nishati na Madini, Mhe. Nazir Karamagi (Mb), kupitia kwa Kamishna wa Nishati, Ndugu Bashir Mrindoko, akamtaka Mkurugenzi Mkuu wa TANESCO ajieleze kulikoni anaitumia Richmond taarifa za tahadhari zenye mwelekeo wa kuvunja mkataba. Mkurugenzi Mkuu wa TANESCO akajieleza kwa barua aliyomwandikia Waziri moja kwa moja yenye Kumb. Na. MD/ 003 ya tarehe 23 Novemba, 2006.
Mheshimiwa Spika, siku tano tu baada ya Mkurugenzi Mkuu wa
TANESCO kujieleza, yaani tarehe 28 Novemba 2006, Mwenyekiti wa Bodi ya TANESCO, Balozi Kazaura, alimtaarifu Mkurugenzi Mkuu wa TANESCO kwa barua kwamba asubuhi ya siku hiyo alikuwa kapigiwa
simu na Waziri Karamagi akiwa Jijini Calgary, Canada akimuarifu
kwamba Richmond Development Company LLC walikuwa wanataka
kuhamisha majukumu yao yaliyobaki katika Mkataba wa uletaji
mitambo na uzalishaji umeme wa dharura kwa kampuni nyingine.
Kufuatana na barua ya Balozi Kazaura yenye Kumb. Na.
SEC.216/ C/ RDC ya tarehe 28 Novemba, 2006, Mheshimiwa Waziri
aliagiza, pamoja na mambo mengine, kuwa TANESCO iangalie kama
Mkataba kati ya TANESCO na Richmond Development Company LLC
unaruhusu kukabidhi majukumu kwa kampuni nyingine.
Mheshimiwa Spika, siku hiyo hiyo ya tarehe 28 Novemba 2006,
uongozi wa TANESCO ulimshauri Mwenyekiti wa Bodi amtaarifu Mhe.
Waziri kwamba Kifungu cha 15.12 cha Mkataba huo hakiruhusu
kukabidhi majukumu ya Mkataba kwa Kampuni nyingine isipokuwa
kwa maafikiano ya pande mbili za Mkataba. Hatimaye, siku sita
baadaye, yaani tarehe 4 Disemba 2006, TANESCO ikapokea barua
kutoka kwa Richmond Development Company LLC ikielezea
makusudio ya Richmond kuhamisha majukumu yake yote ndani ya
Mkataba huo kwenda kwa Dowans Holdings, S.A.
Siku hiyo hiyo TANESCO ikaijibu Richmond kwamba haikuwa tayari
kuridhia pendekezo hilo kwa sababu kuu tatu:
(i) Kifungu 15.12 cha Mkataba kinataka kuwepo kwa makubaliano ya
pamoja ya kimaandishi (written mutual agreement) kutoka kwa
wahusika wote wa Mkataba (Parties) kabla ya kufikiwa uamuzi wa
kuhamisha Mkataba.
(ii) Richmond Development Company LLC haijatoa sababu zozote za
msingi kwa pendekezo hilo la kuhamisha Mkataba.
(iii) TANESCO haifahamu historia, uzoefu wala uwezo wa kifedha wa
hao wanaopendekezwa kuhamishiwa Mkataba.
Aidha, TANESCO ilikumbushia barua zake za awali ilizoiandikia
Richmond Development Company LLC kuhusu ukiukwaji wa masharti
ya Mkataba, lakini Richmond haikuzijibu. Hivyo, TANESCO ikataka
ipate kwanza majibu ya masuala yote iliyoyaainisha kabla ya kufikiria
kuridhia pendekezo la kuhamisha Mkataba huo.
Mheshimiwa Spika, kama kawaida ya Wizara ya Nishati na Madini,
TANESCO ikashinikizwa kukubaliana na ombi la Richmond hata kabla
kampuni hiyo ya Kimarekani haijajibu hoja za msingi za TANESCO.
Tarehe 21 Disemba 2006 TANESCO ikaiandikia barua Richmond
Development Company LLC kukubali pendekezo la kuhamisha
majukumu yake kwa Dowans Holdings, S.A.
Uamuzi huo wa kuruhusu uhaulishwaji wa Mkataba kipindi ambacho
nchi ilikuwa imeondokana na hali ya dharura, tena kwa masharti
yaleyale ya kulaliwa yanayoweza kukubalika pale tu ambapo nchi
imebanwa kweli kweli na tatizo, ulimfedhehesha hata Mkurugenzi
Mwendeshaji wa Dowans Holdings S.A., Bw. Guy Piccard, raia wa
Kanada, alipohojiwa na Kamati Teule tarehe 27 Disemba, 2007. Bw.
Piccard haoni kwa nini mkataba huo usiangaliwe upya kutokana na
mazingira ya udharura kutokuwepo.
3.2 Mzigo wa Malipo wa TANESCO
Mheshimiwa Spika, nimeeleza awali kuwa mbali na kulipia gharama
ya umeme wenyewe, TANESCO inawajibika chini ya Mkataba huo
kulipa gharama za uwezo wa mitambo (capacity charges) ambazo ni
sh. milioni 152 kila siku hadi mwisho wa Mkataba. Aidha, chini ya
Mkataba huo, TANESCO inabebeshwa mzingo wote wa kodi, malipo
na gharama mbalimbali zinazoweza kumkabili mwekezaji! Kifungu
cha 3.4 cha Mkataba wa TANESCO na Richmond kinasema:
“All taxes and charges arising in relation to the importation and
exportation of the plant, equipment, tools, spare parts, consumables, testing and monitoring equipment or in connection with the supplier’s performance of its obligations under this Agreement generally that
become due in accordance with the laws of Tanzania shall be paid for
by TANESCO at its sole cost and expense” .
Mheshimiwa Spika, Tafsiri ya jumla ya kifungu hiki cha Mkataba ni kwamba: kodi na ada zote zinazohusiana na uingizaji ndani ya nchi na usafirishaji nje ya nchi wa mitambo yote, vifaa, vipuli n.k. na
gharama zote zinazohusiana na utekelezaji wa wajibu wa Richmond
(sasa Dowans) chini ya Mkataba, yaani gharama za uendeshaji
(operations), za matengenezo (maintenance) ya mitambo na gharama ya gesi inayotumika kuzalishia umeme, ni wajibu wa TANESCO kuzibeba!

Mheshimiwa Spika, mzigo mkubwa ambao TANESCO inabeba chini ya
mkataba na Richmond (sasa Dowans) unajirudia katika mikataba
mingine kati ya TANESCO na makampuni mengine ya umeme kama
vile I PTL, AGGREKO, ALSTOM na SONGAS ambayo kwa ujumla
yanachukua sehemu kubwa ya mapato ya shirika hilo, hivyo
kuvuruga kabisa mizania yake. Kwa wigo wa tafsiri wa mikataba hii
inayotuumiza kwa kujitakia, TANESCO inawajibika kuwalipia hawa
wanaojiita wawekezaji hata gharama za bima na ada za mawakili
wao!
Mheshimiwa Spika, tumefikishwa hapa tulipofika na mikataba
mibovu, maamuzi ya kiimla na papara ya baadhi ya watendaji
waandamizi wa Serikali wasiozingatia maslahi ya muda mrefu ya
Taifa. Net Group Solution (PTY) ambayo kwa kiwango kikubwa
imechangia sana katika kuidumaza TANESCO kiutaalamu na kifedha,
iliingizwa TANESCO kwa ubabe bila kujali hoja za msingi za
wataalamu na wafanyakazi wa TANESCO. Matokeo yake wote
tunayaelewa. Vivyo hivyo, Richmond Development Company LLC,
kampuni isiyo na rekodi yoyote ya kiufundi hata ya kuchomeka “bulb”
kwenye kishikio chake, ikapewa mradi mkubwa na Serikali wa
kuzalisha umeme wa dharura bila kujali kuhusu ufanisi wake tena
katika kipindi ambacho nchi ilikuwa gizani! Huu ni ujasiri wa kifisadi.
4.0 UTEKELEZAJI WA MRADI
4.1 Barua ya Dhamana ya Benki (Letter of Credit)
Mheshimiwa Spika, ili kufanikisha utekelezaji wa haraka wa mradi wa
umeme wa dharura, Mkataba kati ya TANESCO na Richmond
Development Company LLC, ulitoa fursa ya kufunguliwa kwa Barua ya Dhamana ya Benki (Letter of Credit), kwa kifupi nitaiita LC, kwa madhumuni ya kulipia gharama za maandalizi na za usafirishaji wa
mitambo ya uzalishaji wa umeme huo wa dharura. Mkataba ulitaka
TANESCO, Benki Kuu ya Tanzania, Wizara ya Fedha na Richmond
Development Company LLC waketi pamoja kukubaliana masharti ya
LC hiyo.
Mheshimiwa Spika, vyombo hivyo vya Serikali vilikaa tarehe 7 Julai,
2006 baada ya kupokea mapendekezo kutoka Richmond
Development Company LLC ya namna ambavyo ingetaka ilipwe.
Vyombo hivyo vya Serikali vikarekebisha kidogo madai ya Richmond
na kuamua kuwa kampuni hiyo ilipwe Dola za Kimarekani 30,000,000
(milioni thelathini), sawa na asilimia 30 ya thamani ya malipo ya
Mkataba kwa kipindi cha miaka miwili kwa masharti kwamba: asilimia
12 ya fedha hizo ilipwe kama malipo ya awali (Advance Payment)
baada ya kuwasilishwa hati ya madai (I nvoice), hati ya Uthibitisho wa
Udhamini wa Benki (Bank Guarantee) kwa TANESCO na uthibitisho
wa kusafirisha mitambo kuleta Tanzania; asilimia 10 ilipwe baada ya
kuwasilishwa hati za kusafirishia mitambo kwa mpangilio wa awamu;
asilimia 8 ilipwe mara baada ya uzinduzi wa mitambo.
Mheshimiwa Spika, siku tatu baadaye Richmond Development
Company LLC ikataka masharti hayo yarekebishwe ili kuipa kampuni
hiyo unafuu zaidi, wazo ambalo TANESCO ililikataa kwa kuhofia kuwa
kampuni hiyo ingeweza kupotea baada ya kupata malipo ya awali
yasiyo na masharti magumu. Tarehe 27 Julai, 2007 Wizara ya Nishati
na Madini ikaingilia kati mvutano huo na kuitisha kikao
kilichosimamiwa na Waziri Mhe. Dr. I brahim Msabaha, Mb kama
Mwenyekiti. Kikao hiki kilihusisha wajumbe kutoka Wizara ya Fedha,
TANESCO, Benki Kuu ya Tanzania, Mwakilishi kutoka CTI na
Richmond Development Company LLC. Kama ilivyokuwa kwa kikao
cha tarehe 7 Julai, 2006, Mwanasheria Mkuu wa Serikali wala
mwakilishi wake hakuhudhuria.
Mheshimiwa Spika, kikao hiki kikaamua kurekebishwa kwa masharti ya LC kama ilivyopendekezwa na Richmond Development Company LLC. Baadhi ya marekebisho yalikuwa:
(i) Kampuni hiyo ilipwe asilimia 17.5 ya jumla ya thamani ya Mkataba
baada ya Benki ya kampuni hiyo kupokea hati za usafirishaji wa
mitambo (shipping documents), hati ya bima, orodha ya vifungashio
(packing list), hati za uasili wa bidhaa (Certificate of origin), hati za
upangaji wa mizigo (packing lists), pamoja na hati ya madai (I nvoice)
kwa mtambo wa MW 22.
(ii) Kampuni hiyo ilipwe vilevile asilimia 17.5 ya jumla ya thamani ya
Mkataba baada ya TANESCO kutoa hati ya uthibitisho ya mitambo
kuwasili eneo la kazi (Ubungo, Dar-es-Salaam).
4.2 Mchakato wa Kufungua Barua ya Dhamana ya Benki
Mheshimiwa Spika, baada ya makubaliano hayo, tarehe 23 Agosti,
2006 TANESCO iliiomba Citibank (Tanzania) kufungua LC kwa ajili ya
Richmond Development Company LLC yenye thamani ya Dola za
Kimarekani 30,696,598.00. Siku hiyo hiyo ya terehe 23 Agosti 2006,
Citibank (Tanzania) iliwajulisha TANESCO kwamba isingeweza
kufungua LC kwa ajili ya Richmond Development Company LLC,
kutokana na kile walichoeleza kuwa ni kutopata muda wa kutosha
kuchunguza kwa kina uwezo wa mteja anayehusishwa na dhamana
ya malipo hayo (due diligence) kabla ya kuingia Mkataba huo.
Mheshimiwa Spika, baada ya kukataliwa na Citibank, TANESCO
waliiomba Benki ya CRDB kufungua Barua ya Dhamana ya Benki hiyo
kwa masharti sawa na yale yaliyopelekwa Citibank (Tanzania).
Tarehe 25 Agosti, 2006 CRDB ikafanya mawasiliano Citibank (New
York). Lakini tarehe 2 Septemba 2006, Citibank (New York)
ikaifahamisha CRDB kuwa wao pia wasingeweza kushiriki katika
kufungua LC kwa Richmond Development Company LLC kutokana na
mahitaji ya lazima ya kuzingatiwa chini ya Kifungu Namba 7 cha
Kanuni za UCP 500. Kifungu hicho ndicho kilichowafanya Citibank
(Tanzania) kukataa kufungua Barua kama hiyo.
Mheshimiwa Spika, kitendo cha benki hizo mbili za Kimarekani
kukataa kufungua LC kwa jili ya kampuni ya Kimarekani, kilitosha
kuzua wasiwasi wa msingi kuhusu kampuni hiyo. Kwa kuwa
Watanzania tuliishaamua kufa na Richmond, tukasonga mbele! Hivyo,
tarehe 2 Septemba 2006, CRDB ikafungua upya LC kwa ajili ya
Richmond Development Company LLC kupitia Benki nyingine ya nje
iitwayo HSBC kwa masharti yale yale ambayo CRDB ilipokea kutoka TANESCO. Hatimaye HSBC ikafungua LC kwa ajili ya kampuni hiyo lakini kwa kutumia jina lingine la RDEVCO na siyo Richmond
Development Company LLC!
4.3 Maombi ya Mapya ya Richmond kubadilisha tena Masharti ya LLC.
Mheshimiwa Spika, baada ya LC kufunguliwa na kuthibitishwa
uwajibikaji kwa utekelezaji wa masharti ya Mkataba ulianza rasmi.
Hata hivyo, tarehe 4 Oktoba 2006, Richmond Development Company
LLC kwa mara nyingine tena, iliipelekea TANESCO maombi ya kutaka
kuifanyia marekebisho ya LC kwamba:-
(i) LC iruhusu malipo ya awali (upfront payment) ya Dola za
Kimarekani milioni 10;
(ii) Richmond Development Company LLC iruhusiwe kusafirisha
mtambo wa kwanza kwa njia ya ndege kwa gharama ya Dola za
Kimarekani 5,696,568.00;
(iii) Asilimia 50 ya Barua ya Dhamana ya Benki ilipwe baada ya
uthibitisho kutoka TANESCO juu ya kupokelewa kwa mitambo nchini.
Mheshimiwa Spika, tarehe hiyo hiyo ya 4 Oktoba, 2006 Wizara ya
Nishati na Madini ikaitisha kikao kujadili maombi hayo. Kikao hiki
kilichohudhuriwa na wawakilishi kutoka Wizara ya Nishati na Madini,
TANESCO, Benki ya CRDB na Richmond Development Company LLC,
kikakubali maombi yote ya Richmond Development Company LLC na
kuagiza kuwa hatua za utekelezaji zifuatie mara moja.
Mheshimiwa Spika, pamoja na ukweli kwamba mchakato mzima
ulitawaliwa na udharura, Kamati Teule haielewi ni vipi Wizara ya
Nishati na Madini ilikuwa ikitekeleza kila pendekezo jipya lililotolewa
na Richmond Development Company LLC bila kujali madhara ambayo
yangewea kutokea pindi kampuni hiyo ingelipwa na kuingia mitini.
Mheshimiwa Spika, baada ya kubaini kwamba mapendekezo hayo
mapya ya kuibeba Richmond yalikuwa nje ya masharti ya LC
yaliyoainishwa katika Mkataba wa malipo kati ya TANESCO, Benki
Kuu ya Tanzania, Wizara ya Fedha na CRDB Bank, Wizara ya Nishati
na Madini ikaijulisha Wizara ya Fedha kuhusu maamuzi mapya ya LC
kutokana na maombi ya Richmond Development Company LLC.
Mheshimiwa Spika, Wizara ya Fedha haikuridhishwa na mapendekezo
yaliyotolewa kwani malipo yoyote ya awali kutoka fungu maalum la Multilateral Debt Relief I nitiative ni lazima yafanyike kwa uthibitisho wa kuridhisha. Sehemu ya barua hiyo iliyoandikwa na Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha, Ndugu Gray Mgonja, inasema:
: “... tunaona kuwa tofauti na taarifa zilizotolewa wakati wa
majadiliano ya Mkataba kuwa mkandarasi aliyechaguliwa alikuwa na
vifaa tayari kuvileta nchini, sasa ni wazi kuwa si hivyo.
Kama unavyojua, msingi wa malipo kuhusu mitambo ya kununua au kukodisha chini ya Mradi wa Nishati ya Dharura unaofadhiliwa kupitia I MF MDRI , ni mkataba unaotokana na majadiliano.
Napenda kupendekeza kuwa malipo yoyote ya awali kutoka akaunti ya MDRI lazima yaandamane na dhamana ya kuridhisha kutoka kwa mkandarasi. Sharti hili linaonyesha kutokuzingatiwa chini ya
mapendekezo yenu”.
Mheshimiwa Spika, pamoja na maelekezo na ushauri huu wa Wizara
ya Fedha, Wizara ya Nishati na Madini siku hiyo hiyo ikaiandikia
barua TANESCO kuitaka itekeleze maombi ya Richmond Development
Company LLC mara moja kubadilisha masharti ya malipo:-
“ . . . I wish to inform you that the proposed amendments to the
existing Letter of Credit are acceptable and you are advised to liaise
with CRDB Bank to effect the changes as soon as is practical. . . .
Barua ya Katibu Mkuu wa Nishati na Madini (Kumb. Na.
CBD.214/ 324/ 01 ya tarehe 6/ 10/ 2006) inasomeka.
Mheshimiwa Spika, Kamati Teule imejiuliza bila kupata majibu: Ni nini
kilifanyika hadi Wizara ya Nishati na Madini ikatoa kauli hii ambayo ni
tofauti kabisa na ushauri ilioupata kutoka Wizara ya Fedha? Nini
msingi wa ukereketwa au ufukukutwa bayana wa Wizara ya Nishati
na Madini kuhusu Richmond?
Mheshimiwa Spika, katika kutekeleza maagizo ya Wizara, TANESCO
iliiandikia barua Benki ya CRDB tarehe 6 Oktoba, 2006 kuitaka
kufanya mabadiliko hayo mapya kwenye LC ya Richmond. Tarehe 9
Oktoba, 2006 Benki ya CRDB iliijibu TANESCO na kuikumbusha
kwamba LC inasimamiwa na makubaliano ya pamoja chini ya
uangalizi wa Benki Kuu ya Tanzania. Kwa msingi huo TANESCO
ikatakiwa kufuata taratibu kwa kuiomba Benki Kuu ya Tanzania kibali
cha kufanya marekebisho katika Kifungu 1(a) cha Mkataba wa
makubaliano ya taratibu za malipo ili kuwezesha maombi
yaliyopendekezwa kufanyiwa kazi. Jibu hilo likailazimu TANESCO
kufuta maombi hayo.
Mheshimiwa Spika, hadi LC hiyo ya Richmond inaisha muda wake
(tarehe 30 Novemba, 2006), kampuni hiyo ya Kimarekani haikuweza
kutekeleza sharti hata moja na hivyo kushindwa kuchukua fedha
kama ilivyokuwa imepangwa. Swali linalojitokeza ni: I wapo CRDB
ingekubali kubadilisha masharti ya LC na kuipa Richmond
Development Company LLC fedha ilizoomba bila kibali cha Benki Kuu
ya Tanzania; Je, Richmond ingeleta nchini mitambo kama
ilivyokusudiwa au ingekuwa ni hasara kwa Taifa?
Kwa upande mwingine, mchakato mzima wa Richmond Development
Company LLC wa kutaka kufanya mabadiliko katika Barua ya
Dhamana ya Benki mara kwa mara unadhihirisha nia yao ya kutaka
kupata mtaji. Pia inadhihirisha kwamba Richmond Development
Company, LLC haikuwa na uwezo wa kifedha wa kutekeleza Mkataba
huu kinyume na tamko kwenye Mkataba kuwa:-
“The Supplier (i.e. Richmond) has the equipment and the financial
and technical capability to construct, install, commission, operate and maintain such a plant as required by TANESCO”. (Msambazaji (yaani Richmond) ana vifaa na uwezo wa kifedha na wa kitaalam kujenga, kusimika, kuiwasha, kuendesha na kuendeleza mtambo huo kama TANESCO inavyohitaji.)
Mheshimiwa Spika, kwa msingi huo Kamati Teule ilijiuliza maswali
yafuatayo:-
(i) Je, utafiti ulifanywa kufahamu gharama halisi za mitambo mipya
kutoka kwa watengenezaji wenyewe bila ya kupitia kwa mawakala?
Kamati Teule ilibaini kuwa zoezi hilo liliwahi kufanyika mwaka 1998 tu
ambapo Wizara ya Nishati na Madini ilitoa kazi hiyo kwa wataalam wa sekta (consultants) na kufanikisha kugundua kuwa bei ya mitambo ya umeme ya I PTL (400 MW) ambayo ilitakiwa kuuzwa kwa Dola za
Kimarekani milioni 150 (Tsh. 187.5 bilioni) bei yake halisi ilikuwa ni
Dola za Kimarekani milioni 85 (Tsh.106.2 bilioni) tu na hivyo kupata
kigezo cha kukataa bei yao. Hivyo basi, kutokana uzoefu huo, Wizara
ya Nishati na Madini kwa kushirikiana na TANESCO walitakiwa
kufuatilia bei hizo za mitambo na pia makadirio ya kazi za ujenzi ili
kupata picha ya gharama halisi ya mradi jambo, ambalo
halikufanyika.
Mheshimiwa Spika, kwa viongozi wa Wizara na TANESCO kushindwa
kujua bei halisi ya mitambo kutoka kwa watengenezaji wenyewe kwa
takribani miaka 10 huku wakisafiri kwenda nje ya nchi kila kukicha
kwa mikutano, warsha, makongamano, n.k, na kwa Wizara
kung’ang’ania kutumia mawakala badala ya watengenezaji wa
mitambo, nchi yetu imegeuzwa gulio la wajanja kuikamua na
kuwabebesha wananchi mzigo wa kodi.
Mheshimiwa Spika, Kamati Teule ilipotembelea Marekani, iliamua
kuwatembelea baadhi ya watengenezaji wa mitambo ya uzalishaji wa
umeme huko huko Houston Marekani kujua bei za mitambo yao.
Mmoja wa watengenezaji wenye jina kubwa duniani, Kawasaki Gas
Turbines – Americas, anatengeneza na kuuza Mtambo mpya aina ya
GPB180 wenye uwezo wa kuzalisha MW 17.5 kwa Dola za Kimarekani
7.5 milioni (Tsh. 9.4 bilioni). Mawakala huwa wanatuletea mitambo
ya aina hiyo hiyo kwa bei mara mbili ya bei halisi.
(ii) I wapo TANESCO au Serikali iliweza kufungua LC ya Dola za Kimarekani 30,696,598; je, fedha hizo zisingeweza kutosheleza kununua mitambo mipya ya uzalishaji umeme, na mitambo hiyo
kubakia mali ya TANESCO, badala ya kuingia katika Mikataba ya ghali
ya kukodisha mitambo?
Aidha, taarifa za watendaji wa Wizara ya Nishati na Madini kwamba
wakati wa kipindi cha mchakato wa zabuni ya umeme wa dharura
kulikuwa na ugumu wa kupatikana mitambo ya umeme wa dharura
zimethibitishwa na Kamati Teule kuwa sio za kweli. Mheshimiwa Spika, ni ukweli kwamba kulikuwa na ukame, lakini
ukame huo haukuwa wa mitambo ya kuzalisha umeme kwani
mitambo hiyo hutengenezwa muda wote na sio kwa kutegemea
mvua. Aidha, utafiti wetu umebaini kuwa katika kipindi hicho cha
matatizo ya umeme nchini, kampuni zote za kutengeneza mitambo
hiyo ya umeme zilikuwa zina mitambo kadhaa ikisubiri wateja.
Kawasaki ilikuwa na mitambo 8 ya kisasa tena yenye kutumia gesi na
dizeli (dual fuel plant). Serikali nyingi, ikiwemo ya Nigeria, ni wateja
wazuri wa kampuni hiyo ambao huteremshiwa bei kwa mtambo moja
hadi Dola za Kimarekani milioni 6.7 milioni badala ya Dola za
Kimarekani milioni 7.5 bei ya kawaida.
Mheshimiwa Spika, kwa thamani ya LC iliyofunguliwa kwa Richmond
Development Company LLC ya Dola za Kimarekani milioni 30.7 au
Tsh 38.4 bilioni, TANESCO ingeweza kununua mitambo mipya yote
minne pamoja na kumudu kulipia gharama za kusafirisha kwa meli
hadi Dar-es-Salaam. Hivyo ili zipatikane MW 105.6 zilizohitajiwa na
TANESCO ingehitajika mitambo sita (6) ambayo ni sawa sawa Dola za
Kimarekani milioni 45 au Tsh. 56.25 bilioni badala ya Dola za
Kimarekani milioni 87 au Tsh. 108.7 bilioni tulizobebeshwa na
Richmond Development Company LLC.
Mheshimiwa Spika, Je, si dhahiri kuwa hii ndiyo ilikuwa nia ya
Richmond Development Company LLC, yaani kupata fedha za malipo ya awali (advance payment) ili ikatununulie mtambo mmoja na kuja kutukodisha sisi wenyewe, hivyo kufaidika na capacity charge ya kila mwezi kwa Mkataba wa miaka miwili? Kwa mtambo mmoja wa MW 22, capacity charge ni Dola za Kimarekani takriban 730,871 au Tsh. Milioni 913.6 kwa mwezi, hivyo kwa miezi 24 ni wastani wa Dola za Kimarekani 17,540,912 au Tsh. Bilioni 21.9.
(iii) Kwa kuwa thamani ya LC inalipwa kama malipo ya awali
(advance payment), Je, hii si sawa na kutoa mkopo kwa Richmond Development Company LLC? Kamati Teule inaona kwamba hiyo ni sawa na kutoa mkopo usio na riba kwa mfanyabiashara wa nje ili awe mwekezaji.
(iv) Kwa nini katika Mkataba wa Richmond Development Company
LLC kifungu cha kufidia malipo ya awali (advance payment) ya LC
hakikuwekwa bayana ndani ya Mkataba tofauti na Mikataba mingine,
badala yake ikawekwa fursa ya kujadiliana na mkandarasi? Kamati
Teule haioni sababu yeyote ya msingi mbali na wahusika kujiwekea
fursa ya kukidhi maslahi yao binafsi.
3.0 5.0 TAARI FA ZA PPRA na TAKURU
3.1 5.1 Taarifa ya PPRA
3.2
3.3 Mheshimiwa Spika, uamuzi wa Serikali wa kuipa Richmond
Development Company LLC zabuni ya kuzalisha umeme wa dharura
wa MW 105.6 na baadaye kuingia mkataba na TANESCO, ulizua
mjadala wa manung’uniko ya wananchi wa kada mbalimbali
walioshuhudia kushindwa kwa kampuni hiyo kutekeleza mradi huo
katika muda muafaka. Umma wa Watanzania wa kawaida,
wanasiasa, wasomi, wanataaluma, wanahabari, na wadau mbalimbali hawakusita kuilalamikia Serikali kwa uteuzi huo wa Richmond ambao walihisi kuwa uligubikwa na maslahi binafsi ya baadhi ya viongozi.
3.4 Mheshimiwa Spika, Mamlaka ya Udhibiti wa Ununuzi wa Umma
(PPRA) na Taasisi ya Kuzuia Rushwa (TAKURU) ambayo sasa ni Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU), kwa mamlaka ya kisheria ambayo taasisi hizi inayo, zikaamua
kulichunguza suala hili.
3.5
3.6 Mheshimiwa Spika, kwa ujumla PPRA ilifanya uchunguzi makini
na wa kina kujua kama Sheria na Kanuni za Ununuzi wa Umma
zilifuatwa. Taarifa hiyo imebainisha wazi kuwa pamoja na nia nzuri ya
Serikali ya kutaka kuiokoa nchi kutokana na hali mbaya ya umeme,
mchakato mzima wa zabuni ulikiuka Sheria ya Ununuzi wa Umma ya
Mwaka 2004 na Kanuni za Ununuzi wa Umma za Mwaka 2005 kama tulivyoelezea kwa kina sehemu ya pili ya taarifa hii fupi. Kwa ujumla Kamati Teule imeridhishwa na taarifa ya PPRA ambayo imeandikwa kitaalamu ikiwa na vielelezo vya wazi ambavyo Mamlaka imevitumia.
5.2 Taarrifa ya TAKURU
Mheshimiwa Spika, kwa ujumla uchunguzi uliofanywa na TAKURU,
ambao taarifa yake unadai kuwa ulikuwa wa “kina na wenye umakini
wa hali ya juu’’ ulibaini kwamba:-
Mchakato wa kumpata mzabuni ulikuwa wa wazi na shindanishi;
Hakuna ushahidi uliopatikana kuthibitisha vitendo vya rushwa,
uzembe na hata kupokea kamisheni. Pia hakuna ushahidi
uliopatikana wa Afisa yeyote Serikalini kumiliki hisa au kuwa na
madaraka katika Richmond Development Company LLC;
Kamati maalum iliyoundwa haikupata muda wa kutosha kuifanyia
uchambuzi wa kina Richmond Development Company LLC ili
kufahamu uwezo wake kiufundi na kifedha na badala yake ilitegemea
uwezo wa Kampuni ya Pratt & Whitney kama kigezo cha kuipatia
Richmond zabuni;
Utafiti wa kina haukufanywa kutambua uwezo wa Kampuni ambayo
ingepaswa kusimamia shughuli za Richmond Development Company
LLC yaani Richmond Development Company (T) Ltd; na
Mapungufu machache yalikuwepo lakini ya “kawaida kiutendaji” na hayakuhusisha rushwa au manufaa ya aina yeyote ile kwa watendaji wa Serikali na wala hakuna hasara iliyosababishwa na mapungufu hayo.
Mheshimiwa Spika, Kamati Teule ilishindwa kuona mantiki ya
matokeo ya uchunguzi wa TAKURU kama ifuatavyo:-
(i) Mchakato ambao TAKURU imedai kuwa ulikuwa wa wazi na
shindanishi uliendeshwa na Wizara ya Nishati na Madini bila
kuzingatia taratibu za sheria na kanuni za ununuzi wa umma.
Kamati Teule imeshindwa kuelewa ni mbinu zipi taasisi hii ilitumia
katika kueleza kuwa mchakato wa zabuni ulifanywa kwa uwazi na
kuwa shindanishi. Je, uwazi gani na ushindanishi gani ulikuwepo kwa
Wizara ya Nishati na Madini ikishirikiana kwa karibu na Ofisi ya Waziri
Mkuu, kusitisha mchakato wa zabuni ndani ya TANESCO na kuunda
chombo kipya nje ya taratibu ili kumteua mzabuni kwa niaba ya
TANESCO?
(ii) Hoja ya TAKURU kuwa kulikuwa na mapungufu, lakini mapungufu
hayo yalikuwa ya kawaida ambayo hayajengi makosa ya jinai haina
msingi. Kwa Wizara kuilazimisha taasisi nyingine ya ununuzi, yaani
TANESCO, kusaini Mkataba ambao haukupitishwa na vyombo vyake vya maamuzi; kwa kampuni hiyo ya Kimarekani kujitambulisha kwa majina mbalimbali katika mchakato huo: mara Richmond
Development Company LLC, mara RDC, RDVECO, na mara nyingine
RDEVCO; yote haya kwa TAKURU ni makosa ya “kawaida ya
kiutendaji”?
(iii) Taarifa ya TAKURU imeeleza kwamba Richmond Development Company LLC ilikuwa ifunguliwe Letter of Credit yenye thamani ya Dola za Kimarekani 30,696,598.00. Sawa, lakini TAKURU haikuona jitihada za kampuni hiyo kujaribu kubadilisha masharti ya LC hiyo
mara ratu? TAKURU haikushangazwa na benki za Kimarekani kukataa
kuihudumia kampuni ya Kimarekani? TAKURU haikushangazwa na
kiherehere cha Wizara ya Nishati na Madini kutekeleza matakwa na
kampuni hiyo hata pale ambapo yalikwenda kinyume na makubaliano
ya msingi?
(iii) TAKURU haikuona hasara ambayo nchi ilipata kutokana na zabuni
hiyo wakati kila mwananchi aliona hasara bayana kwa nchi kukosa umeme kwa kipindi kirefu na kuathiri uzalishaji mali na huduma za lazima nchini.
(iv) TAKURU iliamini kuwa hakukuwa na uzembe. Je, kwa Wizara na
watendaji mbalimbali wa Serikali kuamini kuwa Richmond
Development Company LLC na Pratt & Whitney zilikuwa na ubia bila
kudai nyaraka za ubia; kwa viongozi wa Serikali kumwona tu mzungu
na business card yake, na kuamini moja kwa moja kuwa ni mwakilishi
wa Pratt & Whitney wakati siyo; kwa Serikali kuamua kusaini
Mkataba na kampuni ambayo haijafanyiwa uchunguzi wa kina
kujiridhisha kuwa si kampuni hewa au ya mkobani; hivyo vyote kweli
si uzembe?
(v) Pamoja na kuwajibika kisheria kujisajili kwenye Bodi ya Usajili ya
Makandarasi, na wahandisi wake kusajiliwa na Bodi ya Usajili wa
Wahandisi (ERB), Richmond Development Company LLC haikufanya
hivyo na ililindwa na Wizara ya Nishati na Madini kubaki kama
ilivyokuwa! Hilo nalo TAKURU haikuliona?
(vi) Richmond Development Company LLC, haikuwa na nyaraka
zozote za kikampuni kuonyesha kuwa imesajiliwa Marekani, haikuwa
na uthibitisho wa kibenki kuwa ina fedha kuendesha mradi wa
umeme ili kupata sifa ya uwekezaji nchini, haikuwa na Business Plan
iliyoandaliwa vizuri na kwa uangalifu, klakini ikapata huduma ya
haraka Kituo chetu cha Uwekezaji na kupewa Certificate of
I ncentives.
Mheshimiwa Spika, ikizingatiwa kuwa TAKURU ni taasisi nyeti Kitaifa
ambayo ina uwezo wa kutosha kitaaluma, kifedha na kirasilimali watu
katika kufuatilia masuala mbalimbali ya uchunguzi, haikuwatendea
haki Watanzania kwa kazi ya ubabaishaji iliyofanya.
Mkurugenzi wa Upelelezi na Makosa ya Jinai wa TAKURU ndugu Alex
Mfungo aliitetea Taasisi yake mbele ya Kamati Teule kuwa ilifanya
uchunguzi kwa mujibu wa sheria ya mwaka 1971 iliyokuwa na
mapungufu mengi na kwamba ilikuwa vigumu sana kuthibitisha
madai ya rushwa yaliyokuwa yanalalamikiwa na wananchi
Mheshimiwa Spika, pamoja na utetezi huo, bado TAKURU haikufanya
kazi iliyotegemewa na wananchi kufanya ya kufichua uovu.
I lichofanya ni kuuficha ukweli kwa hoja za ubabaishaji.
5.3 5.4 5.5
5.6 5.3 Vyombo vya Habari – Magazeti
5.7
Mheshimiwa Spika, vyombo vya habari hususan magazeti vilifanya
kazi kubwa na ya ziada katika kutafuta ukweli kuhusu suala hili. Ni
vyombo hivi vya habari kupitia makala mbalimbali, tahariri na taarifa
maalum, vilivyoamsha shauku ya wananchi kuhusu suala hili.
Naomba kuchukua fursa hii, Mheshimiwa Spika, kuvipongeza vyombo
vyote vya habari, wamiliki wake, wahariri, waandishi wa habari,
watangazaji na wapiga picha kwa ujasiri na moyo wa kizalendo katika
kupambana na kila aina ya ufisadi kwa kutumia kalamu.
Mheshimiwa Spika, ufuatiliaji wa karibu wa vyombo vya habari
kuhusu suala hili ulikuwa moja ya sababu kubwa kwa Richmond
Development Company LLC kujitoa mapema kwenye Mkataba huo.
Mmiliki wa Kampuni hiyo Bw. Mohammed A. Gire alikiri mbele ya
Ujumbe wa Kamati Teule uliotembelea Houston, Texas, Marekani
kuwa moja ya sababu zilizoifanya kampuni yake kusitisha shughuli
zake ni kutokana na kuandamwa kwa kuandikwa kila siku na vyombo
vya habari vya Tanzania. I kamlazimu kuajiri kampuni ya G&S Media
Consultancy ili kupunguza makali ya maumivu aliyokuwa anayapata,
haikusaidia.
Mheshimiwa Spika, Kamati Teule inakumbushia ahadi ya Serikali ya
kuanzisha mafunzo maalum ndani na nje ya nchi kwa ajili ya
kuwawezesha wanahabari kuongeza ujuzi na kujenga uzoefu wa
kuhoji na kuandika habari za uchunguzi wenye kina stahili, shughuli
ambayo ni sehemu muhimu ya kuimarisha demokrasia na utawala
bora nchini.
6.0 RI CHMOND DEVELOPMENT COMPANY LLC NI KI NA NANI ?
6.1 Utambulisho wake Kisheria
Mheshimiwa Spika, Mkataba wa uzalishaji umeme wa dharura
unaielezea kwenye utangulizi Richmond Development Company LLC
kuwa ni kampuni iliyosajiliwa chini ya sheria za Jimbo la Texas,
Marekani na yenye anuani ifuatayo: 5825 Schumacher, Houston
Texas 77057, Marekani. Aidha, kifungu cha 5.1 (a) cha Mkataba huo
kinatoa maelezo ya ziada kuhusu Richmond Development Company
LLC kuwa ni kampuni yenye ukomo wa hisa (limited by shares)
ambayo uwepo wake Tanzania haukinzani na sheria za nchi. Kifungu
hicho kidogo kinamalizia kwa kutamka bayana kuwa kampuni hiyo ina
nguvu na mamlaka yote stahili ya kikampuni (all requisite corporate power and authority) ya kumiliki au kukodisha na kutumia mali zake na kuendesha biashara zake kama ilivyokusudiwa nchini Tanzania.
Mheshimiwa Spika, hiyo ndiyo sura ya Richmond Development
Company LLC kama ilivyoainishwa katika Mkataba huo wa kisheria
uliotiwa saini kwa upande wa TANESCO na aliyekuwa Kaimu
Mkurugenzi Mwendeshaji wa TANESCO, Johannes G. Lottering na
kushuhudiwa na aliyekuwa Kaimu Katibu (Ag. Company Secretary)
wa TANESCO, Godson Makia na kwa upande wa Richmond na Meneja
wake, Mohamed Gire na kushuhudiwa na wakili maarufu nchini, Dr.
Ringo Tenga ambaye alijitambulisha katika mkataba huo kama Katibu
wa Richmond Development Company LLC.
6.2 Hadhi ya Richmond kisheria/ kikampuni Marekani
Mheshimiwa Spika, uchunguzi wa kina uliofanywa na Kamati Teule
ndani na nje ya nchi na kwa msaada mkubwa wa Ubalozi wa
Tanzania Washington D.C na Wizara yetu ya Mambo ya Nje na
Ushirikiano wa Kimataifa, umetoa picha tofauti kabisa na ile iliyomo
kwenye mkataba huo. Kamati Teule imejiridhisha kuwa hakuna
kampuni yenye jina la Richmond Development Company LLC
iliyokuwa imesajiliwa Jimbo la Texas wakati wa kusaini mkataba huo
au iliyosajiliwa baada ya mkataba huo hadi tunapowasilisha ripoti hii
kwa Mhe. Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
tarehe 31 Disemba, 2007.
Hitimisho tulilofikia linashabihiana kwa vigezo vyote na ushauri wa
kitaalamu uliotolewa na kampuni mashuhuri ya mawakili ya Virginia, Marekani inayoitwa Hunton & Williams LLP kwa Bodi ya Wakurugenzi ya TANESCO mwezi Oktoba 2006. Katika ripoti yake yenye jumla ya kurasa 19, kampuni hiyo ya mawakili imetamka bayana kuwa hakuna kampuni yenye jina la Richmond Development Company LLC kwenye masijala ya Katibu wa Jimbo la Texas ambaye moja ya majukumu
yake ni sawa na ya Msajili wa Makampuni wa Tanzania.
Hunton & Williams LLP wameituhumu Richmond Development
Company LLC kwa upotoshaji wa hadhi yake kikampuni
(misrepresentation of its corporate status) na kutoa tamko lisilo
sahihi (incorrect statement) kuhusu hadhi yake chini ya sheria za
Texas. Ukaguzi wa kumbukumbu za Katibu wa Jimbo la Texas
uliofanywa na kampuni hiyo ya mawakili Oktoba 2006, ulionesha
kuwa hakuna kampuni yenye jina la “Richmond Development
Company LLC” iliyokuwa imeanzishwa na kuendesha shughuli zake
jimboni Texas wakati huo.
Mheshimiwa Spika, aidha, tarehe 10 Oktoba, 2006 gazeti la kila siku
la Kiingereza linalochapishwa hapa nchini, The Citizen, lilimkariri afisa
mmoja katika Jimbo la Texas, Bw. William Pate, akisema makampuni
yote yanayofanya biashara halali jimboni humo yana kumbukumbu
zake katika ofisi ya Katibu wa Jimbo la Texas. Alisema ofisi hiyo haina
taarifa au kumbukumbu zozote kuhusu kampuni hiyo inayojiita
Richmond Development Company LLC.
Wajumbe wa Kamati Teule waliotembelea Marekani kati ya tarehe 10
na 16 Disemba, 2007 waliambiwa na Bwana Mohamed Gire, kuwa
Richmond Development Company LLC ni jina mbadala la biashara la
kampuni yake iitwayo RDEVCO LLC. Bwana Gire ambaye aliamua
mkutano wake na Wajumbe wa Kamati Teule ufanyike ofisini kwa
wanasheria wake, Duane Morris LLP waliopo 3200 Southwest
Freeway, suite 3150, jijini Houston, alisisitiza kuwa sheria za Texas
zinawaruhusu wafanyabiashara na makampuni kutumia majina
mbadala au tofauti na yale yaliyopo kisheria kwa sababu za
kibiashara. Kamati Teule iliyazingatia maelezo ya Bwana Gire kwa
lengo la kuyafanyia kazi.
Ni kweli kabisa kuwa majimbo mengi Marekani, likiwemo la Texas,
yanaruhusu matumizi ya majina mbadala katika biashara au huduma.
Kwa Kiingereza majina hayo yanaitwa “assumed names” au “dba”,
kwa kirefu: “doing business as”. Katika nchi nyingine nyingi kama vile
Tanzania, Uingereza, I reland, Australia na baadhi ya majimbo ya
Marekani na sehemu za Kanada, neno linalotumika zaidi ni “t/ a”,
yaani “trading as”.
Mheshimiwa Spika, katika nchi zote hizo, sheria zinaweka taratibu za
kuzingatia ili kuepusha vitendo vya kitapeli katika matumizi ya majina
mbadala ya kibiashara. Nchini Tanzania na nchi zingine za Jumuiya ya Madola, zipo sheria maalum za usajili wa majina ya biashara tu ambapo kampuni au mfanyabiashara au mtu yeyote yule ambaye kwa sababu za kibiashara au vinginevyo, asingependa kutumia jina lake halali katika biashara fulani, anaweza kusajili jina mbadala kwa
biashara hiyo bila kulazimika kuunda kampuni tofauti. Majina
mbadala ya kibiashara hapa kwetu Tanzania yanasajiliwa chini ya
Sheria ya Usajili wa Majina ya Biashara (Business Names
(Registration) Ordinance) Sura ya 213.
Nchini Marekani vilevile, huwezi ukakurupuka tu na kuanza kutumia
jina mbadala la biashara bila kupitia usajili maalum ambao
unawawezesha watu wengine kukagua jalada la majina hayo
mbadala kwa lengo la kupata utambulisho kamili wa wanayoyatumia.
Vilevile, sheria zinalazimu majina hayo kuchapishwa magazetini kwa
lengo la kuutaarifu umma. Lengo, kama tulivyodokeza awali, ni
kulinda raia wema dhidi ya vitendo vya udanganyifu.
Katika Jimbo la Texas ambako Bwana Gire anaishi, ni kosa la jinai
kutumia jina mbadala bila kulisajili. Usajili wa jina mbadala unadumu kwa miaka mitano ambapo mtumiaji lazima asajili jina hilo upya kati ya tarehe 1 Januari na 31 Disemba ya mwaka wa tano.
Sasa je, ni kweli kwamba jina la Richmond Development Company
LLC ni jina mbadala la kampuni ya Bwana Gire iitwayo RDEVCO LLC? Je, jina hilo lilisajiliwa ipasavyo? Katika kujibu maswali hayo mbele ya mawakili wake wawili, Bwana Gire aliwakabidhi Wajumbe wa Kamati Teule hati ya uthibitisho ya Harris County, Texas ambayo kwa maoni yake, ilikuwa inathibitisha kuwa Richmond Development Company
LLC ni jina mbadala la biashara!
Kamati Teule imeikagua hati hiyo kwa kina na kuona kuwa badala ya
kumsaidia Bwana Gire, inazidi kuthibitisha kuwa si mfanyabiashara
mwadilifu ila tapeli kwa sababu kuu mbili:
(a) Mbali na kwamba hati hiyo ya Bwana Gire ni kivuli tu au nakala ya
“hati” halisi (kama ipo), nakala ambayo haina uthibitisho wowote wa
uhalali na uhalisia wake, ilikuwa ina saini ya afisa mmoja tu badala ya
wawili walioainishwa katika hati hiyo;
(b) Badala ya hati hiyo kutamka kuwa RDEVCO LLC imesajili jina la
Richmond Development Company LLC kama Bwana Gire alivyotaka
Kamati Teule ielewe, hadithi mpya kabisa inaanzishwa kuwa
Richmond Development Company ni jina mbadala lililosajiliwa na
Richmond Development Company LLC! La kushangaza ni kuwa katika baadhi ya barua zake alizoiandikia TANESCO na Wizara ya Nishati na Madini, Bw. Gire anatamka kuwa Richmond Development Company ni jina mbadala la biashara la RDEVCO LLC,
Mheshimiwa Spika, mtu anaweza akadanganyika akafikiri kuwa
kiwango hiki cha ubabaishaji hakithibitishi utapeli pekee, bali vilevile
elimu duni ya mmiliki wa kampuni hizo, Bwana Gire, inayomfanya
asione hatari kubwa anayojitwalia ya hata kumfikisha jela kwa
udanganyifu. Lakini kwa mfanyabiashara mzoefu aliyejizungushia
mawakili wa kumtetea mambo yakimwendea mrama, anajua
analolifanya. Hivyo basi, Richmond Development Company LLC ni
kampuni ya kimakusudi, ya kimkakati ambayo haikamatiki,
haishitakiki, haipigiki faini na haiadhibiki kwa lolote lile itakalolifanya
kwani haina uhai wa kikampuni (corporate personality).
Mheshimiwa Spika, pamoja na Bwana Gire kuamua kufanyia mkutano
wake na Wajumbe wa Kamati Teule ofisini kwa wanasheria wake na
si kazini kwake mwenyewe, Wajumbe walihakikisha kuwa
wanatembelea mtaa unaotajwa kwenye mkataba kuwa ofisi za
Richmond Development Company LLC, yaani 5825 Schumacher,
Houston Texas, 77057, USA. Anuani hiyo ikawafikisha kwenye jengo
lenye jina la Richmond Printing LLC, jina walilothibitisha kuwa la
kampuni iliyosajiliwa chini ya Sheria ya Kampuni yenye Ukomo wa
Hisa ya Texas (Texas Limited Liability Company Act) tarehe 1 Agosti,
1994 kwa madhumuni ya kuendesha biashara ya uchapishaji na
biashara zingine zinazoruhusiwa na sheria kwa kampuni ya aina hiyo.
Kampuni hiyo ilianzishwa ikiwa na mwanahisa na meneja mmoja tu
kwa jina Mohamed Gire.
Aidha, Wajumbe wa Kamati Teule wakatambua kuwa jengo hilo la
Richmond Printing LLC linatumiwa vilevile kama ofisi za RDEVCO LLC,
kampuni ambayo ilisajiliwa chini ya sheria hiyo hiyo ya Texas tarehe
11 Septemba, 2003 ikiwa na madhumuni mapana ya kujishughulisha
na “biashara yoyote halali”. Kampuni hiyo vilevile ilianzishwa ikiwa na
mwanahisa na meneja mmoja tu kwa jina Mohamed Gire.
Tunalazimika kusema kuwa jengo hilo vilevile ni “makao makuu” ya
kampuni hewa ya Richmond Development Company LLC

Licha ya kutumia jengo moja, kampuni zote hizo zinamhusu mtu
mmoja, Mohamed Gire, na zinatumia anuani moja. Kutokana na
uchambuzi huu, ni wazi kuwa maelezo yaliyomo kwenye utangulizi
wa Mkataba kati ya Richmond Development Company LLC na
TANESCO kuwa chombo hicho cha biashara cha Bw. Gire ni “kampuni
iliyosajiliwa chini ya sheria za Jimbo la Texas”, si sahihi hata kidogo.
6.3 Hadhi ya Richmond kisheria/ kikampuni Tanzania
Mheshimiwa Spika, Richmond Development Company LLC si jina geni
Tanzania. Jina hilo lilianza kusikika nchini kwa mara ya kwanza
mwaka 2003 na kwa kishindo likihusishwa na mradi mkubwa wa
takriban shilingi bilioni 400 wa ujenzi wa bomba la mafuta la urefu
wa kilometa 1,150 kutoka Dar es Salaam hadi Mwanza.
Mheshimiwa Spika, katika barua yake ya kujitambulisha iliyotumwa
kwa Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini na Mkurugenzi
Mkuu wa Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC) tarehe 28
Mei, 2003, Richmond Development Company wakati huo ikijiita kwa kifupi RDC, ikajitambulisha kuwa kampuni yenye uzoefu wa zaidi ya miaka 25 katika miradi ya nishati na kwamba imekamilisha miradi mbalimbali ya aina hiyo kwa zaidi ya Dola za Kimarekani milioni 500 katika nchi zinazoendelea. Kutokana na wasifu huo, TPDC ikawapa
RDC nakala ya ripoti ya upembuzi yakinifu iliyofanywa na kampuni ya
COWI consult (Tanzania) Consulting Engineers and Planners Ltd
mwaka 1997 ili kupata taarifa za awali kuhusu mradi huo. Aidha
Wizara ya Nishati na Madini ikairuhusu RDC kuleta mapendekezo ya
awali kuhusu mradi huo.
Mapema mwezi Oktoba, 2003 Wizara ikapokea mapendekezo ya
awali ya mradi kutoka RDC ambayo yalipitiwa na wataalamu wa
Wizara na TPDC na kukutwa na mapungufu mengi yakiwemo:
kukosekana kwa tathmini za kifedha na za kiuchumi za mradi,
kukosekana kwa tathmini za mazingira, na kukosekana kwa mpango
wa kuwapa makazi waathirika katika njia ya bomba. Kutokana na
mapungufu hayo, Wizara ikasita kuipa RDC mradi huo muhimu na
kuitaka kampuni hiyo kwanza irekebishe mapungufu yote
yaliyojitokeza. RDC nayo ikaweka sharti la kupewa upendeleo wa
kutoruhusu kampuni nyingine kwenye mradi huo kwa kipindi maalum
(exclusivity period) ili kukamilisha kazi hiyo bila wasiwasi wa
kunyang’anywa mradi.
Mheshimiwa Spika, tarehe 30 Juni, 2004 Mhe. Daniel Yona, wakati huo Waziri wa Nishati na Madini na Bwana Mohamed Gire, wakati huo akijiita Mwenyekiti wa RDC, wakasaini mkataba wa awali
(Memorandum of Understanding) ulioipa RDC exclusivity period ya
miezi 18 kufanya upembuzi yakinifu wa kina. Mkataba huo, pamoja
na mambo mengine, uliitaka RDC kuipa Wizara ripoti za maendeleo
ya utekelezaji wa mradi kila baada ya miezi sita na uliipa Wizara
jukumu la kuhakikisha kuwa mradi huo unatekelezwa na RDC mara
baada ya zoezi la upembuzi yakinifu wa kina kufanikishwa.
Mheshimiwa Spika, tangu mkataba huo usainiwe, RDC haikuonekana
tena ikijishughulisha na utekelezaji wa sehemu yake ya mkataba.
Kumbukumbu za mawasiliano kati ya Wizara na kampuni hiyo,
zimetawaliwa na malalamiko ya watendaji wa Wizara kuhusu
ubabaishaji wa RDC. Hatimaye tarehe 9 Januari, 2006, Ndugu. Bashir
J. Mrindoko, kwa niaba ya Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na
Madini, akaiandikia barua RDC kuitaarifu kuwa mkataba kati yake na
Wizara kuhusu bomba la mafuta ulikoma tarehe 30 Disemba, 2005
na wawekezaji wengine sasa wanapewa fursa kuendelea na mradi
huo.
Sehemu ya barua ya Katibu Mkuu inasomeka hivi: “The Ministry of
Energy and Minineral (sic) notes with regret that throughout the 18
month exclusivity period, in spite of several reminders, the Richmond Development Company failed to honor its obligations as provided for in Art.2.1 and 2.2 of the Memorandum”. (Wizara inasikitika kuwa kwa kipindi chote cha miezi 18 ya upendeleo, Richmond Development
Company, pamoja na kukumbushwa mara kwa mara, ilishindwa
kuheshimu wajibu wake kama ulivyoainishwa katika I bara ya 2.1 na
2.2 ya Mkataba).
Mheshimiwa Spika, naomba turejee kwenye hoja ya awali ya kupima
ukweli uliomo kwenye kifungu cha 5.1 (a) cha Mkataba kati ya
TANESCO na kampuni hiyo ya Richmond tulichokinukuu awali
kinachosema Richmond Development Company LLC ni kampuni
yenye ukomo wa hisa ambayo uwepo wake Tanzania haukinzani na
sheria za nchi na kwamba kampuni hiyo ina nguvu na mamlaka yote
stahili ya kikampuni ya kumiliki au kukodisha na kutumia mali zake na
kuendesha biashara zake nchini.
Katika kupima ukweli wa kauli hizo ndani ya mkataba, kikwazo
kikubwa cha mwanzo ambacho Kamati Teule ilikipata kilikuwa ni
msingi wa kuichunguza Richmond Development Company LLC kama
kampuni wakati uhalali wake kama kampuni huko ilikotoka
unabishaniwa au kwa lugha iliyonyooka, haupo. Richmond
Development Company LLC, kwa maneno mengine, si kampuni ya mchana bali ya usiku, kampuni ya mfukoni au ya sanduku la barua (mail box company)! Hiyo ndiyo kampuni ambayo shirika la umma,
TANESCO, iliingia nayo mkataba wa mabilioni ya fedha za walipa kodi
wa Tanzania.
Mheshimiwa Spika, kampuni ya wanasheria ya Kimarekani ya Hunton
& Wiliams LLP iliyopewa kazi na Bodi ya Wakurugenzi ya TANESCO
kuichunguza Richmond Development Company LLC, kama
tulivyoeleza hapo awali, inathibitisha kuwa tarehe 23 Juni, 2006 siku ambayo mkataba huo ulisainiwa, Richmond Development Company LLC haikuwa na nguvu za kisheria wala mamlaka yoyote ya
kikampuni kuiwezesha kuendesha shughuli zake Tanzania.
Kamati inaamini kuwa wamiliki au waendeshaji wa kampuni hiyo
wanaotambulishwa kwenye tovuti ya kampuni hiyo
(www.rdevco.com), Bwana Mohamed A. Gire na Dk. Mohammed S.
Huque, waliliona tatizo hilo na kuamua siku 19 tu baada ya kusainiwa
kwa Mkataba huo kusajili kampuni mpya kwa jina la Richmond
Development Company (T) Limited yenye makao yake makuu jijini Dar es Salaam. Kampuni hiyo mpya ilisajiliwa tarehe 12 Julai, 2006 na kupewa Hati ya Usajili nambari 57014 ikiwa na wanahisa wawili, kwa majina:
1. Richmond Development Company LLC yenye anuani ya 5825
Schumecher (tunadhani ni Schumacher), Houston – Texas 778057
USA (hisa 750,000) na
2. Naeem Gire wa S.L.P. 1998, Dar es Salaam (hisa 250,000).
Mheshimiwa Spika, kwa kusajili kampuni hiyo mpya, ni dhahiri kuwa
wamiliki wa kampuni hiyo walitaka wasibanwe na Kifungu cha 434
cha Sheria ya Makampuni ya Tanzania (Na. 12 ya 2002)
kinachotamka wazi kuwa kampuni zote za nje ambazo zinaanzisha
ndani ya nchi mahali pa biashara (a place of business), zinawajibika
kuwasilisha kwa Msajili wa Makampuni taarifa mbalimbali za kampuni
ndani ya siku 30 toka zianzishe mahali pa biashara, kama vile: sheria
au mkataba unaoelezea muundo wa kampuni (charter, statutes or
memorandum and articles of association); orodha ya wakurugenzi na
katibu wa kampuni; anuani kamili ya ofisi kuu ya kampuni; na nakala
ya taarifa ya mahesabu ya kampuni na shughuli za kampuni.
Mheshimiwa Spika, kwa kutekeleza masharti yote chini ya kifungu
cha 434 cha Sheria ya Makampuni ya 2002, kampuni ya nje
itathibitishwa na Msajili wa Makampuni kuwa imetimiza masharti.
Uthibitisho huo utakuwa ushahidi kamili wa usajili wa kampuni hiyo
ya kigeni nchini ambao utaipa kampuni hiyo haki sawa na kampuni
iliyosajiliwa Tanzania katika kumiliki ardhi. Ni dhahiri kuwa taarifa
zinazodaiwa chini ya kifungu hicho cha sheria zisingeweza kutolewa
na Richmond Development Company LLC, kwa sababu kampuni hiyo
isiyo na usajili stahili Marekani haiwezi kuwa nazo.
Pamoja na juhudi hizo za wamiliki wa kampuni ya Richmond, Kamati
Teule ilibaini kutokana na ushauri mbalimbali iliopata wa kisheria, kuwa tatizo la uhalali wa Richmond ya Tanzania lilikuwa palepale kwani kifungu cha 3(1) cha Sheria ya Makampuni kinataka watu wawili au zaidi kuwa na uwezo wa kufungua kampuni. Kwa kuwa mmoja wa wanahisa waliofungua kampuni hiyo ya Richmond ya Tanzania ni Richmond Development Company LLC ya Marekani (yenye asilimia 75 ya hisa zote za kampuni hiyo iliyosajiliwa
Tanzania) na kwa kuwa kampuni hiyo ya kimarekani haijasajiliwa
Marekani wala hapa Tanzania kwa mujibu wa kifungu cha 434 cha
Sheria ya Makampuni na kwa kuwa, kutokana na hiyo sababu,
kampuni hiyo ya kimarekani haina nguvu wala mamlaka stahili ya
kikampuni, Richmond Development Company (T) Limited ina
mwanahisa mmoja tu kwa jina Naeem Gire, hali ambayo haikubaliki
kisheria.
Mheshimiwa Spika, ni wazi kuwa picha iliyojengwa kwenye mkataba
tunaouongelea hapa kuhusu hadhi na uhalali wa Richmond
Development Company LLC nchini Tanzania ilikuwa ya kisanii, ya
uongo na isiyo na msingi wowote kisheria. Kinachosikitisha hapa ni
kuwa mwezi Februari, 2006, yaani mwezi moja tu baada ya Wizara
ya Nishati na Madini kuiandikia barua Richmond Development
Company LLC kuwa haina imani nayo, “kampuni” hiyo ya Bwana Gire,
ikajitosa kwenye zabuni nyingine ya Wizara hiyohiyo ya Nishati na
Madini, zabuni ya kuingiza nchini jenereta za kuzalishia umeme wa
dharura wa Megawati 100.
6.4 Uwezo wa Richmond Kifedha, Kitaalamu, Kiutendaji
Mheshimiwa Spika, tumeeleza kuwa Richmond Development
Company LLC iliweza kuaminiwa na Serikali kufanya upembuzi
yakinifu wa kina wa mradi wa bomba la mafuta la Dar es Salaam hadi
Mwanza kwa kujitambulisha kuwa:
(a) Kampuni hiyo ina uzoefu mkubwa wa zaidi ya miaka 25 katika
kuendeleza miradi ya nishati;
(b) Kampuni hiyo inaaminiwa na taasisi mbalimbali za biashara na
fedha za Marekani na ina mahusiano ya karibu na Serikali ya
Marekani;
(c) Kampuni hiyo imekamilisha miradi mikubwa ifuatayo duniani:
kituo cha umeme cha MW 130 cha Gaziantep, Uturuki (gharama za mradi $117 milioni) na utafutaji wa mafuta na gesi kusini mashariki mwa Ulaya ($150 million).
Mheshimiwa Spika, Serikali ingejaribu kuzichunguza sifa hizo za
rejareja za Richmond Development Company LLC hata kwa
kuuandikia Ubalozi wa Marekani Dar es Salaam au kukagua tovuti
yake (
www.rdevco.com), ukweli ungelidhihirika kuwa “kampuni” hiyo
si chochote wala lolote. Tovuti yake yenyewe imesheheni makosa
madogo madogo ya Kiingereza na kupambwa na taarifa za juu juu za
miradi ambayo “kampuni” hiyo inadai kuitekeleza, hivyo kuzua
maswali mengi na hali inayoashiria upeo mdogo kielimu wa wamiliki
wa kampuni hiyo.
Kwa mfano ukurasa wa kwanza wa tovuti hiyo iliyoandaliwa mwaka
2004 unabeba dhamira mbili za “kampuni”, lakini dhamira ya kwanza
haieleweki, inahitaji mpangilio mpya wa sentensi kwa Kiingereza
sanifu. Mbali na makosa madogo madogo ya kisarufi na mpangilio,
ambayo yamepamba kurasa zote 11 za tovuti hiyo, ukurasa wa 7
unaorodhesha miradi mbalimbali ambayo “kampuni” hiyo ilikuwa
inatekeleza: ujenzi wa uwanja wa kisasa wa michezo unaoweza
kuchukua watazamani 65,000; ujenzi wa bomba la mafuta la
kilometa 1,150 na ukarabati wa viwanja mbalimbali vya ndege nchini
Tanzania. Miradi yote hiyo ilikuwa porojo tupu ambazo watendaji
wetu Serikalini hawakustahili kuzifumbia macho.
Mheshimiwa Spika, kama ilivyotarajiwa, “kampuni” hiyo ikashindwa
kutekeleza sehemu yake ya mkataba. Mashahidi kadhaa walioongea na Kamati Teule wakati wa uchunguzi, walisema ingelikuwa maajabu kwa “kampuni” ya aina hiyo iliyokuwa haina uwezo kifedha hata wa kuwasafirisha wawakilishi wao kwenda Afrika ya Kusini kwa
mazungumzo ya kutafuta fedha za mradi, kampuni iliyokuwa haina
uelewa stahili wa masuala ya nishati na iliyokosa rekodi nzuri ya
utendaji, kufanikisha mradi huo.
Kwa hali ya kawaida, kampuni yoyote inayoshindwa kutekeleza
masharti ya mkataba na Serikali, inalazimika kukaa pembeni kwa
muda kusubiri angalau mapungufu yake yasahaulike kidogo. Aidha
muda ambao kampuni hiyo itakuwa imekaa pembeni utachukuliwa na
waungwana kuwa wa kujisahihisha, wa kurekebisha mapungufu na
kuweza kuaminiwa tena. Lakini si kawaida kwa kampuni iliyoshindwa
kutekeleza kazi moja ya mteja kurejea muda mfupi baadaye kutafuta
kazi nyingine tena yenye unyeti mkubwa kwa mteja huyohuyo bila
kigugumizi wala soni.
Hivyo basi, Mheshimiwa Spika, kwa Richmond Development Company
LLC kuingia kwenye mchakato wa zabuni nyingine ya Wizara ya
Nishati na Madini hata kabla wino kwenye barua iliyoandikiwa na
Wizara ikilalamikia utendaji kazi wake haujakauka sawasawa, na kwa
Wizara kufumbia macho ubabaishaji bayana wa “kampuni” hiyo na
kuiruhusu kushiriki kwenye zabuni ya umeme wa dharura inayohitaji
uzoefu maalum bila wasiwasi wa madhara ambayo yangeweza
kutokea kwa Taifa, hisia za maslahi binafsi ya baadhi ya viongozi wa
Serikali hazikwepeki.
7.0 HI TI MI SHO NA MAPENDEKEZO
7.1 Hitimisho
Mheshimiwa Spika, Kamati Teule imeuchambua kwa kina mchakato
mzima wa zabuni ya uzalishaji umeme wa dharura ulioipa ushindi
Richmond Development Company LLC ya Houston, Texas, Marekani mapema mwaka 2006 ili kuzitolea majibu yaliyokamilika hadidu rejea zote sita ambazo Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa
Tanzania, Mheshimiwa Samuel J. Sitta(Mb), aliipa Kamati Teule
tarehe 15 Novemba, 2007 mjini Dodoma.
Mheshimiwa Spika, kurasa zote 165 za Taarifa kubwa ya Uchunguzi
ya Kamati Teule ambayo inatokana na kazi kubwa ya kuwahoji jumla
ya mashahidi 75, kuwauliza maswali 2,717 na kupitia nyaraka 104,
zimebeba ushahidi usio na mashaka yoyote kwamba Wizara ya
Nishati na Madini, iliibeba Richmond Development Company LLC
kutoka mwanzo wa mchakato wa zabuni hadi mwisho. Kwa kufanya hivyo Wizara, kwa kutokufuata misingi ya utawala bora, ikachangia kwa kiasi kikubwa urefushaji wa mgao wa umeme ulioathiri shughuli mbalimbali za kiuchumi na kijamii nchini.
Kamati Teule imeridhika kuwa ukiukwaji huo unaweza kuwa
ulichangiwa na hoja ya kukidhi maslahi binafsi. Pengine ndiyo sababu
ya Wizara hii kuonyesha tabia ambayo haikuonyeshwa na Wizara
zingine ya kukataa katakata kuiruhusu Kamati Teule kuona majalada
ya Wizara hiyo yenye mawasiliano kuhusu zabuni hiyo.
Mheshimiwa Spika, kwa muhtasari tu, tumeonyesha katika Sehemu
ya Pili ya Taarifa hii jinsi Wizara ya Nishati na Madini ilivyopindisha
maamuzi ya Baraza la Mawaziri kwa kusitisha mpango uliokuwa
umekaribia utekelezaji wa kuzalisha umeme kupitia mitambo ya
kukodi ya kampuni ya CDC Globeleq bila kuufikisha ujumbe wa
Serikali kwa kampuni hiyo wa kurekebisha masharti yao ili mradi huo
utekelezwe. Hayo yamefanyika siku ileile Baraza la Mawaziri limetoa
maagizo na siku nne baada ya kuanza mgao wa umeme kwa mikoa
yote ya Tanzania Bara inayounganishwa na Gridi na Taifa.
Tumeonesha vilevile maamuzi yenye jeuri na kiburi ya kukiuka kwa
makusudi Sheria ya Ununuzi wa Umma ya mwaka 2004 na Kanuni
zake za mwaka 2005, licha ya Baraza la Mawaziri kusisitiza kwamba
Sheria ya Ununuzi wa Umma na kanuni zake izingatiwe. Kama vile
Wizara hiyo haihusiki kabisa na utawala wa sheria na utawala bora,
ikailazimisha TANESCO isiheshimu ushauri wa kitaalamu wa Mamlaka
ya Udhibiti wa Ununuzi wa Umma (PPRA) na kuingilia mchakato wa
zabuni wa procurement entity nyingine kwa kuiweka pembeni Bodi ya
Zabuni ya TANESCO, kuiagiza TANESCO ivunje sheria kwa
kuwabadilisha wajumbe wa Bodi yake ya Zabuni na Wizara kufanya
maamuzi ya ununuzi kwa niaba ya TANESCO na kuulazimisha uongozi
wake kusaini mkataba na kampuni ambayo TANESCO waliikataa mara
tatu kwa vigezo vya kitaalamu kuwa haifai kwa kazi hiyo. Huo
ulikuwa udhalilishaji mkubwa wa viongozi na watendaji ndani ya
TANESCO.
Mheshimiwa Spika, tumebainisha kuwa mwezi mmoja tu kabla ya
hiyo zabuni ya kuzalisha umeme wa dharura, Wizara ya Nishati na
Madini ilikuwa imeiandikia Richmond Development Company LLC
kuitaarifu kuwa imeshindwa kutekeleza mkataba baina yake na
Wizara kuhusu mradi wa bomba la mafuta. Kimya cha Wizara kuhusu
udhaifu wa Richmond Development Company LLC, kuliipa Kamati
Teule mashaka kuhusu uadilifu wa viongozi wa Wizara hiyo.
Tumeonyesha vilevile kuwa Richmond Development Company LLC
ilikingiwa kifua na kufunguliwa kila mlango na Wizara: majaribio ya
Richmond Development Company LLC kubadilisha masharti ya Barua ya Dhamana ya Benki (LC) yaliungwa mkono na Wizara ya Nishati na Madini kwa hamasa kubwa kiasi cha kupuuza maelekezo ya Wizara ya Fedha kwa kulazimisha kufanya mabadiliko katika LC hiyo nje ya mkataba wa makubaliano wa fedha kwenye akaunti ya
escrow.(Tumenukuu na kuambatanisha kwenye Taarifa hii barua
mbili zilizoandikwa na Wizara hizi mbili tarehe 6 Oktoba, 2006
zikionesha hamasa iliyoigubika Wizara ya Nishati na Madini kuisadia
Richmond bila hata kujali maslahi ya Taifa). Tumeonyesha hata jinsi
Richmond Development Company LLC ilivyoanza kazi bila
kujiandikisha Bodi ya Usajili ya Makandarasi na wahandisi wake
kuacha kujiandikisha Bodi ya Usajili ya Wahandisi na jinsi Wizara ya
Nishati na Madini ilivyokuwa wima kuitetea kampuni hiyo ya
Kimarekani. Aidha, Kamati Teule imejionea jinsi Richmond
Development Company (T) Ltd, kampuni tanzu ya Richmond
Development Company LLC, ilivyopata Cetificate of I ncentives kutoka
Tanzania I nvestment Centre bila kukidhi masharti ya msingi kama
vile ushahidi wa mtaji wa kutosha kutekeleza mradi.
Hatimaye, Mheshimiwa Spika, TANESCO walipotaka kuuvunja
mkataba kati yao na Richmond Development Company LLC kwa
kampuni hiyo ya Kimarekani kushindwa kutekeleza sehemu yake ya
mkataba na kwa kutoa taarifa za uongo kuhusu hadhi ya kampuni
hiyo, ni Wizara ya Nishati na Madini iliyoingilia kati na, bila aibu,
“kuwezesha” mkataba huo urithiwe na kampuni nyingine katika
kipindi ambacho nchi ilikuwa haihitaji kabisa umeme wa ziada licha
ya kuwepo fursa za wazi kisheria kwa TANESCO kuvunja mkataba
huo bila ya athari za hasara zozote.
Mheshimiwa Spika, ubebwaji wa Richmond Development Company
LLC na Wizara ya Nishati na Madini ulichangiwa na kurahisishwa zaidi
na ukosefu wa umakini wa maafisa ndani ya Ofisi ya Mwanasheria
Mkuu wa Serikali ambao, badala ya kuwa washauri wa sheria wa
Serikali, wanageuka kuwa wasindikazaji! Taarifa hii imesheheni
mifano ya matukio mbalimbali ya majadiliano ambayo Mwanasheria
wa Serikali au wawakilishi wake hawafiki, hivyo kukosa uelewa
mpana wa michakato mbalimbali. Hata wakifika, mchango wao wa
kuilinda nchi dhidi ya vifungu vya sheria vya kutumaliza, hauonekani.
Mheshimiwa Spika, katika suala hili la Richmond Development
Company LLC, Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali ilichangia sana
kulea ubabaishaji kwa kutohudhuria vikao vya majadiliano na
kufumbia macho dosari bayana au pengine kutojali. Mahojiano ya
Kamati Teule na Mwanasheria Mkuu wa Serikali na Mwakilishi wake kwenye majadiliano ya mikataba, yanajieleza yenyewe katika Taarifa Rasmi za Bunge (Hansard) za tarehe 30 Novemba, 2006 na tarehe 5 Disemba, 2007. Ulikuwa wajibu wa Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali kugundua kuwa Richmond Development Company LLC si
kampuni yenye ukomo wa hisa; ulikuwa wajibu wa Ofisi ya
Mwansheria Mkuu wa Serikali kuieleza Wizara ya Nishati na Madini
kuwa Sheria ya Ununuzi wa Umma inataka kampuni inayoshinda kwa
kigezo cha bei ya chini kufanyiwa post qualification, uchunguzi wa kina baada ya kuteuliwa; ulikuwa wajibu wa Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali kuishauri Serikali kuwa business card na karatasi walizoonesha Richmond Development Company LLC haviwezi kuwa mbadala wa consortium agreement kati yake na Pratt & Whitney ya utekelezaji wa mradi huo wa umeme.
Mheshimiwa Spika, utetezi mkuu uliotolewa na viongozi wa Wizara ya Nishati na Madini ni kwamba nchi ilikuwa katika dharura, hivyo ilibidi Wizara ichukue hatua ilizochukua na kwamba kanuni ya 42 ya Public Procurement (Goods, Works, Non-consultant Services and Disposal of Public Assets by Tender) Regulations, 2005 inairuhusu Wizara
kuingilia kati mchakato kwenye taasisi yake. Kamati Teule iliyakataa
maelezo haya kwani yanapotosha maana halisi ya emergency
procurement chini ya Kanuni ya 42. Ni kweli kuwa kanuni hiyo inatoa
mwanya na uhuru mpana zaidi wa maamuzi, lakini uhuru huo ni kwa
taasisi yenyewe. Ni makosa kwa taasisi moja ya ununuzi
(procurement entity) kuingilia maamuzi ya procurement entity
nyingine kwa kisingizio cha dharura kama Wizara ya Nishati na
Madini ilivyofanya. I kiwa Wizara ilitaka ifanye kazi hiyo yenyewe, kwa
nini basi isisaini mkataba na Richmond Development Company LLC
yenyewe as a procurement entity, badala yake kuibambikizia
TANESCO mzigo ambao haukuwa wake?
Mheshimiwa Spika, Kamati Teule sasa inaelewa chimbuko la tabia
mbaya iliyoenea nchini ya ajali ikitokea watu kukimbilia kusaidia.
Lakini si wote wenye dhamira ya kusaidia, kuokoa. Baadhi yao lengo
kuu ni kuiba, kupora! Viongozi tunaobuni miradi kutokana na
majanga ya kitaifa, hatuna tofauti na watu wanaokimbilia ajali kama
waokoaji kumbe wezi. Ukame nchini ulitabirika, lakini hatukuchukua
hatua mapema pengine kwa kusubiri janga kubwa litokee ili kupata
fursa ya miradi ya akina Richmond.
Mheshimiwa Spika, Kamati Teule iliyaona mawasiliano ya karibu kati
ya Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati na Madini katika hatua
mbalimbali za zabuni hiyo. Kwa kuwa Waziri wa Nishati na Madini
aliyekuwepo awali, Mhe.Dk. I brahim Msabaha(Mb) na Katibu Mkuu
wa Wizara hiyo, Ndugu Arthur Mwakapugi, hawakukiri kutumwa au
kuagizwa kuibeba kampuni hiyo ya Kimarekani, kwa mfumo wa
uongozi na utawala bora wanawajibika wenyewe kama ambavyo
Waziri Mkuu atapimwa wadau kivyake.
Mheshimiwa Spika, ifikapo mwaka 2025, Tanzania inatakiwa iwe
imeondoka kwenye kundi la nchi za kipato cha chini (low-income
countries) na kuingia katika kundi la nchi za kipato cha kati (middle-
income countries). Kipato cha Watanzania kinategemewa kupanda
kutoka Dola za Kimarekani 210 kwa mwaka kilichopo sasa hadi Dola
za Kimarekani 3,420 kwa mwaka. Kwa fedha ya Tanzania ni kutoka
sh. 262,500/ = hadi sh. 4,275,000/ = kwa mwaka. Kama Rais wetu wa
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania anavyosema: maisha bora kwa
kila Mtanzania yanawezekana, kila mtu atimize wajibu wake.
Moja ya sifa kuu za nchi za kipato cha kati ni kilimo cha kisasa na
maendeleo ya kati ya viwanda, shughuli ambazo haziendi bila nishati
ya kutosha na ya bei nafuu. Msingi wa kujenga uwezo wa kutosha wa
nishati ili kuendeshea viwanda, unatakiwa uanze kujengwa sasa na si
baadaye. Kamati Teule inakubaliana na ushauri uliotolewa na Kamati
ya Uwekezaji na Biashara katika Taarifa yake kwa Bunge kwa mwaka
2006 kuwa Serikali sasa iandae mpango madhubuti wa muda wa kati
na muda mrefu (power system master plan) ukionesha ni namna gani nchi itatekeleza na kukabiliana na tatizo la mfumo mzima wa uzalishaji na usambazaji wa umeme.
Mheshimiwa Spika, mpango wa aina hii utaipunguzia Serikali
gharama ya kuingia mikataba ya dharura mara kwa mara kila
kukitokea ukame. Aidha mpango huo ujumuishe pamoja miradi kama
ya Stieglers George ya kuzalisha umeme wa MW 2100 na zaidi,
makaa ya mawe ya Mchuchuma, umeme wa nishati ya gesi asilia,
upepo, jua, taka n.k. Hapo tutakuwa tumejijengea msingi mzuri wa
kupokea changamoto za maendeleo ya nchi za kipato cha kati.

7.2 Mapendekezo ya Kamati Teule
Mheshimiwa Spika, Kutokana na uchunguzi wa kina tuliuainisha
katika taarifa hii, Kamati Teule imejiridhisha na hivyo inatamka
bayana mbele ya Bunge Tukufu kuwa mchakato wa zabuni ya
kuzalisha umeme wa dharura wa MW 100, uliopelekea Richmond
Development Company LLC kuteuliwa na hivyo kusaini mkataba na
Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) tarehe 23 Juni 2006 na
baadaye kurithiwa na Dowans Holdings S.A tarehe 23 Desemba
2006, uligubikwa na vitendo vya ukiukwaji taratibu, kanuni na sheria
za nchi na hivyo kujenga kiwingu cha mashaka ya upendeleo,
ubadhirifu na rushwa ambavyo vimechangia kumuongezea
mwananchi mzigo wa gharama za umeme. Aidha, Kamati Teule
imethibitisha bila ya shaka lolote kuwa uteuzi wa Kampuni dhaifu
kifedha, kiufundi na kiuzoefu na ambayo haina usajili Marekani wala
Tanzania kama kampuni yenye ukomo wa hisa, yaani Richmond
Development Company LLC, ulitokana na kubebwa bila woga wala
aibu na viongozi waandamizi wa Serikali. Kutokana na msingi huo
Kamati Teule inapendekeza yafuatayo:
(1) Sheria ya Ununuzi wa Umma ya Mwaka 2004 (Public Procurement
Act, 2004) haina nguvu ya kutosha ya kuiwezesha Mamlaka ya
Udhibiti wa Ununuzi wa Umma (PPRA) kutekeleza majukumu yake ya
kuhakikisha kwamba Ununuzi wa Umma unaboreshwa kwa kuongeza
ushindani wa ukweli na uwazi na hivyo kuipa Serikali thamani halisi
ya pesa zake. Kamati Teule inapendekeza kwamba sheria hii ipitiwe
upya ili kuiboresha kwa kuipa Mamlaka nguvu zaidi za udhibiti na
uwezo wa kuchukua hatua pale Sheria na Kanuni zinapokiukwa,
badala ya kutoa ushauri tu kama ilivyo sasa.
(2) Mamlaka ya Udhibiti wa Ununuzi wa Umma isiwajibike Wizara ya
Fedha ambayo nayo ni taasisi ya ununuzi (procurement entity)
badala yake iwe chombo huru kinachowajibika Ofisi ya Rais na taarifa
zake kuwasilishwa Bungeni.
(3) Mkataba kati ya TANESCO na Richmond Development Company
LLC na sasa Dowans Holdings S.A, kama ilivyo mikataba kati ya
TANESCO na I PTL, SONGAS, AGGREKO na Alst om Power Rent als
inatoa unafuu usiostahili kwa makampuni hayo ya umeme na
kuiumiza TANESCO na hatimaye watumiaji na walipa kodi kimapato,
k.m mikataba hiyo kuwa na vipengele vya kuibana TANESCO
kuyalipia makampuni hayo kodi zinazohusika na uendeshaji
(operations), matengenezo/ marekebisho ya mara kwa mara ya
mitambo (maintenance) gharama za bima, ada za mawakili na
washauri elekezi (consultants) gharama za mafuta na gesi ya
kuendeshea mitambo, gharama za ukodishaji mitambo (capacity
charges) ambazo TANESCO hulipa kila mwezi si chini ya wastani wa
shilingi bilioni 2 kwa kila kampuni, izalishe au isizalishe umeme.
Kamati Teule inatoa rai kwa Serikali kuwa mikataba yote hii ipitiwe
upya mapema iwezekanavyo kama ambavyo mikataba ya madini
inavyopitiwa upya sasa na Serikali. Bila kufanya hivyo, mzigo
mkubwa wa gharama za umeme utawaelemea wananchi na
kushindwa kufikia azma ya Serikali ya maisha bora kwa kila
Mtanzania.
(4) Mkataba kati ya TANESCO na Richmond Development Company
LLC ulikuwa wa uzalishaji umeme wa dharura kipindi ambacho nchi
ilikuwa katika hali ngumu ya ukame uliokausha mabwawa yote ya
kuzalishia umeme. Kamati Teule inaitaka Serikali kutathmini upya
uhalali wa kuwepo na kuendelea kuwepo na mkataba huo kutokana
na udanganyifu bayana uliofanywa na Richmond Development
Company LLC kuhusu uwezo wake kifedha, kiufundi, na uzoefu wake
katika masuala ya uzalishaji umeme; usajili na uwepo wake kisheria
kama kampuni halali yenye ukomo wa hisa nchini Marekani na
Tanzania; uhusiano wake kisheria na Kampuni kubwa ya Kimataifa ya
Pratt & Whitney na utambulisho wa Mzungu mmoja kwa jina la John
Perun kama mwakilishi wa Pratt & Whitney, mambo ambayo
Kampuni hiyo kubwa ya Kimataifa imeyakanusha vikali.
(5) Mkataba kati ya TANESCO na Richmond Development Company
LLC na sasa Dowans Holdings S.A umesheheni makosa mengi ya
kisheria yanayoashiria udhaifu mkubwa wa kitaalamu katika Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali au ukosefu wa umakini ama ubinafsi katika kuiwakilisha Serikali. Kwa mfano, kushindwa kutambua
ukosefu wa sifa za kikampuni za Richmond Development Company
LLC; kushindwa kuishauri Serikali kuifanyia kampuni hiyo ukaguzi wa
awali (due deligence) au ukaguzi baada ya uteuzi (post qualification);
kushindwa kutambua tofauti kati ya consortium agreement na
proprietary information agreement; kushindwa kuona dosari kisheria
za proprietary information agreement; kushindwa kuona tofauti
kisheria kati ya Richmond Development Company LLC,
RDEVCO,RDVECO na RDC, majina ambayo wamiliki wa Richmond
Development Company LLC walikuwa wanayatumia kwa kubadilisha
badilisha (interchangerbly) kwa makusudi; kushindwa kuwashauri
Wajumbe wa GNT kwamba business card si mbadala wa hati mahsusi kisheria; kushindwa kuishauri Serikali kuhakikisha kuwa muhtasari wa majadiliano kati ya Kamati ya Serikali ya Majadiliano (GNT) na
Richmond Development Company LLC ambao ulizingatia baadhi ya
maslahi ya nchi, uwe sehemu ya Mkataba kati ya TANESCO na
Richmond Development Company LLC; kushindwa kuishauri Serikali
kutumia fursa iliyokuwepo wazi ya kuvunja Mkataba baada ya
Richmond Development Company LLC kushindwa kutekeleza sehemu
yake ya Mkataba; kushindwa kuhudhuria idadi kubwa ya vikao
muhimu vya majadiliano;n.k. Mwanasheria Mkuu wa Serikali ambaye
katika majadiliano yake na Kamati Teule alionyesha kutokuelewa
kabisa kilichokuwa kinatendeka na wasaidizi wake, na mwakilishi wa
Mwanasheria Mkuu wa Serikali Wakili wa Serikali Donald Chidowu,
ambaye ushiriki wake katika GNT haukuwa na tija yeyote,
wawajibishwe na Mamlaka ya juu ya nchi kwa kuchangia kuiingiza
nchi katika mkataba wa aibu.
(6) Katika mikataba yote na makampuni ya nje Serikali ihakikishe kuwa Wakala wa Usajili wa Biashara na Leseni (BRELA) inatumika kikamilifu katika kupata taarifa kamili za kampuni hizo, kama vile
wanahisa, mitaji na anwani. Aidha, Ofisi zetu za Ubalozi zilizo sehemu
mbalimbali duniani zihusishwe katika majadiliano na makampuni
yanayotoka nje ya nchi kwa lengo la kupata taarifa zao za msingi na
kuboresha nguvu ya hoja ya Serikali.
(7) Madhumuni ya Mkataba kati ya TANESCO na Richmond
Development Company LLC yalikuwa kuzalisha umeme wa dharura
kwa kipindi cha miezi kumi na mbili (12) tu.
Muda huo ungeweza kuongezwa baada ya kutathmini hali ya
ongezeko la maji katika mabwawa ya kuzalishia umeme nchini. Kabla
ya muda wa tathmini hiyo haujafikiwa, wakati majadiliano
yakiendelea GNT ikaongezea Richmond Development Company LLC muda wa kukodi mitambo hiyo kuwa miaka miwili (2). Kamati Teule haikuona vielelezo vyovyote vilivyojenga uhalali kwa GNT kuongeza muda huo. Uamuzi huo umeliongezea Taifa mzigo mkubwa wa
gharama zisizokuwa za lazima. Mathalan, kwa upande wa capacity
charges tu, TANESCO itailipa Dowans Holdings S.A jumla ya shilingi
bilioni 54.8 kwa kipindi kilichongezwa cha mwaka mmoja. Aidha, GNT
ilishindwa kutambua ulaghai wa Richmond Development Company
LLC kuhusu mwakilishi wa Pratt & Whitney na hivyo kuamini karatasi
ambayo ilikuwa haijathibitishwa na mawakili na diskette zenye picha
za mitambo ya Pratt & Whitney, vielelezo ambavyo Kamati Teule
imegundua na kuthibitisha kuwa vilikuwa vya kugushi. Vilevile, bila
kujali kwamba TANESCO ingelezimika kuilipa Richmond Development
Company LLC shilingi milioni 152 kwa siku kama gharama ya kuweka
vifaa vyao nchini, GNT ikakubali kilegelege kuitoza Richmond
Development Company LLC shilingi milioni 12 tu kwa siku kama fidia
kwa ucheleweshaji wa kuanza kuzalisha umeme kulingana na tarehe
iliyokubalika kwenye mkataba. Kamati Teule inapendekeza kuwa
Wajumbe wote wa GNT ambao ni maafisa waandamizi wa Serikali
wawajibishwe mara moja kwa kushindwa kutumia elimu na ujuzi wao
kulinda maslahi ya Taifa.
(8) Pamoja na Uongozi wa TANESCO kubainisha mapungufu ya
Richmond Development Company LLC na kutoa notisi tarehe 27
Octoba 2006 ya kusitisha Mkataba tena kwa ushauri mahsusi kutoka
Kampuni ya Kimataifa ya Mawakili, Wizara ya Nishati na Madini
haikuupenda mwelekeo huo hivyo tarehe 28 Novemba 2006 baadaye
Waziri wa Nishati na Madini Mhe. Nazir Karamagi, Mb akiwa nje ya nchi Calgary, Canada alimuagiza Mwenyekiti wa Bodi ya TANESCO Balozi Kazaura kuangalia uwezekano wa kuhaulisha Mkataba wa Richmond kwa kampuni nyingine. Siku tano baada ya mawasiliano hayo, yaani tarehe 4 Desemba 2006, TANESCO ikapokea barua
kutoka Richmond Development Company LLC ikielezea nia ya
kampuni hiyo kutumia haki yake chini ya kifungu 15.12 cha mkataba
ili kuhamisha majukumu yake ndani ya mkataba kwenda kwa
kampuni mpya ya Dowans Holdings S.A. Kamati Teule ilipata taarifa
za ndani ya Wizara na TANESCO kuwa viongozi wa Wizara kama
kawaida yao waliishinikiza TANESCO kuridhia ombi hilo la Richmond
Development Company LLC kuhaulisha mkataba kwa Dowans
Holdings S.A. TANESCO ikalazimika kuridhia uhaulishaji wa mkataba
huu badala ya kutumia fursa iliyokuwepo ya kusitisha mkataba baada
ya kutoa notisi ya siku thelathini. Kamati Teule inaamini kwamba
uamuzi wa Wizara ya Nishati na Madini kuizuia TANESCO isitumie
fursa ya kusitisha mkataba huo, unaashiria jinsi viongozi wetu wanavyojali zaidi faida na maslahi ya makampuni ya nje kuliko maslahi mapana ya Taifa. Tarehe 3 Desemba TANESCO kama
ilivyoagizwa ikaridhia uhaulishwaji wa mkataba huo lakini kipindi ambacho hali ya maji katika mabwawa yetu ya kuzalishia umeme ilishaanza kurejea kuwa ya kawaida. Uamuzi huo umeingizia Taifa
hasara kubwa. Hivyo basi Kamati Teule inapendekeza kwamba Waziri
wa Nishati na Madini Mhe. Nazir Karamagi, Mb aliyeshabikia sana
uhaulishaji huo, awajibishwe.
(9) Matokeo ya uchunguzi ya Kamati Teule kama yalivyoainishwa
hapo juu yanadhihirisha wazi jinsi Taifa lilivyotumbukizwa kwenye
hasara kubwa kutokana na mkataba huo wa Richmond Development
Company LLC na Dowans Holdings S.A, kinyume na taarifa
iliyotolewa na TAKUKURU (wakati huo TAKURU) kwamba Taifa
halikupata hasara yoyote. Taarifa ya TAKUKURU ililenga kuficha
ukweli (white wash) hivyo ikaishia kujikanganya kwa kukiri kuwepo
kwa mapungufu lakini yasiyokuwa na athari. Taarifa hiyo
imemong’onyoa kwa kiasi kiasi kikubwa hadhi na heshima ya chombo
hiki muhimu cha kitaifa kilichopewa dhamana ya kupambana na
rushwa na sio kuipamba ili kurejesha heshima ya umma katika taasisi
hiyo. Kamati teule inapendekeza mabadiliko ya haraka ya uongozi wa
taasisi hiyo.
(10) Taratibu za malipo ya madai ya mkataba wa umeme wa dharura zinafanywa kupitia Barua ya Dhamana ya Benki iliyofunguliwa kati ya TANESCO na benki ya CRDB ya dola za Kimarekani milioni
30,696,598 iliyofunguliwa tarehe 27 Desemba 2006. Kamati Teule
imethibitisha kwamba hadi kufikia tarehe 19 Juni 2007 malipo
yaliyolipwa na Benki Kuu yamefikia Dola za Kimarekani 35,561,598
kiasi hicho ni zaidi ya Barua ya Dhamana ya Benki kwa dola za
kimarekani milioni 4,565,000 wastani wa shilingi bilioni 5.7. Kamati
Teule inashangaa ni vipi Benki Kuu iidhinishe malipo hayo
nje ya Barua ya Dhamana ya Benki iliyofunguliwa kati ya TANESCO,
CRDB Bank na Dowans Holdings S.A. Kwa kuwa Benki Kuu ndio
msimamizi mkuu wa akaunti maalum (Escrow Account), Gavana wa
Benki Kuu pamoja na Bodi ya Wakurugenzi wachunguze kwa makini
uhalali wa malipo hayo na kuhakikisha kwamba udhaifu wa namna hii
haujitokezi tena hapo baadaye.
(11) Wakati umefika sasa kwa Sheria ya Maadili ya Viongozi wa
Umma ya mwaka 1995 (Public Leadership Code of Ethics Act)
ifanyiwe marekebisho makubwa ili kudhibiti utaratibu unaonekana wa
kawaida sasa wa viongozi waandamizi wenye dhamana kisiasa
kuendelea na biashara zao wakiwa madarakani, hivyo kuwaweka
kwenye mtihani mkubwa wa mgongano wa kimaslahi katika maamuzi
yao. Tufike mahali ambapo sheria iwalazimu kuchagua kati ya
Utumishi wa Umma au biashara binafsi. Viongozi waandamizi wenye
dhamana kisiasa (mawaziri na kuendelea) kuendelea na biashara zao
wakiwa madarakani hivyo kuwaweka kwenye mtihani mgumu wa
mgongano wa kimaslahi.
(12) Serikali iondokane kabisa na utaratibu wa kutumia mawakala
katika ununuzi wa mitambo ya kuzalisha umeme nchini na
kuhakikisha kuwa Wizara husika ina taarifa za bei halisi ya mitambo
kila wakati ili kujiepusha na mchezo wa kawaida wa mawakala
kupandisha bei mara mbili au zaidi ya bei halisi. Kamati Teule
ilishuhudia bei za mitambo hiyo jijini Houston, Texas Marekani kwa
watengenezaji kiwandani ikiwemo kampuni ya Kawasaki Gas Turbines
– Americas ambayo iko chini ikilinganishwa na bei zinazotolewa na
mawakala hao, jambo ambalo lingeiwezesha Serikali kununua na
kumiliki badala ya kukodi kwa muda mfupi na kwa gharama kubwa.
Mathalan, MW 105 zingepatikana kwa kununua mitambo sita ya MW
17,5 kila mmoja kwa gharama ya shilingi bilioni 56.25 badala ya
shilingi bilioni 108.7 tulizotandikwa na Richmond Development
Company LLC mitambo hiyo ikibaki mali ya wakodishaji. Kwa
kumalizia Kamati Teule ilithibitisha kwamba kauli iliyokuwa inatolewa
mara kwa mara na baadhi ya viongozi wote tuliowahoji kwamba
kipindi hicho cha ukame haikuwa rahisi kupata mitambo hiyo na
ilikuwa ikigombaniwa na nchi nyingi kauli hiyo ilikuwa sio ya ukweli
na upotoshaji mkubwa.
(13) Utaratibu tuliourithi kutoka kwa wakoloni na kuuzoea wa kuiona mikataba ya kibiashara kuwa ni siri hata kwa walipa kodi wenyewe na kuwa uwanja wa pekee wa watendaji, ambao Waziri wa Mipango
Uchumi na Uwezeshaji Mhe. Dk Juma Ngasongwa (Mb) aliusifia
bungeni tarehe 19 Aprili 2007 kuwa best practice wakati akijibu swali la Mhe. Masolwa C. Masolwa (Mb) Mbunge wa Bububu, umepitwa na wakati na unakiuka misingi ya demokrasia na uwajibikaji. Matokeo ya utaratibu huu ni kuwepo kwa mikataba mibovu inayoficha vipengele
vinavyoibebesha Taifa mizigo mikubwa ya gharama zisizokuwa za
lazima kama tulivyoainisha katika pendekezo namba 3 hapo juu.
Kamati Teule inatoa wito kwa Serikali kuondokana na utaratibu huu
usio na tija kwa kuzihusisha Kamati za Kudumu za Bunge kwenye
hatua za awali za maandalizi ya mikataba hiyo. Aidha, Kamati Teule
inatoa wito kwa Kamati zote za Bunge zihakikishe kuwa zinapitia
mikataba mikubwa nay a muda mrefu ya kibiashara chini ya sekta
zao ili kuliondolea Taifa mizigo isiyo ya lazima. Pale ambapo
upatikanaji wa mikataba hiyo unakwamishwa kwa urasimu usio wa
lazima Kamati zitumie utaratibu uliotumiwa na Kamati ya Bunge ya
Uwekezaji na Biashara ya kuunda Kamati Teule yenye ufunguo wa
mikataba iliyofichika.
(14) Pamoja na dharura iliyokuwa inalikabili Taifa, Serikali haiwezi
kuwa kinara wa uvunjaji wa taratibu, kanuni na sheria za nchi kwa
makusudi. Kamati Teule imeanisha katika taarifa hii vitendo vya
ubabe, ujeuri na kiburi vilivyofanywa na viongozi wa Wizara ya
Nishati na Madini alimradi kampuni waliyoitaka iteuliwe kiasi cha
kupindisha hata maamuzi ya Baraza la Mawaziri bila wasiwasi
wowote, kukaidi ushauri wa kitaalamu wa Mamlaka ya Udhibiti wa
Ununuzi wa Umma mara tatu mfululizo na kinyume na maagizo ya
Baraza la Mawaziri lililotaka Sheria ya Ununuzi wa Umma izingatiwe,
kukiuka sheria kwa makusudi kwa kuingilia mchakato wa zabuni wa
taasisi nyingine ya ununuzi, kuvipuuza vyombo vya ndani vya
maamuzi vya TANESCO (Bodi ya Wakurugenzi, Bodi ya Zabuni n.k),
kuilazimisha Bodi na Menejimenti ya TANESCO kuridhia maamuzi
yaliyofanywa na Wizara ya kuibeba Richmond Development Company
LLC kinyume cha sheria na taratibu n.k. Wizara hiyo katika kuibeba
Richmond Development Company LLC ilifikia hatua ya kupotosha kwa
makusudi ushauri wa Wizara ya Fedha uliozuia malipo ya awali ya
Dola za Kimarekani Milioni 10 katika Barua ya Dhamana ya Benki ya
Richmond Development company LLC. Siku iliyopotosha ilikuwa
tarehe 6 Octoba 2006. Kamati Teule inapendekeza kwamba Waziri
wa Nishati na Madini wa wakati huo Mhe. Dk. I brahim Msabaha (Mb)
na Katibu Mkuu Ndugu Arthur Mwakapugi wachukuliwe hatua kali za
kinidhamu kwa kuliingiza Taifa kwa makusudi kwenye mkataba na
kampuni ya mfukoni ambao umesababisha hasara kubwa kwa nchi.
Aidha Kamishna wa Nishati Ndugu Bashir Mrindoko naye achukuliwe
hatua za kinidhamu kwa kushindwa kumshauri Katibu Mkuu mpya wa
Wizara kuhusu udhaifu wa Richmond Development Company LLC
ambao ulijulikana dhahiri na Wizara toka mwaka 2004 kwenye
mkataba wa Bomba la Mafuta. Ndugu Mrindoko ndiye aliyeiandikia
barua kampuni hiyo kusitisha mkataba wake na Serikali mwezi
mmoja tu kabla ya mchakato wa zabuni ya umeme wa dharura
haujaanza.
(15) Utaratibu wa kuteua wakurugenzi na makamishna katika Wizara
kuwa wajumbe wa bodi za wakurugenzi za mashirika yaliyo chini ya
Wizara, unazua mgongano wa kimaslahi, kudhoofisha usimamizi na
uwajibikaji, hivyo Serikali iupige marufuku mara moja. Mfano
Kamishna wa Nishati ni Mjumbe wa Bodi ya Wakurugenzi ya
TANESCO ambaye alishiriki kwenye kikao kilichowakataa wazabuni
wote kuwa hawafai na kuishauri Serikali vilivyo, aliporejea Wizarani
alishiriki katika kutengua maamuzi ya Bodi ya TANESCO.
(16) Uhuru mkubwa ambao viongozi wa Wizara ya Nishati na Madini
waliutumia bila wasiwasi katika kuhakikisha kwamba kampuni
waliyoitaka, Richmond Development Company LLC, inapewa zabuni
ya umeme wa dharura; maelekezo ya mara kwa mara ya Waziri Mkuu kwa Wizara katika kila hatua ya mchakato huo; upendeleo wa dhahiri ambao Richmond Development Company LLC iliupata kutoka taasisi mbalimbali za Serikali k.m Kituo cha uwekezaji (TI C) ambacho kilifikia hatua ya kufumbia macho baadhi ya taratibu zake za msingi ili kuipa kampuni tanzu ya Richmond Development Company LLC cheti cha
uwekezaji haraka iwezekanavyo; kutotimiza masharti ya Bodi za
Makandarasi na Wahandisi na Wizara ya Nishati na Madini kuikingia kifua kampuni hiyo isichukuliwe hatua za kisheria; uteuzi wa mwisho wa Richmond Development Company LLC kuwa mkandarasi
kufanywa na Waziri Mkuu mwenyewe tarehe 21 Juni 2006; uamuzi
wa kuiteua Richmond Development Company LLC kuwa mkandarasi kusafishwa na TAKURU ( sasa TAKUKURU) kuwa ulikuwa wa wazi na wa haki; uamuzi wa Serikali kuizuia TANESCO isivunje mkataba na kampuni hiyo licha ya sababu zote kisheria kuwepo, ni baadhi tu ya viashiria vya nguvu kubwa iliyo juu ya Wizara ya Nishati na Madini kutumika katika suala hili na Kamati Teule kutokana na ushahidi wa kimaandishi, kimazingira na wa mdomo, inaiona nguvu hiyo kuwa ni Waziri Mkuu.
I bara ya 52 ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya
Mwaka 1977 inatamka wazi kuwa Waziri Mkuu ndiye mwenye
madaraka ya juu ya udhibiti, usimamiaji, utekelezaji wa siku hadi siku
wa kazi na shughuli za Serikali ya Jamhuri ya Muungano na ndiye
Kiongozi wa shughuli za Serikali Bungeni. Kamati Teule
haikufurahishwa hata kidogo na taarifa hizo zinazomgusa moja kwa
moja Mhe. Waziri Mkuu katika kuipendelea Richmond Development
Company LLC. Hata hivyo Kamati Teule imetimiza wajibu wake kwa
uwazi na ukweli kama ilivyoagizwa na Bunge letu Tukufu. Kwa
kuzingatia umuhimu wa nafasi aliyonayo Mhe. Waziri Mkuu katika
uendeshaji wa shughuli za Serikali na uongozi wa nchi kwa ujumla, ni
wajibu wake yeye mwenyewe kupima uzito wa matokeo ya
uchunguzi huu na wajibu wake kikatiba ndani na nje ya Bunge. Vile
vile ni wajibu wa Bunge ambalo linathibitisha uteuzi wake kwa mujibu
wa I bara ya 51 inayothibitisha uteuzi wake. Kuangalia ikiwa matokeo
ya uchunguzi huu hayajaathiri hadhi na uzito wake ndani ya Bunge.
Mheshimiwa Spika, kwa kumalizia Kamati Teule ya Bunge
ilifadhaishwa sana na tabia ya baadhi ya watendaji wa Serikali ya
kukaidi amri ya kuwasilisha nyaraka zinazohitajika na Kamati Teule.
Kamati Teule inaliomba Bunge litafakari kitendo cha aina hii na
kufikiria hatua za kuchukua dhidi ya watendaji wa namna hiyo.
7.0 SHUKRANI
Mheshimiwa Spika, naomba kurudia kukushukuru wewe binafsi na
Bunge lako Tukufu kwa kutupa heshima hii kubwa ya kuunda Kamati
Teule ya Bunge.
Pia napenda kuishukuru Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa
Kimataifa kwa ushirikiano wake mzuri ambao uliiwezesha Kamati hii
kupata taarifa mbalimbali. Vilevile naushukuru Ubalozi wa Tanzania
wa Washington D.C, Marekani kwa kuwawezesha baadhi ya Wajumbe
wa Kamati hii waliosafiri kwenda Marekani kufanya kazi yao kwa
ufanisi. Nakishukuru Chama cha Uwekezaji cha Watanzania waishio
Marekani (Tanzanian American I nvestment Forum- TAI F) chini ya
Mwenyekiti wake Dk. Lenard Tenende kwa mapokezi mazuri ya
Wajumbe wa Kamati Teule walipozuru Houston, Texas - Marekani.
Mheshimiwa Spika, naomba vilevile nimpongeze Mwenyekiti wa
Kamati ya Uwekezaji na Biashara, Mhe. William Shellukindo (Mb) na wajumbe wake wote kwa kusimama kidete kuhakikisha kuwa kamati yao inapata majibu kupitia kamati Teule ya Bunge.
Shukrani za pekee na pongezi ziwaendee waandishi wa habari na
vyombo vyao walioweka maslahi binafsi pembeni na kupiga kelele
kwa nguvu zao zote kuhusu mwenendo uliokuwa hauridhishi wa
mchakato wa zabuni ya umeme wa dharura. Kwa niaba ya Kamati
Teule naomba, Mheshimiwa Spika, nichukue fursa hii kumpa pole
mwandishi mahiri na jasiri Saed Kubenea na mwenzake Ndimara
Tegambwage kwa mkasa wa kushambuliwa na kuumizwa vibaya na
watu tunaoamini hawafai kuitwa Watanzania.
Vilevile shukrani zetu ziende kwa Watanzania na watu wote wenye
nia njema na nchi hii waliotuunga mkono kwa kutupa taarifa
mbalimbali, maoni kwa njia ya barua pepe, simu n.k.
Kwa kumalizia namshukuru Katibu wa Bunge Ndg. Damian S.L Foka
kwa kuisadia Kamati hii kufanya kazi vizuri. Aidha, shukrani za pekee
zinatolewa kwa Katibu wa Kamati hii Ndg. Anselm Mrema
akishirikiana na Ndg. Emmanuel Mpanda, Ndg. Lina Kitosi na Ndg.
Nenelwa Mwihambi kwa kuisaidia Kamati kufanikisha kumaliza kazi hii
kwa ufanisi.
Mheshimiwa Spika, naomba kutoa hoja.
Mhe. Dk. Harrison G. Mwakyembe
MWENYEKI TI
KAMATI TEULE YA BUNGE
06 Februari 2008
.
Mh mbunge anapochungulia nyumba ya mpiga kura wake kama vile kuna simba ndani..!!.
ATCL nao wanadaiwa-mwendo wa ufisadi kwakwenda mbele Hata hivyo, ATCL ina kitanzi kingine cha mkataba wa ndege ya kukodi aina ya Air Bus A320, iliyokodiwa mwaka 2007 kwa kampuni ya Wallis Trading Inc kwa mkataba wa mia...ka sita wakati ndege hiyo ni mbovu.
Taarifa ya serikali inaonyesha kwamba gharama za kuvunja mkataba huo ni dola za Marekani milioni 18.0.
Hadi Machi mwaka huu, ATCL ilikuwa inadaiwa dola za Marekani milioni 15.5 kutokana na malimbikizo ya gharama za kuikodisha Euro milioni 1.6 zitokanazo na matengenezo makubwa na Euro 104,000 kwa ajili ya malipo kwa kampuni iliyosimamia matengenezo ya ndege hiyo.
Kuhusu mazungumzo ya namna ya kulipa deni hilo, Waziri Nundu alisema bado hajapata taarifa za kina kuhusu yanayoendelea ATCL na kwamba akishapata taarifa atajua nini cha kufanya.
Kampuni ya ATCL imekuwa na matumizi makubwa ikilinganishwa na mapato ambapo taarifa ya serikali ya Aprili ilieleza kwamba kwa kipindi cha Julai mwaka jana hadi Machi mwaka huu, mapato yalikuwa ni sh bilioni 7.8 wakati matumizi yalikuwa ni sh bilioni 26 jambo lililosababisha hasara ya sh bilioni 18.
Ni kampuni ya China Sonangol International ya China ambayo ilionyesha nia ya kutaka kuwekeza ATCL lakini ni takribani mwaka mmoja sasa tangu serikali ilipoanza mazungumzo na kampuni hiyo bila muafaka.
Kwa upande wake Mkurugnzi wa ATCL, David Mataka, amesema hatma ya kufufuka kwa Shirika la Ndege nchini (ATCL) linaloelekea kufa itajulikana wiki ijayo baada ya kikao cha pande mbili kati ya Serikali na Uongozi wa Shirika hilo.
Mataka, alisema kwamba matarajio ya Watanzania ya kuona ATCL inaanza kazi kikamilifu ni makubwa, lakini kwa sasa hataweza kuwahakikishia kitu chochote hadi hapo kikao hicho kitapokaa na kutoa maamuzi juu ya shirika hilo.
Alisema, katika mkutano huo ambao utafanyika katikati ya wiki ijayo, utaweza kutoa dira halisi ya shirika hilo kama litaanza kazi na mbia wanayemtarajia ambaye ni Shrika la Ndege la Sonongol linalomilikiwa kati ya nchi ya China na Angola au vinginevyo.
Hata hivyo, Mataka alimshukuru Rais kwa kumteua waziri Nundu kusimamia wizara ya Uchukuzi kwa kuwa ni mtu anayefahamu kwa undani masuala ya usafiri wa anga na shirika hilo kwa ujumla, hivyo anaamini Watanzania wataweza kuona mambo mazuri yakitoka ndani ya kikao hicho.
Alisema wanatarajia kujadili kwa kina mpango wa kulifufua shirikahilo(MasterPlan),ambapo uongozi huo umependekeza kuanza kwa kijitegemea zaidi kuliko kusubiri mwekezaji kutoka nje ya nchi.
"Ndani ya mpango huo sitoweza kusema tutaanza na ndege ngapi kubwa, lakini binafsi ningependa tuanze sisi wenyewe na wawekezaji iwe kama kitu cha akiba tu," alisema Mataka.
Akizungumzia harakati walizozifanya za kuhakikisha ATCL inabaki japo kwa mwendo wa kuchechemea, Mataka alieleza mpaka sasa wamebakiwa na ndege mbili tu aina ya Bomberdia-8q300 zenye uwezo wa kubeba abiria 50 kila moja.
Hata hivyo, kati ya ndege hizo, moja imeharibika na imepelekwa nchini Afrika ya Kusini kwa ajili ya matengenezo na ndege iliyobaki inaendelea kutoa huduma katika mikoa ya Dar es Salaam, Mwanza, Tabora na Kigoma.
Alisema, katika kipindi hicho kigumu wamejitahidi kuhakikisha ndege hizo zinajiendesha zenyewe, ikiwa ni pamoja na kuwezesha kununua mafuta, chakula pamoja na huduma zingine.
"Huko nyuma huduma hizo tulikuwa tunakopa, lakini kwa sasa tumefikia wakati tumeanza kulipia huduma mbalimbali muhimu katika safari za anga, kwa kweli mpaka tumefikia hapo tunaweza kusema tumejitahidi kiasi," alisema.
Aliongeza kuwa Shirika hilo kwa sasa lina jumla ya wafanyakazi 182 kati ya wafanyakazi zaidi ya 300. Waliobakia wengi wao ni wale wenye utalaam maalum wakiwemo marubani, mafundi pamoja na watu wachache wanaofanya kazi ya utawala."The jaws of power are always open to devour, and her arm is always stretched out, if possible, to destroy the freedom of thinking, speaking, and writing."
John Adams
Mh kikweteYUPO KIMYA KAMA VILE HAYA MHUSUROSTAM AZIZ NA RICHIMOND NA DOWANSCHENGE NA RADA

FEDHA ZA EPA.!!.  NA  DAUDI BALALI kweli alikufa,?? na ninani aliekabidhiwa mirathi tumshitaki kutokana na makosa ya Mh balali..!!??.

Mpaka sasa hivi serikali imefanikiwa kuokoa kiasi cha fedha kipatacho bilioni 72 za kitanzania kutoka kwenye matumizi mabaya ya Benki kuu ya Tanzania kutoka kwenye kitengo cha Tanzania's External Payments Arrears(EPA)AMBAPO bilioni 19 kati ya hizo zilipatikana baadae.
Waziri wa wizara ya fedha na uchumi Mh.Mustafa Mkulo alisema kwamba bilioni 72 hizo ni kati ya zile bilioni 133 ambazo zilitumika kwa matumizi mabaya.